Mkuu sasa hivi daladala zimeruhusiwa kuingia mjini,maana yake zipo daladala za kutoka k.koo to mbezi mwisho,Mbagala to mbezi beach yani route zote saivi daladala zinaenda (uwe na kibali tu ambacho ni 15,000) wanachofanya daladala sasa
wanachukua abiria stend konda anatangaza Mwisho ubungo,wanachukua level seat abiria mpk ubungo,wakifika ubungo abiria wote wanashuka kisha konda wanatangaza tena Gari inaenda k.koo,wanapanda abiria wengine wa k.koo,wakifika k.koo
kwenye kugeuza kuja mbezi Konda anatangaza Mbezi 2000 abiria wanagombania wakutosha,sasa piga hesabu ya 2000 kwa kichwa kwa level seat,nafasi za kusimamisha daladala wanapakia mizigo ambayo nayo inalipiwa nauli.
Tukumbuke mwendokasi hawaruhusu mizigo mikubwa,kwahyo abiria wenye mizigo wote sasa hivi wanakimbilia daladala na kwa nauli ya 2000 + 1000 ya mzigo wake anaona ni fair sana,maana kabla ya hapo ilim bidi abiria mwenye mzigo apande Noah ambayo nauli yake ni 3000 kwa yeye na mzigo wake 2000 jumla 5000
kwa sasa hivi daladala zimekuja analipa 3000 yeye na mizigo yake from k.koo to mbezi mwisho (huoni jinsi ambavyo daladala wanapiga pesa nyingi sasa hivi)