Biashara ni kama kung-fu, sio kila mtu anaweza kufanya

Biashara ni kama kung-fu, sio kila mtu anaweza kufanya

Kumi4

Senior Member
Joined
Nov 4, 2021
Posts
101
Reaction score
106
Sijui niseme vipi ila kiukweli Biashara sio kitu cha kila mtu, kuna vivumbi vya kila mtindo viko humo ndani, nisiwachoshe niwape misiba yangu miwili mitatu kwanza:-

Mwaka 2021 kibarua changu kiliingia mbolea na kashikashi zikastawi kama hazina akili nzuri sasa bana ukilinganisha na mshahara wenyewe ulivyo ni wa mbuzi nikajikuta mpaka narudi mtaa sijajiweka sawa ile kiviile, nilijipiga piga nikanunua mashine ya juice ya miwa na kutengeneza banda la chuma la kisasa la futi 6 kwa 7 nikalitega mahali.

Nina mwanangu mmoja yeye hakuwahi kubahatika kuajiriwa so akaniomba awe anazugazuga pale nikasema fresh nikajikuna kuna nitafuta laini za Nini pesa nikaweka na kamataji uchwara kama 300,000 tu hivi. Location ilikuwa ni sokoni mjini Mbagala pale. Basi yule mwamba akawa anauza vifurushi tu mwezi ukiisha faida inakuja 10,000 na sio mbali saana na hapo (Ikfahamike kuwa hapo mashine ya juice iko tu ndani maana ilikosa mtu wa kuiendesha).

Gharama za uendeshaji zikawa kubwa pamoja na kwamba tulikuwa hatulipi kodi ni ushuru tu poale sokoni 500 kwa siku. Mwamba akaja akakacha baada ya msingi kwenda kwa jamii. Nikasema fresh.

Sasa basi ndio nikaingia mtaani rasmi na kuamua kuifufua mashine ya juice 'niutesti' upepo. Nilipoanza tu raia ninaokaa nao home wakawa wananisihi kuwa nisikae kimama maana lile ni eneo la soko na kama mnavyojua biashara kwenye masoko zinahitaji UTU UZIMA, mi nikasema fresh najilipua hivyo hivyo, eeh! Shule hapa ndipo ilipoanzia, enewei ngoja niwahishe futari kwanza kwa mama Saidi nikipoa narudi tena kujazia.
 
Biashara yyt ukiingia Kwa njia ya kusema unaenda kujaribu lzm ufelii mkuu.

Biashara haijaribiwi balii unaifanya km kazi zingine zinazoitaji mudaa .

Vinginevyo ukiingia Kwa njia ya kujaribu mtajii unarudi Kwa jamii
 
Sijui niseme vipi ila kiukweli Biashara sio kitu cha kila mtu, kuna vivumbi vya kila mtindo viko humo ndani, nisiwachoshe niwape misiba yangu miwili mitatu kwanza:-

Mwaka 2021 kibarua changu kiliingia mbolea na kashikashi zikastawi kama hazina akili nzuri sasa bana ukilinganisha na mshahara wenyewe ulivyo ni wa mbuzi nikajikuta mpaka narudi mtaa sijajiweka sawa ile kiviile, nilijipiga piga nikanunua mashine ya juice ya miwa na kutengeneza banda la chuma la kisasa la futi 6 kwa 7 nikalitega mahali.

Nina mwanangu mmoja yeye hakuwahi kubahatika kuajiriwa so akaniomba awe anazugazuga pale nikasema fresh nikajikuna kuna nitafuta laini za Nini pesa nikaweka na kamataji uchwara kama 300,000 tu hivi. Location ilikuwa ni sokoni mjini Mbagala pale. Basi yule mwamba akawa anauza vifurushi tu mwezi ukiisha faida inakuja 10,000 na sio mbali saana na hapo (Ikfahamike kuwa hapo mashine ya juice iko tu ndani maana ilikosa mtu wa kuiendesha).

Gharama za uendeshaji zikawa kubwa pamoja na kwamba tulikuwa hatulipi kodi ni ushuru tu poale sokoni 500 kwa siku. Mwamba akaja akakacha baada ya msingi kwenda kwa jamii. Nikasema fresh.

Sasa basi ndio nikaingia mtaani rasmi na kuamua kuifufua mashine ya juice 'niutesti' upepo. Nilipoanza tu raia ninaokaa nao home wakawa wananisihi kuwa nisikae kimama maana lile ni eneo la soko na kama mnavyojua biashara kwenye masoko zinahitaji UTU UZIMA, mi nikasema fresh najilipua hivyo hivyo, eeh! Shule hapa ndipo ilipoanzia, enewei ngoja niwahishe futari kwanza kwa mama Saidi nikipoa narudi tena kujazia.
Lete mavitu sasa
 
Biashara yyt ukiingia Kwa njia ya kusema unaenda kujaribu lzm ufelii mkuu.

Biashara haijaribiwi balii unaifanya km kazi zingine zinazoitaji mudaa .

Vinginevyo ukiingia Kwa njia ya kujaribu mtajii unarudi Kwa jamii
Na hilo ndilo nililolisanukia mkuu
 
Sijui niseme vipi ila kiukweli Biashara sio kitu cha kila mtu, kuna vivumbi vya kila mtindo viko humo ndani, nisiwachoshe niwape misiba yangu miwili mitatu kwanza:-

Mwaka 2021 kibarua changu kiliingia mbolea na kashikashi zikastawi kama hazina akili nzuri sasa bana ukilinganisha na mshahara wenyewe ulivyo ni wa mbuzi nikajikuta mpaka narudi mtaa sijajiweka sawa ile kiviile, nilijipiga piga nikanunua mashine ya juice ya miwa na kutengeneza banda la chuma la kisasa la futi 6 kwa 7 nikalitega mahali.

Nina mwanangu mmoja yeye hakuwahi kubahatika kuajiriwa so akaniomba awe anazugazuga pale nikasema fresh nikajikuna kuna nitafuta laini za Nini pesa nikaweka na kamataji uchwara kama 300,000 tu hivi. Location ilikuwa ni sokoni mjini Mbagala pale. Basi yule mwamba akawa anauza vifurushi tu mwezi ukiisha faida inakuja 10,000 na sio mbali saana na hapo (Ikfahamike kuwa hapo mashine ya juice iko tu ndani maana ilikosa mtu wa kuiendesha).

Gharama za uendeshaji zikawa kubwa pamoja na kwamba tulikuwa hatulipi kodi ni ushuru tu poale sokoni 500 kwa siku. Mwamba akaja akakacha baada ya msingi kwenda kwa jamii. Nikasema fresh.

Sasa basi ndio nikaingia mtaani rasmi na kuamua kuifufua mashine ya juice 'niutesti' upepo. Nilipoanza tu raia ninaokaa nao home wakawa wananisihi kuwa nisikae kimama maana lile ni eneo la soko na kama mnavyojua biashara kwenye masoko zinahitaji UTU UZIMA, mi nikasema fresh najilipua hivyo hivyo, eeh! Shule hapa ndipo ilipoanzia, enewei ngoja niwahishe futari kwanza kwa mama Saidi nikipoa narudi tena kujazia.
Wadau nimerudi.

Unajua nimrahisi sana kwa mtu ambae yuko kwenye ajira kupigia mstari michanganuo ya biashara ya ki abunuasi, kuna ile huwa tunaita biashara ya baa kwamba mnachora ramani mkiwa mmefunua vizibo vya konyagi ila mbungi sasa linaanza mkiingia front, basi mwanenu ajira ilivyonipiga chini rasmi nikasema sasa huu ndio muda wa mimi kujenga nipate na kausafiri kangu mana biashara nitaisimamia mwenyewe.

Day one nikaingia zangu sokoni nikachukua mzigo mmoja wa miwa nikaanza kukamua, hiyo siku kamua sana mchuzi wa muwa nikatoa glass kama 3 hivi siku nzima nikasema fresh sio mbaya biashara inataka muda. Basi bwana siku zikawa zinasonga ila sasa mzigo hautoki, ilikuwa naweza nunua mzigo mmoja wa miwa nikakamua wiki mbili, kwa waliowahi kufanya hii biashara mtakuwa mnanielewa, nikasema fresh ngoja nifunge na kandoro nazo hola vimbwanga vya mara siioni elfu 2 mara elfu 5 vikaanza sasa hapo ndo nikawa nayakumbuka maneno ya wakubwa vilivyo sasa.

Kwani kutafuta shekhe shingapi? Nakumbuka siku nimejiuliza hivyo jioni yake tu nikamfata shekhe wangu mmoja nikamwambia kuna mambo hayako sawa ebu nifanyie kisomo kwanza shekhe akasema mchezo mdogo nitafutie kama 30,000 ambayo na yenyewe sikuwa nayo nikaona sasa hapa mambo yanatakuwa kuw siriaz zaidi ikabidi nimkope huduma, shekhe akapiga dua sana nakumbuka nilienda nae mpaka kibandani pale nako akapatia baraka.

Kwa muda kama wa miezi mitatu hivi kiukweli hapakuwa na mabadiliko ya kutia matumaini nikabadili upepo. Kipindi hiko nakumbuka nilikuwa na Kompyuta yangu moja kuu kuu hivi ila kwa kuwa na mimi nina ujuzi na mambo hayo nikajiambia ebu acha nifungue ka library hapa niwe naingiza nyimbo na muvi pengine inaweza kuwa nafuu basi kijana wenu nikaianza safari. Nakumbuka mtaja wa kwanza kuja alikuwa faza mmoja hivi akataka nimuwekee muvi za mambo yetu yale ila sasa ni mtu tunaheshimiana so alinianzia mbali sana kudadeki kama anataka kununua ngozi ya mtu, tukafanya biashara tukamaliza.

Kwenye hiyo library sasa likaja swala la umeme kuisha kila mara, nanunua umeme unawekwa kwenye mita ya soko kinachofanyika hakieleweki lisaa au masaa kadhaa umeme umeisha na mbaya ilikuwa ni lazima tushee mita basi hapo likaanza tatizo jipya. Ngoja niheme narudi.
 
Biashara ndogo ndogo masokoni uwe mzitooo. Kuna bro wangu pale mbande analoga kifala.. na anauza kichizii .... Washindani wake wanachekaga tu akiwa anauza
Shida watu wa hivyo hawakuelekezi kwa wataalamu stahiki, mi sikuzote nasema sina tatizo na uchawi kama tu hadhuriki mtu wala mali zake, kama ishu ni kulinda maslahi yangu nitakufanya uwe kenge nichagulie na mtaro wa kukustiri.
 
Shida watu wa hivyo hawakuelekezi kwa wataalamu stahiki, mi sikuzote nasema sina tatizo na uchawi kama tu hadhuriki mtu wala mali zake, kama ishu ni kulinda maslahi yangu nitakufanya uwe kenge nichagulie na mtaro wa kukustiri.
Kuna jamaa alimsaidia pale mbagala kizuiani. Ila mkuu kuhama ni dawa. Zanzibar rate ya jealousy na envy sio kubwa hasa kwa wageni. Watu wanatoboa sana huku...
 
Biashara ni fani kama fani nyingine zinazohitaji elimu ambayo haifundishwi mashuleni

Sababu zinazofanya wafnyabiashara wadogo wanashindwa biashara

1.Kukosa customer care
ukishauriwa na mteja hata kama jambo dogo jitahidi ufanye maboresho mteja mmoja anawakilisha wateja 10 ukiboresha huduma wateja wanakufuata

2.Kutaka kuuza kwa kila mtu kuwa na wateja wengi kwa haraka

Unaweza kuwa na wateja wachache lakini ukapata faida pia unaweza kuwa na wateja wengi na usifikie lengo la faida

Ukiingia kwenye biashara yoyote kama mtaji wako ni mdogo tafuta wateja wako wachache wakuzalishie faida fanya mark kwa wateja wanaorudia kuipata huduma mara kwa mara kama wateja wanapungua jaribu kuuliza kwa wateja wachache upate feedback nini sababu ukiboresha huduma yako wanarudi

Nilichojifunza kwenye mafanikio ya biashara/huduma kubwa au ndogo yanahitaji watu wanaowaza kufanya maboresho kila siku kulingana na mahitaji ya wateja
 
Biashara ni fani kama fani nyingine zinazohitaji elimu ambayo haifundishwi mashuleni

Sababu zinazofanya wafnyabiashara wadogo wanashindwa biashara

1.Kukosa customer care
ukishauriwa na mteja hata kama jambo dogo jitahidi ufanye maboresho mteja mmoja anawakilisha wateja 10 ukiboresha huduma wateja wanakufuata

2.Kutaka kuuza kwa kila mtu kuwa na wateja wengi kwa haraka

Unaweza kuwa na wateja wachache lakini ukapata faida pia unaweza kuwa na wateja wengi na usifikie lengo la faida

Ukiingia kwenye biashara yoyote kama mtaji wako ni mdogo tafuta wateja wako wachache wakuzalishie faida fanya mark kwa wateja wanaorudia kuipata huduma mara kwa mara kama wateja wanapungua jaribu kuuliza kwa wateja wachache upate feedback nini sababu ukiboresha huduma yako wanarudi

Nilichojifunza kwenye mafanikio ya biashara/huduma kubwa au ndogo yanahitaji watu wanaowaza kufanya maboresho kila siku kulingana na mahitaji ya wateja
Unalijua Giza la hapa bongo
 
Sijuagi kama kuna bznes ya mtu kuzugazuga tu. Leo ndio nimeona kwako.
 
Wadau nimerudi.

Unajua nimrahisi sana kwa mtu ambae yuko kwenye ajira kupigia mstari michanganuo ya biashara ya ki abunuasi, kuna ile huwa tunaita biashara ya baa kwamba mnachora ramani mkiwa mmefunua vizibo vya konyagi ila mbungi sasa linaanza mkiingia front, basi mwanenu ajira ilivyonipiga chini rasmi nikasema sasa huu ndio muda wa mimi kujenga nipate na kausafiri kangu mana biashara nitaisimamia mwenyewe.

Day one nikaingia zangu sokoni nikachukua mzigo mmoja wa miwa nikaanza kukamua, hiyo siku kamua sana mchuzi wa muwa nikatoa glass kama 3 hivi siku nzima nikasema fresh sio mbaya biashara inataka muda. Basi bwana siku zikawa zinasonga ila sasa mzigo hautoki, ilikuwa naweza nunua mzigo mmoja wa miwa nikakamua wiki mbili, kwa waliowahi kufanya hii biashara mtakuwa mnanielewa, nikasema fresh ngoja nifunge na kandoro nazo hola vimbwanga vya mara siioni elfu 2 mara elfu 5 vikaanza sasa hapo ndo nikawa nayakumbuka maneno ya wakubwa vilivyo sasa.

Kwani kutafuta shekhe shingapi? Nakumbuka siku nimejiuliza hivyo jioni yake tu nikamfata shekhe wangu mmoja nikamwambia kuna mambo hayako sawa ebu nifanyie kisomo kwanza shekhe akasema mchezo mdogo nitafutie kama 30,000 ambayo na yenyewe sikuwa nayo nikaona sasa hapa mambo yanatakuwa kuw siriaz zaidi ikabidi nimkope huduma, shekhe akapiga dua sana nakumbuka nilienda nae mpaka kibandani pale nako akapatia baraka.

Kwa muda kama wa miezi mitatu hivi kiukweli hapakuwa na mabadiliko ya kutia matumaini nikabadili upepo. Kipindi hiko nakumbuka nilikuwa na Kompyuta yangu moja kuu kuu hivi ila kwa kuwa na mimi nina ujuzi na mambo hayo nikajiambia ebu acha nifungue ka library hapa niwe naingiza nyimbo na muvi pengine inaweza kuwa nafuu basi kijana wenu nikaianza safari. Nakumbuka mtaja wa kwanza kuja alikuwa faza mmoja hivi akataka nimuwekee muvi za mambo yetu yale ila sasa ni mtu tunaheshimiana so alinianzia mbali sana kudadeki kama anataka kununua ngozi ya mtu, tukafanya biashara tukamaliza.

Kwenye hiyo library sasa likaja swala la umeme kuisha kila mara, nanunua umeme unawekwa kwenye mita ya soko kinachofanyika hakieleweki lisaa au masaa kadhaa umeme umeisha na mbaya ilikuwa ni lazima tushee mita basi hapo likaanza tatizo jipya. Ngoja niheme narudi.
Hapo mtu mzima tunaheshimiana nimecheka sana
Hapo wengi tumekuelewa sana wazee wa PIGA WINDOW
sisemi kwa ubaya kuna mzee mmoja alikiwa mweka hazina wa msikiti mtaani
Kanifata ananiambia nataka frash nzuri nikamuuliza gb ngapi
Akajibu Aaahaa yoyote tu nzuri
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] Ilichukua masaa mawili kumuelewa na frash kumbe alikuwa nayo sema atanianza vipi nimuelewe dah ! umenikumbusha mbali sana nimecheka sana
 
Back
Top Bottom