Bernard Membe, kama basi limekuacha chukua pikipiki ufike

Bernard Membe, kama basi limekuacha chukua pikipiki ufike

Sawa na hii ndiyo ile tunayosema haki inabaki kwa wenye maamuzi, kuna kitu unaweza kuwaza juu ya mfumo wa siasa na hatima ya maisha ya raia wa kawaida.

Sheria inakulinda ukiwa unaisimamia ndipo hapa tunaona hata hawa kina Mbowe nk wanasema katiba, katiba, katiba, hapana wakiingia kwenye lile jumba hawawezi kubadirisha.

Maana itakuwa inawalinda na hawawezi kutufanya raia tuunde katiba kama ile ya jaji Warioba ambayo wanajua inambana mmojawapo na kumtupa nje ya ulingo.
Kwenye Jamii kuna Makundi mawili la watawala na watawaliwa, watawala hawawezi ruhusu katiba inayowabana
 
Mikwara ehe! Ngoja utashangaa mpaka uzimie. Unajua watu wa CCM walio naye bega kwa bega? Ni watu wazito na hata kama watahamia chama chovu kama TLP Magufuli + dola hawataweza kuzuia huo mshindo.
Ukishakuwa nje ya mfumo na wanufaika awapo upande wako huna chako ukakune nazi tu
 
Waliokuwa kwenye system then wakashindwa kuibadilisha systems ili iwafae hata siku systems ikiwatupa wapambane na Hali yao
Watu wanapojisahau kuwa mfumo wa hovyo waouendekeza na wanaojidanganya kuwa wao hautawadhuru kana kwamba mhanga si Mtz mwenzao, sasa yanawakuta, nae anadai tume ya uchaguzi!
 
Siwezi kusema kauli ya Father of The Nation Mwl. JKN kuwa mpinzani wa kweli atatoka ndani ya CCM, maana hata wakati wa Edo kauli hii ilitamkwa sana na kuaminisha umma kuwa sasa siasa ya Tanzania imepata uhalisia.

CCM ni chama chenye mizizi iliyosambaa sana kiasi ukichimba juu juu huwezi kuiona na unaweza kusema huu mti utakufa mbona unaishi pasipo mbolea hahahaaaa.

Hapana/Ndiyo kwa mtizamo unaoweza kuwa nao, hapa tunakutana na safari nyingine ya kisiasa ambayo kila uchaguzi mkuu unapokaribia visa vya aina hii huwa haviishi kabisa toka jemedari JKM alipokuwepo ukikumbuka wakati wa kambona mpaka yule jamaa aliyetaka kuanzisha jeshi la msituni ili kumng'oa Julius.

Leo tunaye (kitengo mbobezi au lijendari) Bernard Camilius Membe, jamaa anaonyesha nia adhimu ambayo naweza kusema inaleta chachu kuufikia uchaguzi wa mwaka huu kupitia (chama babu) CCM ambapo kwa uharisia hawezi kupenya kwa vyovyote na njia yoyote.

Hapa anakwambia "Unaweza kwenda Dar es Salaam kwa basi, kama basi limekuacha chukua pikipiki utafika"

Lakini anakwambia, "ningekupa majina yote sita ya vigogo wanaoniunga mkono"

Hebu mfuatilie kwenye mahojiano hayo nimekuwekea hapo.
Kachero kachanganyikiwa kawa kama samaki nje ya maji hana ujanja,anangángánia CCM utadhani CCM ni baba /mama yake aende kwa akina Mbowe au Zitto ndio apambane na JPM,CCM wamemtupia virago baado tu anangángánia kama si kukosa busara ni nini sasa.
 
Kachero kachanganyikiwa kawa kama samaki nje ya maji hana ujanja,anangángánia CCM utadhani CCM ni baba /mama yake aende kwa akina Mbowe au Zitto ndio apambane na JPM,CCM wamemtupia virago baado tu anangángánia kama si kukosa busara ni nini sasa.
Na kama anajiona anakubalika na WaTz, basi angeanzisha chama chake akapata wafuasi lukuki watakaomuunga mkono.

Asing'ang'anie Ccm walikomfukuza!

Kung'ang'ania ng'ang'ania huku mwishowe ataonekana amechanganyikiwa na kwamba sindano ya kufurushwa imemwingia barabara!
 
Ajitahidi kuwa mwangalifu asijepata ajali maana pikipiki ni risk Sana na inahitaji uzoefu hasa Kama unafukuzana na mabasi ya kisasa yana Kasi Sana pia mashimo ya barabara za lami ni hatari.
 
Leo ndio anakumbuka kwamba inatakiwa iwepo tume huru ya uchaguzi. Walipokuwa ndani ya mfumo walichekelea leo wametolewa wanalilia.

Simpendi Jiwe ila sometimes ni afadhali anavyowanyoosha hadi nzi wa kijani wenzie. Ili hata wanaotamba sasa hivi wajue ipo siku mfumo utawabwaga, hivyo watumie muda huu kutengeneza katiba bora ikiwemo tume huru ya uchaguzi.

Acha akome.
 
Na kama anajiona anakubalika na WaTz, basi angeanzisha chama chake akapata wafuasi lukuki watakaomuunga mkono.

Asing'ang'anie Ccm walikomfukuza!

Kung'ang'ania ng'ang'ania huku mwishowe ataonekana amechanganyikiwa na kwamba sindano ya kufurushwa imemwingia barabara!
Mkuu kuachwa au kuachika kwa gafla kubaya na kunaumiza sana, pamoja na siasa kitakiwa kucheza kwa akili wengi wakiwa na nguvu humo humo ndani wanajisahau kuwa hiyo nguvu imeegemea nini..!.

Mfano hapo jamaa anasema ana watu wazito kama 6 na yeye wa saba, hata hao 6 najua kwa sasa kila mmoja anajitafakari endapo watachukua uhamuzi mgumu what next baada ya uhamuzi wao.

Kweli kama unataka mabadiriko using'ang'ani pale ulipo toka ili uonyeshe tofauti yako na aliye ndani lakini wengi hata wakitoka wanashindwa hii ni kutokana na mfumo uliopo unampa nguvu kubwa akiyeshika mpini, ukija kwa wananchi ndiyo kabisaaa, hofu na mashaka juu yako inakuwa kubwa ukiwa nje.
 
Membe anatumika na ccm kuwafanya vichwa panzi wasahau kuhusu upinzani. Mkija kushtuka Mbowe ameuza chama kwa Membe kama alivyokiuza kwa Lowasa.
 
Back
Top Bottom