Biashara Leo: Ingia kwenye Biashara yenye ushindani lakini usishindane

Biashara Leo: Ingia kwenye Biashara yenye ushindani lakini usishindane

Makirita Amani

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2012
Posts
1,915
Reaction score
3,422
Moja ya faida za kuingia kwenye biashara katika kipindi hiki ni kwmaba huna haja ya kuumiza sana kichwa ni biashara gani ufanye. Japo wengi bado wanaumia vichwa.

Zama hizi kila aina ya biashara inafanywa, tena kama unapanga kuingia kwenye biashara ndogo ndogo basi popote ulipo kuna biashara zaidi ya 100 ambazo unaweza kufanya.

Huhitaji akili nyingi kuweza kuzijua biashara hizo 100, unachohitaji ni wewe kuwa mchunguzi na mtafiti wa kawaida tu. Angalia kila biashara inayofanyika kwenye eneo unalotaka kufanyia biashara zako. Biahsara yoyote ambayo ina upinzani mkubwa yaani inafanywa na watu wengi hiyo ni biashara ambayo ina wateja wengi pia. Vinginevyo hao wote wangeshashindwa na kuachana na biashara hiyo.

Sasa hiyo ndio biashara ambayo wewe unaweza kuingia na kama inaendana na vipaji au mapenzi yako basi ndio umeshaupata mgodi wa dhahabu. Kazi yako ni kuchimba tu na kuipata dhahabu yenyewe.

Lakini naposema uingie kwenye biashara yenye ushindani simaanishi uingie tu kichwa kichwa. Usiingie na kuiga kile ambacho kila mtu anafanya, utakuwa unajitengenezea njia nzuri ya kushindwa.

Chunguza kwanza ni vitu gani wafanyabiashara wengine wanafanya na ni wapi wanakosea. Kisha angalia unawezaje kuboresha pale wanapokosea na kutoa thamani zaidi ya wanayotoa sasa. Kwa kufanya hivi utatengeneza biashara yenye faida kubwa sana.

Wewe usiingie kwa akili ya kushindana, ingia kwa akili ya kuwa bora kuliko wengine wote wanaofanya biashara hiyo. Hakikisha unatoa thamani kubwa sana kwenye biashara hiyo na kuwaridhisha wateja wako. Hii itawafanya wateja kuwaambia wengine na wengine na hatimaye biashara yako kukua zaidi.

Angalizo; unahitaji muda, unahitaji kuweka juhudi sana na unahitaji uvumilivu. Mambo sio rahisi ila yanawezekana. usikate tamaa.

N;B kwa wale ambao bado wanaumia vichwa kuhusu biashara gani ya kufanya, tuwasiliane kwa mawasiliano hayo hapo chini.

Nakutakia kila la kheri kwenye biashara yako.

Kipengele hiki cha BIASHARA LEO kinakupa mbinu muhimu za kutatua changamoto za kibiashara zinazokuzuia kufikia mafanikio makubwa. Pia unajifunza kuepuka makosa unayofanya kwenye biashara yako na yanakuzuia kufanikiwa.

Kwa ushauri zaidi wa kibiashara, ikiwepo jinsi ya kupata wazo bora la biashara, jinsi ya kuanza na kukuza biashara na jinsi ya kupambana na changamoto za biashara piga simu 0717396253.
 
Asante umenipa kitu cha kuongeza kwa mwaliko wa kesho kijijini.
 
Back
Top Bottom