Biashara ya Barakoa na Sanitizer ni kilio tu sasa hivi

The Humble Dreamer

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2015
Posts
7,574
Reaction score
10,598
Wakuu Salaam;

Hii kazi ya barakoa na sanitizer imekua kilio tu saivi. Mwanzoni mambo yalikua safi, ukilala ukiamka hela hii hapa, ni tofauti na sasa hivi.

Serikali ingetoa updates za maambukizi ya Corona mara 2 au 3 hivi yenye peak nzuri tu mzigo najua ungeisha maana kipindi cha nyuma kila ikitangaza tu, mauzo na faida ni kemkem.

Sasa hivi ni kilio tu. Nilichukua barakoa 2 niwape rafiki zangu hawakupokea, wakadai wanakereka kuzivaa. Nilichoka.

Kuna hasara inataka kuninyemelea nikiona mchana kweupe. Sasa hii hasara inatakiwa kupita mbali.

Wito wangu umeshaeleweka.
 
Biashara asubuhi, mlipiga hela ile mapema ila kwa sababu ya tamaa hamridhiki.... mngetamani corona iendelee kushika kasi.
Mkuu kila mtu anapambania tonge lake.
Siyo tunatamani corona iendeleee bali serikali ipige kelele watu wachukue tahdhar ili mambo yakae sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…