Biashara hii ina faida kupita biashara zote

Biashara hii ina faida kupita biashara zote

steve_shemej

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2015
Posts
1,175
Reaction score
1,588
Natumai wazima wote.

Leo nimeona niwashilikishe aina hii ya biashara yenye faida kubwa pengine ulikuwa haujui.

Pichani hiyo ni crasher, wengine huita karasha. Ni mtambo unaotumika kuvunjia mawe yenye madini kwenye migodi ya wachimbaji wadogo.

Mtambo huu unatumia mashine ya Diesel gear box na karasha lenyewe.

Unapataje pesa
Ukishakuwa na mtambo huo unaenda kuuweka sehemu ambayo kuna wachimbaji wadogo wa dhahabu. Wao huwa hawana huu mtambo; kinachofanyika wanakuja kwako na mawe yao wewe unakuwa unawapasulia.

Kunakuwa na makubaliano mawili: watakulipa pesa au mtagawana percent ya dhahabu itakayo patikana baada ya kuvunja mawe.

Ukifanikiwa kuwa na mtambo huu amini ndani ya miezi mitatu unarudisha pesa yako uliyo wekeza unaanza kula faida na huu mtambo unaweza kufanya kazi mpaka miaka miwili itategemea umetumia plate milimita ngapi kuunda karasha lako Ingawa plate ya milimita 25 na kuendelea ni safi zaidi.

Gharama za kumiliki
Gharama zinategemea aina ya vyuma vilivyo tumika ili uwe na mtambo na uanze kufanya kazi angalau uwe na Tsh 10 mil pia inategemea unaenda kuuweka wapi mtambo wako ila amini within three months hela yako inarudi.

images.jpeg
IMG_20200221_182206_5.jpeg
IMG-20200214-WA0001.jpeg
IMG-20200214-WA0003.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Steve kwani we unapatikana wp? Na kwa sasa ni wapi hasa kuna demand ya hizi karasha? Vp kuhusu makato ya serikali?
 
Steve kwani we unapatikana wp? Na kwa sasa ni wapi hasa kuna demand ya hizi karasha? Vp kuhusu makato ya serikali?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nipo songea sehemu zote zenye machimbo ya dhahabu biashara hi inafanyika sijui we upo wapi unakuwa tuu na leseni ya biashara ila kwa msumbiji biashara inafanyika bira ya Kodi maan migodi mingi ipo polini haifatiliwi ila utulivu mdogo kwa msumbiji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom