Uchaguzi 2020 Bernard Membe hana kabisa mvuto!

Uchaguzi 2020 Bernard Membe hana kabisa mvuto!

Huyu jamaa, ‘jasusi mbobezi’, hana kabisa mvuto akiwa jukwaani.

Siasa kwake naona si jambo alilonalo kiasili.

Anajitahidi sana kuongea na kudondosha vibwagizo akiwa jukwaani, lakini wapi! Hamna kitu kabisa.

Maneno hayamtoki mdomoni kiulaini. Linganisha Lissu akiwa jukwaani na huyo Membe, ni usiku na mchana.

Sauti haina mvuto. Hana msamiati wa kutosha wa kuchotea vibwagizo kuendana na hadhira iliyo mbele yake.

Anachokiweza ni vijembe vya kimafumbo huko Twitter.

Umepewa macho lakini huoni, umepewa masikio lakini husikii na umepewa akili lakini huzitumii.

Kwa mwaka huu ccm lazima hesabuni vidonda tu na mjiandae kugombea KUB na akina NCCR na TLP na CUF ya Lipumba
 
Lowassa ndio hana mpinzani kwa Charisma. Yeye anapanda jukwaani anasema maneno matatu tu Elimu, Elimu, Elimu, ila shughuli yake si mchezo. Charisma yake hadi ilisababisha CCM washindwe kuiba kura Zanzibar, nguvu yote waliweka bara kupambana na mzee wa elimu

..angekuwa na uwezo wa kulitawala jukwaa sijui ingekuwaje.
 
Jamaa yuko vizuri ni mkongwe ila tu Hana Kismati, wazungu wanaita X FACTOR.
 
Juzi niliongea na mtumushi wa Mungu akaniambia kuhusu nguvu ya damu... Lissu alivyopigwa risasi Dodoma alipoteza damu yake 40% hadi madaktari bingwa wa Kenya walisema huu ni muujiza kuwa hai... Sasa watu wanaotoa kafara za wanyama na watoto wa kuwazaa hawawezi kumshinda Lissu kwenye ulimwengu wa kiroho maana Lissu katoa damu yake kama Yesu... CCM mwisho wenu umefika damu ya Lissu inaenda kuwakomboa Watanzania kwenye kivuli cha wachawi na washirikina... tafakuri
 
Lissu anawatesa sana wa kijani, now mpo kama mmenyeshewa mvua, kila mnapogusa hapashikiki. Mrudisheni Nape, naye kwa sababu kazibuka ataweza kushindana na Lissu. Polepole yeye analialia tu kwenye media.
Lissu na Nappe ni ndugu na marafiki
 
Sidhani kama fani unahusiana na chochote hapo!

Siyo kila mwanasheria ana uwezo wa kuzungumza kama Tundu Lissu!

Mfano mzuri ni Shangazi/ Fatma Karume.

Ushawahi kumsikia akiongea huyo shangazi?

Unaweza ukamlinganisha Shangazi na Zitto? Au Shangazi na Mbowe?
100% kuongea ni kipaji cha pekee na ambacho hakihusiani na elimu uliyo nayo.
Pia mfano mwingine ni Prof Lipumba, anapitwa na Kibajaji na Maukuma katika kujenga hoja
 
Membe ni Mkakatati wa Akili wa System. Sijui kwanini watanzania ni mabogus hivi. Nashangaa kusikia Chadema ikiomba Uchumba kwa ACT mnataka ushindi hakika malofa.
Mkuu kwa hiyo kupitia usajili upi wa kisasa unafaa kuendesha gari letu,

T 2020 TAL

T 2020 BCM

T 2020 JPM

Kipya kinyemi.
 
Kikwete anawazidi wote Lissu, Magufuli, Membe..

Charisma na mvuto Tz since independence ni Nyerere na Kikwete

Waliosalia wote wanababia babia
Mkuu kwa Nyerere sawa lakini kikwete ni mjanja mjanja tu hana mvuto kivile lakini anajua kucheza na akili za watu
 
Mleta mada wewe ni mvivu wa kufuatilia interviews na kampeni za wagombea.

Membe yuko vizuri sana kwenye kujenga hoja na pia delivery yake ni nzuri sana, iko composed, ina substance na ina pace nzuri

Kiufupi mada yako hii inalenga kumchafua Membe tu!

Wewe mleta mada hebu ona kipande kifupi tu cha Mwanaume hapa anavyojua kumiliki jukwaa na kutema cheche, acha maneno yako mbofu mbofu

 
Huyu jamaa, hana kabisa mvuto akiwa jukwaani.

Siasa kwake naona si jambo alilonalo kiasili.

Anajitahidi sana kuongea na kudondosha vibwagizo akiwa jukwaani, lakini wapi! Hamna kitu kabisa.

Maneno hayamtoki mdomoni kiulaini. Linganisha Lissu akiwa jukwaani na huyo Membe, ni usiku na mchana.

Sauti haina mvuto. Hana msamiati wa kutosha wa kuchotea vibwagizo kuendana na hadhira iliyo mbele yake.

Anachokiweza ni vijembe vya kimafumbo huko Twitter.


Ongeza na hiki👇
 
Mange Kimambi yalimkuta haya .... dada hatutakuangusha ... wengine wakatengeneza home made gas-mask ...siku ya siku barabara nyeupeeeeeee... wakarudi ooo tumeshinda wameandamana wao badala yetu .... 😂
Nani avunjwe mguu au apoteze hiki kipuuzi hivyo😂🤣😂 Thubuti!
 
Mange Kimambi yalimkuta haya .... dada hatutakuangusha ... wengine wakatengeneza home made gas-mask ...siku ya siku barabara nyeupeeeeeee... wakarudi ooo tumeshinda wameandamana wao badala yetu .... 😂
Nani avunywe mguu au apoteze hiki kipuuzi hivyo😂🤣😂 Thubuti!
 
Back
Top Bottom