Biashara gani hapa dar haitaji mtaji mkubwa lakini inaweza kukulipa sana

Mkuu fanya biashara au huduma kati hizi utatoka, achana na wanaokukatisha tamaa mosi biashara ya mkaa unaanza hata kwa kupima kwenye makopo, pili kuendesha bodaboda, tatu kama huna mtaji kabisa waweza kuomba utingo kwenye magari ukakusanya nguvu na mtaji ,nne uza vitu vidogo vidogo e.g pipi, sigara, vocha, maji n.k, tano uza matunda, sita mtaji ukikuwa nunua mashine ya juice ya miwa ,uza hiyo juice inalipa saana n.k,n.k.
 
Great thinkerz, naomba mawazo yenu, ni bíashara gn hapa dar ya kuuza bidhaa au ya kutoa huduma ambayo haitaji mtaji mkubwa lakini mtu akiifanya kwa maarifa na ustadi mkubwa inaweza mlipa pesa nyingi? Plz naomba mawazo yenu wadau!

Kazi ambayo ahiitaji mkubwa ila inahitaji maarifa na ustadi mkubwa ni UTAPELI
 
Fanya udalali wa vyumba, nyumba, mashamba na vitalu vya gesi.. Utatoka tu
 
JF ishakuwa Genge la Wahuni waliopigwa na Maisha... si Uwanja wa Ushauri tenaaa... Ptuuh
 
Biashara ya udalali! Hata Manji ndio anachofanya. Ananunua huku na kuuza kule tena bila hata mtaji. Anaweka bla bla, anashinda tenda,anaenda benki wanadhamini show. Kiwanda kinaleta mali, then analipwa pamoja na faida yake. Anarudisha hela ya watu ya benki, then anaendelea kutumbua faida yake. Manji hana viwanda, lakini ndiye mmoja wa supplier mkubwa wa bidhaa mbali mbali hapa nchini...
 
pole na majibu mengi. nakushauri tafuta mahali panapofaa na uza bidhaa kwa jumla. cement, bidhaa za ujenzi au bidhaa za maduka kwa jumla zinalipa na zina wateja wengi, mzunguko wake ni mzuri na zinakopesheka.
 
Tafuta eneo zuri, biashara ya chips inalipa na mtaji wake ni mdogo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…