Biashara ambazo mwanafunzi wa chuo kikuu anaweza kufanya bila kuathiri masomo yake

Biashara ambazo mwanafunzi wa chuo kikuu anaweza kufanya bila kuathiri masomo yake

Kwanini usiwashauri wanafunzi wakatia mkazo kwenye masomo wakatoka na vitu kichwani badala ya vyeti tu?
 
Kwa hiyo kwa maoni yako chuoni ni mahala pa kufanya biashara???

That is a crappy.....kuna watu wajinga kweli .....inawezekana dhiki

Imetamalaki mpaka kugeuza chuo pahala pa biashara.
 
Kwa changamoto nilizo kutananazo chuo kufanya biashara ndogondogo hailipi kabisa yaani nikupoteza muda, kidogo betting inalipa na pia unakuwa free ila inaitaji moyo wa chuma..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani tupeane uzoefu kama kuna mtu ashawahi anzisha biashara Wakati yupo chuo na Ikakubali..!! Mimi nilianzisha biashara ya Saa za kikee ilaa daa sikuona faida yakee maana zilikuwa zinasumbua kutoka... Mpaka sasa sijaona biashara ya kufanya huku nasoma na niisimamie mwenyewe.. Tupeane uzoefu bhasi wakuu..
 
Chuoni ulipaswa kuanzisha biashara ya kuuza ped, kwa aina tofauti na size tofauti. Ungefaulu.
 
Najua kuna watu wengi walifanikiwa kupita chuo na kupata Mkopo. Kiukweli hela ya Boom pamoja na stationary, research, field huwa inakuwa hela nzuri kiasi kwamba kama una malengo unaweza itumia kwa manufaa!! Mfano kuanzisha biashara kwa kutumia hizo helaa japo utaishi maisha ya kawaida sana na kujinyima..

Je wewe ulishawahi kuanzishaa biashara ukiwa chuo??? Ilikuwa biashara gani. Je ulifanikiwaaa??? Ushuhuda wako ni wa muhimu sanaa... KARIBUNI
 
Nilianzisha biashara ya bangi malecture wengi walikua wateja wangu it was really interesting ingawa sijawahi vuta !!! Niliwauzia maboya [emoji41] [emoji124]
Nadhani huu ushuhuda unatosha ningesema mwingine wa kuuza nyama choma za [emoji232] ... Kuna watu wataniua ...[emoji17]
 
niliuzaga nguo za ndani za kike,niliwachapa sana block A na B lakini faida sikupata nikajilaumu tu bora ningelia bata tu maana wakinipa papuchi namtika bikini nusu dozen
 
niliuzaga nguo za ndani za kike,niliwachapa sana block A na B lakini faida sikupata nikajilaumu tu bora ningelia bata tu maana wakinipa papuchi namtika bikini nusu dozen
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]aisee kufanya biashara na wadada kazii
 
Huwez kufanya biashara upoo chuo kwa jins ninavoona ......kama huamin jaribu mkuu ......lazima upande mmoja uyumbe
 
Nilianzisha mradi wa kununua mbuzi(vibeberu) vidogo na kuvifuga kwa muda wa miezi minne na kuviuza tena kwa faida,ilinisaidia sana na tangu nihitimu udsm 2016 mpaka sasa ninaishi maisha yanayozidi kuajiriwa
 
duka lenye vitu visivyo muhimu kama cake, eat some more, juice na vinginevyo kama hivyo vilinilipa sana chuoni
niliita ....... mini supermarket
 
Nilikuwa nauza chupi sidiria hereini na cheni! Mabaibui ya mtumba kwa wadada wa kiislam....nilikuwa nauza balaa
 
Ngoja nikushauri kitu mdogo wangu coz sisi tumepia vyuoni kama wewe,unaweza ukadharau hii biashara but amini nakuambia unaweza ukawa kila siku unatoka na 20,000/

Tafuta Kibegi cha mgongoni nenda kwenye maduka ya jumla nunua pipi zile za kisista duu yani pipi kijiti au hata ivory,gum like Batook,n.k,vocha za kukwangua na kurusha,biskuti,karanga,tambi na hata ubuyu.then uwe unazunguka campus amini utauza sana coz maeneo mengi ya chuo biashara hizi hazipo ndani ya maeneo ya chuo(hawaruhusu machinga kuingia chuoni).sasa kwa vile watu ni wavivu kuvuka kutembea kufata pipi au biskuti au vocha we utatumia advantage hiyo kupiga salio.

Biashara za kipuuzi ndo zinalipa sana bora tu usiwe na aibu,uzuri wa biashara hii ni kwamba haiitaji usimamizi ofisi ni mgongoni mwako,haili muda wako wa masomo,unaweza kuifanya hata darasani wakati lecture inaendelea,haina usumbufu wa TRA,easy to carry,watu wakishakuzoea ndo nafasi yako nzuri ya kupiga hatua 1000 ahead!

kila la heri!!
Daah nikiangalia huu ushauri hadi mwenyewe napata wivu kwa nini nisingejuwa mimi ndo mwanafunzi sasa hivi...
 
Anzisha mtandao wa kijamii kwa ajili ya ku date wa kitanzania...
Uwe wa kiswahili... Ambao unaolenga Swahili speakers Tanzania, Kenya, na Diaspora

Duniani watu wanaoongea kiswahili ni almost 100 MIL
Tafuta watu wafuatao as co-founders wenye sifa zifuatazo

1)website developers
2)mobile delevoper
3)Software engineers
4) eneo hilo design iwe ofisi yenu

hakikisha hao watu ni experts

Hakikisha product yenu iwe ni kwa ajili ya android na ios

Na plz iwe bonge LA platform katika kiwango cha dunia isiwe na mambo mengi... Kama kuna msaada zaidi wa ushauri tutafutane tu
 
Back
Top Bottom