Uchaguzi 2020 Bernard Membe ni kachero mtiifu kwa 'boss' wake Magufuli

Uchaguzi 2020 Bernard Membe ni kachero mtiifu kwa 'boss' wake Magufuli

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Kachero ni kachero tu!

Najua sitavunja sheria wala kanuni hapa.

Bernard Membe, Mgombea Urais wa JMT kwa tiketi ya ACT Wazalendo 2020. Historia yake ya kisiasa na utumishi inajulikana. Itoshe tu kusema ni Mtanzania ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za kisiasa na kitaifa.

Tangu sekeseke lake na CCM/Magufuli litokee na kumfukuzisha uanachama, swali moja la msingi sana nimekuwa nikijiuliza ambalo pengine kupitia humu tunaweza kusaidiana kupata majibu.

Labda niulize; kwanini Membe hamtaji kabisa Rais Magufuli kwa jina lake katika kauli zake anazozitoa? Mara zote amekuwa akimtaja kama fulani, bwana yule au kumrefer kivingine bila kumtaja directly. Ni kama anakwepa kumtaja jina hata akiwa anatoa speech kinzani. Je, ni kwa sababu ana kiapo cha utii cha ukachero? Kiapo kinachomzuia kumkosea heshima boss wake?

Ikumbukwe, kanali Lubinga aliwahi kumuonya na kumtahadharisha Membe >> Kanali Lubinga: Membe anaweza kushtakiwa kwa kumshambulia Amiri Jeshi Mkuu. Akumbuke kuna Court Martial, aheshimu kiapo

Kama ndivyo, uwepo wake nje ya system una maana gani kama bado anatakiwa kutii kiapo?
 
Unataka mwalimu akistaafu amtukane mwalimu mwenzake au mkuu wake kwa kuwa sasa haingii darasani kufundisha..

Lugha chafuu haikufanyi na haitaweza kukufanya uwe mpinzani bora zaidi ya kukufanya uwe mashuhuri kwa ujinga na upuuzi.
 
Unataka mwalimu akistaafu amtukane mwalimu mwenzake au mkuu wake kwa kuwa sasa haingii darasani kufundisha..

Lugha chafuu haikufanyi na haitaweza kukufanya uwe mpinzani bora zaidi ya kukufanya uwe mashuhuri kwa ujinga na upuuzi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Tukiachana na kutukana, vipi kuhusu kumtaja kwa jina? Umewahi kumsikia Membe akitaja jina Magufuli hata kwenye hoja za msingi zinazokinzana? Ushajiuliza ni kwanini?
 
Tukiachana na kutukana, vipi kuhusu kumtaja kwa jina? Umewahi kumsikia Membe akitaja jina Magufuli hata kwenye hoja za msingi zinazokinzana? Ushajiuliza ni kwanini?
Hata magu nae hamtajagi kwa jina membe
 
Sio Membe tu, Magufuli huwa hamtaji hata Lissu kwa jina.

Hizi ni kesi tofauti, kwa sababu Lissu yeye humtaja Magufuli kwa jina. Turudi kwa Membe.
labda ni hulka zao tu wanahisi watagawa point kwa team husika so bora kutotaja
 
Tukiachana na kutukana, vipi kuhusu kumtaja kwa jina? Umewahi kumsikia Membe akitaja jina Magufuli hata kwenye hoja za msingi zinazokinzana? Ushajiuliza ni kwanini?
1. Sijawahi.

2a). Anaweza na anaruhusiwa kumtaja kwa kumpa HESHIMA.
b). Hawezi kumtaja kwasababu ana dili na Mambo ya NCHI sio ya mtu, inafaa zaidi kutaja taasisi mbalimbali za serikali badala ya kumtaja mtu.

3. Kwasababu naamini ni mtu makini anaetambua misingi ya utu na haki za binadamu, ikiwemo haki ya kuheshimiana hivyo hawezi kumtaja taja bila sababu ya msingi.
 
Unataka mwalimu akistaafu amtukane mwalimu mwenzake au mkuu wake kwa kuwa sasa haingii darasani kufundisha..

Lugha chafuu haikufanyi na haitaweza kukufanya uwe mpinzani bora zaidi ya kukufanya uwe mashuhuri kwa ujinga na upuuzi.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Hajasema kutukuna bali "kurefer"

Punguza jazba.
 
Back
Top Bottom