Biashara kubwa ya masikini ni kusambaza umbea usiomlipa ndiyo maana anazidi kuwa masikini

Biashara kubwa ya masikini ni kusambaza umbea usiomlipa ndiyo maana anazidi kuwa masikini

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
Umaskini ni mfumo kama ulivyo utajiri hivyo ukiwa kwenye mfumo wa kimaskini utapata madili ya kimaskini tu ili uanze kupata michongo ya kitajiri sharti utoke kwenye mfumo wa kimaskini uhamie kwenye wa KITAJIRI

UKIWA KWENYE MFUMO WA KIMASKINI MCHONGO PEKEE UTAOPATA NI WA KUSAMBAZA UMBEA

UTAJIRI MKUBWA WA MASKINI NI UMBEA ANAJUA HABARI ZA WATU KULIKO FURSA ZA KUMALIZA UMASKINI WAKE

Ukitaka ushibe umbea mfuate Maskini atakupa habari za kila mtu tena kwa undani.

Habari ya kimbea haiwezi pita bila maskini kuijua yaani ataifuatilia kwa nguvu zote mpaka ahakikishe yeye ndio kinara wa habari hiyo ili asambazie na wengine.

Dili kubwa analopata Maskini ni kusambaza umbea usiomlipa hapo atakuwa bize kisha atalala akiwa amechoka na siku inakuwa imeisha hivyo tayari.

Kama unajiona hivyo jua utaendelea kuwa Maskini kwa sababu muda mwingi unafikiria umbea ambao hauwezi kutoa kwenye dimbwi la umaskini zaidi ya kukufanya kuwa maskini zaidi.

#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Mitandaoni Fikia Ndoto Zako
 
Back
Top Bottom