Biashara ambazo hali ishakuwa mbaya kipindi hichi cha Corona

Biashara ambazo hali ishakuwa mbaya kipindi hichi cha Corona

Hapana lakini hilo neno limekaa kimtaani sana ndo mana nimeshindwa kuelewa.
Mlikuwa mnategemea ligi za mpira eti?
tatizo lako Amu wewe wakishua

vibanda umiza ni mabanda ya kuangalia TV
 
Hivi dadapoa wanatumia sanitizer kuwapaka wateja wao mwili mzima kujikinga na mnyama Covide?
Wateja wao mnaweza kutoa ufafanuzi maana kuna ubishi mkubwa sana hapa kijiweni kwetu.
Wanapaka Mshidede tu,

😀 😀 😀 😀
 
Hapana lakini hilo neno limekaa kimtaani sana ndo mana nimeshindwa kuelewa.
Mlikuwa mnategemea ligi za mpira eti?
sio ligi tu za mpira,kila kitu ambacho ungetamani ukione kwenye TV
 
Mkuu daladala wanafikisha hesabu kwa kujaza watu. Sasa hivi hakuna kujaza abiria ni mwendo wa 'level seat' wanafanyaje ili hesabu isitetereke?
Mkuu sasa hivi daladala zimeruhusiwa kuingia mjini,maana yake zipo daladala za kutoka k.koo to mbezi mwisho,Mbagala to mbezi beach yani route zote saivi daladala zinaenda (uwe na kibali tu ambacho ni 15,000) wanachofanya daladala sasa

wanachukua abiria stend konda anatangaza Mwisho ubungo,wanachukua level seat abiria mpk ubungo,wakifika ubungo abiria wote wanashuka kisha konda wanatangaza tena Gari inaenda k.koo,wanapanda abiria wengine wa k.koo,wakifika k.koo

kwenye kugeuza kuja mbezi Konda anatangaza Mbezi 2000 abiria wanagombania wakutosha,sasa piga hesabu ya 2000 kwa kichwa kwa level seat,nafasi za kusimamisha daladala wanapakia mizigo ambayo nayo inalipiwa nauli.

Tukumbuke mwendokasi hawaruhusu mizigo mikubwa,kwahyo abiria wenye mizigo wote sasa hivi wanakimbilia daladala na kwa nauli ya 2000 + 1000 ya mzigo wake anaona ni fair sana,maana kabla ya hapo ilim bidi abiria mwenye mzigo apande Noah ambayo nauli yake ni 3000 kwa yeye na mzigo wake 2000 jumla 5000

kwa sasa hivi daladala zimekuja analipa 3000 yeye na mizigo yake from k.koo to mbezi mwisho (huoni jinsi ambavyo daladala wanapiga pesa nyingi sasa hivi)
 
Mkuu daladala wanafikisha hesabu kwa kujaza watu. Sasa hivi hakuna kujaza abiria ni mwendo wa 'level seat' wanafanyaje ili hesabu isitetereke?
lakini hilo halitoshi dala dala sasa hivi zile sehemu ambazo watu walikua wanasimama nimeshakuta daladala zaidi ya mbili zimetengeneza mabenchi kuunganisha sitii mbili za kushoto na mbili za kulia kwa kuweka benchi kati kati,

ambapo lile benchi linakaliwa na watu wawili ambao hawana miili mikubwa,kwa hvyo ile nafasi ya kusimama kuna daladala imetengeneza benchi watu wanakaaa. hivyo watu wanaingia kwa idadi ile ile,hela ambayo wanapoteza makonda ni ile ya kusimamisha watu mlangoni ambayo hiyo hela wanaijazia na gepu la mizigo,watu wanalipia mizigo.

ki ufupi kwasasa daladala wanapiga hela nzuri kuliko hata ilivyokua mwanzo,matajiri wanalijua hilo ndio maana hamna tajiri alieshusha hesabu,Hesabu ya gari ipo pale pale costa zote hesabu imesimama pale,Eicher zote hesabu nayo ipo pale pale no excuse.

Madereva wanapata hela mkuu tena sana,kuna biashara zimeyumba ila sio ya usafiri.
 
lakini hilo halitoshi dala dala sasa hivi zile sehemu ambazo watu walikua wanasimama nimeshakuta daladala zaidi ya mbili zimetengeneza mabenchi kuunganisha sitii mbili za kushoto na mbili za kulia kwa kuweka benchi kati kati,

ambapo lile benchi linakaliwa na watu wawili ambao hawana miili mikubwa,kwa hvyo ile nafasi ya kusimama kuna daladala imetengeneza benchi watu wanakaaa. hivyo watu wanaingia kwa idadi ile ile,hela ambayo wanapoteza makonda ni ile ya kusimamisha watu mlangoni ambayo hiyo hela wanaijazia na gepu la mizigo,watu wanalipia mizigo.

ki ufupi kwasasa daladala wanapiga hela nzuri kuliko hata ilivyokua mwanzo,matajiri wanalijua hilo ndio maana hamna tajiri alieshusha hesabu,Hesabu ya gari ipo pale pale costa zote hesabu imesimama pale,Eicher zote hesabu nayo ipo pale pale no excuse.

Madereva wanapata hela mkuu tena sana,kuna biashara zimeyumba ila sio ya usafiri.
Oh nilifikiri una mbinu mbadala kumbe mbinu unayoisema ni kuvunja sheria. Faini yake ni 30,000/-. Kilwa road nilishakuta traffic anasimamisha daladala moja moja wanakagua. Unafikiri huu uvunjaji wa sheria dereva ataufanya kila siku kila trip?
 
Yes nawazungumzia hao,Japo hesabu haiwezi kuja sawa kama ya kipindi kile cha kusimamisha abiria ila ni mbinu wanayotumia kufidia pesa wanayoipoteza

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakugeuza nalo hata kabla ya kipindi hiki walikuwepo njia zile zenye shida ya usafiri. Kama ulivyosema mbinu haiwezi kuleta hesabu kama wakati ule wanajaza watakavyo.
 
Back
Top Bottom