Joasi
JF-Expert Member
- Apr 3, 2014
- 766
- 674
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imependekeza kusamehe kodi mafanyabiashara au mwekezaji kwa kipindi cha miezi sita pindi anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).
Serikali imesema msamaha huo, utaanza kutumika Julai Mosi 2019, ili kumuwezesha mfanyabiashara au mwekezaji kujiandaa na mahitaji yanayotakiwa katika shughuli anazofanya, vilevile kuondoa usumbufu, dhana ya woga wakati wa kuanza biashara ikiwamo mahitaji ya leseni ya biashara na vibali vingine.
Hayo yameelezwa Alhamisi hii na Dkt. Mpango wakati akiwasilisha makadirio na mapato ya Serikali kwa mwaka 2019/20.
“Hatua hii inatofautiana na hali ilivyo sasa ambapo mfanyabiashara anapopewa TIN anaanza kufanyiwa tathimi (tax assessment) ya mapato yake ya biashara na kutakiwa kulipa kodi,” alisema Dkt. Mpango.
Serikali imesema msamaha huo, utaanza kutumika Julai Mosi 2019, ili kumuwezesha mfanyabiashara au mwekezaji kujiandaa na mahitaji yanayotakiwa katika shughuli anazofanya, vilevile kuondoa usumbufu, dhana ya woga wakati wa kuanza biashara ikiwamo mahitaji ya leseni ya biashara na vibali vingine.
Hayo yameelezwa Alhamisi hii na Dkt. Mpango wakati akiwasilisha makadirio na mapato ya Serikali kwa mwaka 2019/20.
“Hatua hii inatofautiana na hali ilivyo sasa ambapo mfanyabiashara anapopewa TIN anaanza kufanyiwa tathimi (tax assessment) ya mapato yake ya biashara na kutakiwa kulipa kodi,” alisema Dkt. Mpango.