Biashara hizi zaweza kuanzishwa bila kuwa na mtaji (pesa) mkubwa au bila mtaji kabisa

Biashara hizi zaweza kuanzishwa bila kuwa na mtaji (pesa) mkubwa au bila mtaji kabisa

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,015
Reaction score
2,680
Watu wengi hujikuta wakiwa wanahangaika wataanzaje biashara bila kuwa na kiasi kikubwa cha pesa. Wakati huohuo, wengine wana pesa lakini hawana ujuzi wa msingi wa kuweza kupata zaidi ya kiasi walicho nacho.

Baadhi ya nilizoorodhesha hapa chini, ni biashara ambazo zinahitaji msingi (pesa) kidogo au hata bila pesa zinaweza kuanza kukuingizia kipato. Naamini wengine mnaweza kuongezea:

  1. Kuosha magari (Car Wash)
  2. Blogging
  3. Urembaji wa keki (Cake decorating)
  4. Utengenezaji mishumaa
  5. Mama Ntilie (Catering)
  6. Kutembeza vyakula maofisini (Mobile food vendor)
  7. Kazi ya usafi maofisini (kama mkiwa mmejikusanya kama kikundi)
  8. Computer troubleshooting (kwa graduates wa IT, Computer technicians)
  9. Event coordinator
  10. Kutumbuiza kwenye matukio kama DJ (Event DJing)
  11. Exercise/Sports instructor (wengi wanahitaji huduma hii)
  12. Utengenezaji wa fenicha
  13. Utunzaji wa bustani (Gardening, Landscaping etc)
  14. Usafishaji wa nyumba mtaani (House cleaning)
  15. Interior decorating (naona wengine hadi wanajiita 'interior designers')
  16. Kusaidia watu kubeba mizigo wakitoka kwenye manunuzi (Personal shopping assistant)
  17. Uuzaji wa nafaka/mazao toka kwa wakulima mikoani (wanahitaji kiunganishi na wateja wa mijini)
  18. Usahihishaji wa lugha/maandishi kwenye ofisi mbalimbali pamoja na vyombo vya habari (Proofreading)
  19. Kuwa MC kwenye matukio mbalimbali (Unatakiwa kusoma vitabu vya Public speaking zaidi)
  20. Kutengeneza sabuni (Soap making)
  21. Kufundisha (Teaching); hapa namaanisha kila mtu ana kitu anafahamu ambacho anaweza kuwa mwalimu mzuri
  22. Website design (kama ulisomea mambo ya graphics n.k)
  23. Software developer (kama umesomea software engineering n.k)
  24. Wedding planner/Event Cordinator


Natambua kuna watu waliosomea fani mbalimbali, tusaidiane kuwaelimisha wengine juu ya kutumia elimu zao bila kutegemea kipato kikubwa lakini baadae wakanufaika na elimu zao bila kusubiri kuajiriwa na serikali ama makampuni makubwa.

Watu wengi huko mtaani nikiwaulizaga ni kwanini yeye ni maskini ananiambia kwamba kama agepata milioni 150 angeanzisha biashara ya maana. Lakini utamkuta amekaa sehemu hiyo hiyo moja kila siku mchana kutwa akilalamikia serikali kwa nini haimpi ajira. Ajui kwamba ajira sio serikalini tu. Serikali ina ajira zake. Serikali inaajiri asilimia ndogo sana ya positions zake na ajira zinazobaki zinapatikana kwenye sekta binafsi ambayo ni makampuni binafsi na kujiajiri.

Ieleweke kwamba hata matajiri wemhi duniani walianza na mitaji midogo sana, muulize Mengi na Bakhresa watakuambia. Inachotakiwa ni kujiamini na kujibana ili uukuze mtaji na pia tujifunze kuacha kufikiria watu wengine watatufikiriaje tukianza na mitaji modogo. Kuwa na mafanikio ni tofauti na kuwa tajiri, so unaweza ukaanza na mtaji mdogo kabisa na kuukuza ukawa tajiri kabisa. Siku hizi kila biashara inalipa na sio lazima uwe umepitia chuo kikuu kufanikiwa kimaisha. Waulize matajiri wa mabasi watakuambia.

Ukichagua idea moja kati ya hizo alizoorothesha huyo jamaa hapo juu ukaweka effort na kuacha kuangalia ishu za watu wengine na kufanya biashara yako na kujibana, then mtaji wako utakuwa na pia kuacha kufikiria kuwa tajiri fasta, kwasababu eventually utakuwa tajiri baada ya muda flani kama ukijituma sana. Kama wengine wamekuwa na mafanikio kwa nini nawe usiwe?

Kuna njia kadhaa za kutafuta mtaji wa kuanzia biashara:

1. Kupitia kukopa kwa ndugu, rafiki na jamaa
2. Kukopa benki (ambapo kwasasa ktk nchi yetu mfumo wake si mzuri sana, ila ukiishaianzisha wanaweza kukupa maana mabenki wanatoa mikopo kwa biashara zilizoanza tayari)
3. Kama tayari biashara yako imeshaanza, unaweza uza hisa watu watoe hela ili wawe na asilimia flani za umiliki
4. Anza na biashara zisizohitaji mitaji kabisa

Jinsi ya kuanzisha biashara yenye mafanikio:

Mimi nasomea biashara na tunafundishwa kwamba kuna aina mbalimbali za mifumo ya biasha, aidha uanzishe mwenyewe au na partner n.k. Sasa tunaambiwa kwamba ukianzisha na partner unakuwa na mafanikio zaidi kuliko ukianzisha mwenyewe, mfano makampuni yotemakubwa duniani wameanzisha ma partners: google, microsoft, oracle, apple, n.k. Faida ya upartner ni kuchangia ujuzi na resources. Mfano wewe una elimu flani mwenzako ana hela, au yeye ana ujuzi wewe una connections na watu flani flani. Pia partnerships tax zake si kubwa. Sema partners lazima muwe mnaaminiana sana hata kama mko wengi.

Ideas zisizohitaji pesa nyingi:

1. kinyozi
2. kuuza matofali (veta wana mashine za kufyatulia matofali za bei rahisi kabisa)
3. Kibanda cha chipsi, ice cream, vocha, n.k
4. Duka dogo la reja reja

Anza kidogo then unakua baada ya muda flani. Usiogope kuanza na mtaji mdogo, maana ndo matajiri walianza hivyo na baada ya biashara zao kukua kidogo, ndo wanatokea watu wanawekeza kwenye biashara yako.

Siri nyingine ni kwamba kama utaamua kuandikia biashara yako kuwa kampuni, ukienda brela kuna aina kadhaa za makampuni mfano sole propriatorship (uliyoianzisha wewe mwenyewe), partnerships n.k. Hakunaga investor anayewekeza kwenye sole proprietoship. Ndo maana hata benki hawatoi mikopo kwenye vibiashara vya mtu mmoja mmoja kwasababu sole proprietorships (kampuni iliyoanzishwa na mtu mmoja mmoja) hairusiwi kuuza shares. So anzisha na partner ili muda wowote kama mnata kuongeza capital yenu mtu yeyote anajiunga nanyi na kwekeza kiasi cha pesa.

Ntakupa mfano wa facebook.

Mark zakabegi alipokuwa anaanzisha facebook alikuwa na ujuzi wa programming tu, hana hela wala nini. Ikabidi aanzishe partnership na rafiki zake eduardo na mwingine. Eduardo aliwekeza 15,000 dollars ndo ikafanya hata wawe na ofisi badala ya bwenini walikoianzishia facebook. So kampuni yao ikawa partnership. Baada ya muda kampuni ikawa imekua ndo akatokea jamaa mmoja akawekeza 500,000 dollar akapewa asilimia kadhaa ya shares na ndo hapo facebook ilipopaa kimafanikio. So usiogope kuanza na partner.

Cheers
 
Kwenye Catering ni balaa inabidi uwe na msingi wa kutosha labda kuosha magari ndio unahitaji ndoo ya buku na maji ya sh 500 kuosha gari zima.......Thou kuna ideas nzuri sana umetoa za bizna.
 
Kwenye Catering ni balaa inabidi uwe na msingi wa kutosha labda kuosha magari ndio unahitaji ndoo ya buku na maji ya sh 500 kuosha gari zima.......Thou kuna ideas nzuri sana umetoa za bizna.

Pia ukitaka kufanya Car wash ya kisasa inabidi uwe na mtaji mkubwa, kuosha magari kwa ndoo ni kupoteza muda.
 
Labda huelewi MTAJI ni nini.

Huwezi kuwa seremala kama huna ujuzi wa fani hiyo, na huwezi kufanya proofreading kama hukusoma. Kweli zipo fani zisizohitaji mamilioni lkn bado zina changamoto zake.
 
kweli kabisa biashara ni utayari wa mtu na jinsi gani amejitoa kufanya kazi hiyo.
 
kweli kabisa biashara ni utayari wa mtu na jinsi gani amejitoa kufanya kazi hiyo.

Mkuu kweli inabidi mtu uwe tayari kufanya kazi hiyo, hebu angalia hii biashara mpya inayochipukia kwa kasi mijini; Niliona bango moja pale maili moja Kibaha limeandikwa hivi, " kuuliza njia ni Tsh 500/ na kupelekwa Tsh 1000/". Sijashangaa nikaona bango kama hilo tena pale Sinza. Nikawauliza vijana wa mjini, wakasema hiyo sasa hivi ni kazi rasmi, mpoooooh
 
Kufundisha (Teaching); hapa namaanisha kila mtu ana kitu anafahamu ambacho anaweza kuwa mwalimu mzuri
Natambua kuna watu waliosomea fani mbalimbali, tusaidiane kuwaelimisha wengine juu ya kutumia elimu zao bila kutegemea kipato kikubwa lakini baadae wakanufaika na elimu zao bila kusubiri kuajiriwa na serikali ama makampuni makubwa.

Kufundisha ni moja ya kipengele ambayo inaongoza kwa kutohitaji mtaji kabisa ama kidogo sana. Ila ni vizuri katika kitengo chochote unacho ona upo fiti ukakiboresha kwa kujisomea ama kufanya practices tegemeana na nature ya huo ujuzi wako.
 
Kazi ya usafi maofisini (kama mkiwa mmejikusanya kama kikundi)

huitaji mtaji wala watu wengi, if you got the deal unaweza ajiri watu for day payment
 
Kufundisha ni moja ya kipengele ambayo inaongoza kwa kutohitaji mtaji kabisa ama kidogo sana. Ila ni vizuri katika kitengo chochote unacho ona upo fiti ukakiboresha kwa kujisomea ama kufanya practices tegemeana na nature ya huo ujuzi wako.

Kuna wakati nilipata kazi ya kumfundisha mtoto wa jirani yangu mambo fulani, nilikuwa napata malipo zaidi ya ujira wa Mhindi wangu, mwisho kale kadarasa kakapanuka sana, almanusra niache kibarua kwa Mhindi.
 
Kuna wakati nilipata kazi ya kumfundisha mtoto wa jirani yangu mambo fulani, nilikuwa napata malipo zaidi ya ujira wa Mhindi wangu, mwisho kale kadarasa kakapanuka sana, almanusra niache kibarua kwa Mhindi.


Hapo ndipo udhaifu wetu upo kwa weengi.... 'UTHUBUTU!' Malila hebu fikiria, darasa lilipanuka hadi likazidi pato la ujira lakini bado uliogopa kuendeleza kwa kuboresha na ku invest katika hicho chanzo chako cha pesa nzuri kwa woga wa kushindwa. Tunataka 'saftey' ya kutokuwa na risks na gurantee ya pesa ya mshahara tukisahau kuwa wakati wowote hiyo kazi inaweza kuisha na tukasahau kuwa biashara yako yaweza fika mbali saana na hata kupelekea wewe kuajiri pia...

Kwa hiyo Malila uliacha kufudisha?
 
Hapo ndipo udhaifu wetu upo kwa weengi.... 'UTHUBUTU!' Malila hebu fikiria, darasa lilipanuka hadi likazidi pato la ujira lakini bado uliogopa kuendeleza kwa kuboresha na ku invest katika hicho chanzo chako cha pesa nzuri kwa woga wa kushindwa. Tunataka 'saftey' ya kutokuwa na risks na gurantee ya pesa ya mshahara tukisahau kuwa wakati wowote hiyo kazi inaweza kuisha na tukasahau kuwa biashara yako yaweza fika mbali saana na hata kupelekea wewe kuajiri pia...

Kwa hiyo Malila uliacha kufudisha?

Sijaacha kufundisha na sitaacha, ila nilibadili mbinu ya ufundishaji. Sigawi samaki ila nafundisha kuvua samaki. Narudia tena kwa msisitizo, kufundisha kunalipa mara kumi zaidi ya mshahara wa Mhindi wangu. Darasa langu ni kubwa sana na linakuwa kila siku, sihitaji matangazo.

Kama unaweza kufundisha, fanya hii kazi,itakulipa.
 
Sijaacha kufundisha na sitaacha, ila nilibadili mbinu ya ufundishaji. Sigawi samaki ila nafundisha kuvua samaki. Narudia tena kwa msisitizo, kufundisha kunalipa mara kumi zaidi ya mshahara wa Mhindi wangu. Darasa langu ni kubwa sana na linakuwa kila siku, sihitaji matangazo.

Kama unaweza kufundisha, fanya hii kazi,itakulipa.


Malila kama hutajali toa mwongozo unaokuwezesha ili wengi tuweze kunufaika... BTW naomba kujua unadhani kuna uwezekano kuwa hio kazi kwa mhindi ipo hati hati ya kuweza iacha sababu ya hii kazi yako ulioanza kama mzaha?
 
Malila kama hutajali toa mwongozo unaokuwezesha ili wengi tuweze kunufaika... BTW naomba kujua unadhani kuna uwezekano kuwa hio kazi kwa mhindi ipo hati hati ya kuweza iacha sababu ya hii kazi yako ulioanza kama mzaha?

ashaDii Wewe nawe unao ujuzi wako mzuri kama mwandishi,mtangazaji,au mpelelezi. Unaongoe maneno laini yanayoweza kumtoa nyoka pangoni.
 
ashaDii Wewe nawe unao ujuzi wako mzuri kama mwandishi,mtangazaji,au mpelelezi. Unaongoe maneno laini yanayoweza kumtoa nyoka pangoni.


ha ha ha! Umenifurahisha saana... Basi nitaboresha ujuzi namie nifundishe. Lol, I am humbled.
 
ha ha ha! Umenifurahisha saana... Basi nitaboresha ujuzi namie nifundishe. Lol, I am humbled.

umeonaee? Haya endeleeni kumwaga data watu tumechoka na huu mkosi wa umaskini.malila mie na mwaminia sana hata mie ni mwanafunzi wake japo sina uhakika kama darasa analonifundisha ndilo analowafundisha wengine.
 
umeonaee? Haya endeleeni kumwaga data watu tumechoka na huu mkosi wa umaskini.malila mie na mwaminia sana hata mie ni mwanafunzi wake japo sina uhakika kama darasa analonifundisha ndilo analowafundisha wengine.

Mbona sasa unamwaga unamwaga mchele
 
Back
Top Bottom