Biashara ya Bodaboda

Biashara ya Bodaboda

Sawa bro hebu nisaidie Biashara ya mtaji ya 30M unatakiwa kupata Faida ya kiasi Gani? Na REJESHO La per day unatakiwa kupata kiasi Gani?

Maana hapo Mimi nilianza na mtaji Wa 9M ndio ukafikia hapo kutoka Pikipiki 4 za kuanzia mpka kufika 15.

Hebu nyie watu Wa UCHUMI au BIASHARA mnisaidie hapa Biashara ya 30 millions inatakiwa kuingiza kiasi/ Faida gani per day?
Akikujibu naomba unitagi please
 
Japo napendelea bajaji, ila boda zinalipa pia.
👉Vipi ushawai fanya, au unasikia kwa watu🤔
👉Kama ndio, ni changamoto zipi zilikukumba.
👉Kufeli kwako, unahisi na wengine itakuwa hivyo??
👉Vipi Kama waki/tukiboresha mbinu na mikakati ili kuendana na changamoto zilizopo🤔🤔
👉 Never say it's impossible coz the word it's self says I'm possible
hawa jamaa wanasikia tu kufanya hawajawahi hii biashara ukiiweza ni nzuri sana
 
Nikutie moyo mkuu, hii biashara nzuri sana na tunapambana nayo, mimi ninazo 5 Kinglion mpya kabisa. Nimeenda nazo kwa mkataba na kwa mwezi jumla zinarejesha 1.5M

Pikipiki moja ni 2.6M mpaka inakaa barabarani, mkataba miezi 14, pesa yangu inarudi miezi nane, na miezi sita ni faida.

Mimi sijui kama haina faida ninachojua pesa ya pikipiki yote ipo bank na ikifika mwisho wa mwezi nachota iliyopo naweka Fixed account

Sijawahi tumia hata mia ya hii pikipiki (mfanyakazi serikalini) zikimaliza mkataba nitaagiza ndinga yangu maana ndo malengo


Make sure pesa hawakupi mkononi, iweke bank na uwekeze kweli usitangulize njaa.

Mahesabu ya boda natunza kwenye google sheet. View attachment 2553138
kwenye pikipiki hapo ziandike plate number mfano MC 213 DKH itasaidia usizichanganye
 
kwenye pikipiki hapo ziandike plate number mfano MC 213 DKH itasaidia usizichanganye
Mkuu sio plate#, hizi pikipiki nimezinunua kwa kuzipishanisha miezi na mikataba itaanza kuisha kwa kufuata namba zao na piah majina yao yapo kwa chini
 
Kuna watu wanamaono Daah eti milioni 34 usiwekeze kwenye bodaboda. Kuna watu wananunua Scania mende 130 milioni na aningiza 300,000 kwa siku hapo service juu yake, kuna wenye Daladala 80,000 kwa siku service kwa bosi, mapato, Latra na mengneyo juu ya Boss.

Hakuna kitu kigumu mno kama kumantain biashara mfano hardware, nguo , spare part na nyenginezo zinahitaji ukaribu mno kuzifatilia sasa jamaa anapiga kazi zake anawezaje mudu hizo biashara.
 
Kuna watu wanamaono Daah eti milioni 34 usiwekeze kwenye bodaboda. Kuna watu wananunua Scania mende 130 milioni na aningiza 300,000 kwa siku hapo service juu yake, kuna wenye Daladala 80,000 kwa siku service kwa bosi, mapato, Latra na mengneyo juu ya Boss.

Hakuna kitu kigumu mno kama kumantain biashara mfano hardware, nguo , spare part na nyenginezo zinahitaji ukaribu mno kuzifatilia sasa jamaa anapiga kazi zake anawezaje mudu hizo biashara.
Bro Kuna watu wanafikiria wanachofanya wao ndio wengine wafanye hikohiko.

Mtu anajenga nyumba ya milioni 20 na Kodi anakusanya 200,000/= Kwa mwezi sawa na 7,000/= Kwa Siku lakini hata hawazi kabsa anaona anachofanya ni sahihi. Na hapo anawaza kurudisha hiyo pesa baada ya Miaka 8.
 
Nina mwaka mmoja sasa katika hii Biashara.

Mimi Huwa nawapa vijana Pikipiki mpya FEKON Kwa MKATABA Wa miezi 11 au 12. Mahesabu ni 100,000/= Kila baada ya siku 10 yaani Kwa Siku ni hesabu ya 10,000/=.

Vijana wengine sio waaminifu na kweli hamna mtu mkamilifu Kwa asilimia 100% changamoto zipo anaweza kupata dharula, ajali, kuumwa au matatizo binafsi tu. Ambayo Kwa hizo siku 10 anaweza kukuletea 60K au 70K au 80K etc ila Hamna shida Huwa naandika kama deni ambalo baadae Mkataba ukiishi naongea nae Tena mezanii.

Ni Biashara nzuri Kwa maana FEKON Moja inauzwa 2.3M Kwa Faida wewe Utapata sio chini ya 1M Kwa miezi 11 au 1.3M Kwa miezi 12. Ambayo ni sawa na faida ya 100,000/= Kwa Kila mwezi Kwa Pikipiki Moja.

Mwaka Huu nataka nijaribu Kwa kununua Pikipiki USED na nianze kuwapa vijana Pikipiki USED za 1.2M -1.5 Millions Kwa Mikataba ya miezi 7 mpka miezi 8. Ili nitengeneze Faida nyingi Kwa muda mchache na Kwa kutumia Hela ndogo badala ya kununua Pikipiki mpya ya 2.3M.

Changamoto zipo lakini usikate Tamaa, Kila Biashara inachangamoto zake.

Vijana wapo mtaani kwako ni swala la kupeana Mkataba mbele ya mashahidi wa pande zote mbili na Kwa kusainiwa na Mwenyekiti au Mjumbe Wa Kijiji/ mtaa husika.

Unapatikana wapi mkuu
 
Nina mwaka mmoja sasa katika hii Biashara.

Mimi Huwa nawapa vijana Pikipiki mpya FEKON Kwa MKATABA Wa miezi 11 au 12. Mahesabu ni 100,000/= Kila baada ya siku 10 yaani Kwa Siku ni hesabu ya 10,000/=.

Vijana wengine sio waaminifu na kweli hamna mtu mkamilifu Kwa asilimia 100% changamoto zipo anaweza kupata dharula, ajali, kuumwa au matatizo binafsi tu. Ambayo Kwa hizo siku 10 anaweza kukuletea 60K au 70K au 80K etc ila Hamna shida Huwa naandika kama deni ambalo baadae Mkataba ukiishi naongea nae Tena mezanii.

Ni Biashara nzuri Kwa maana FEKON Moja inauzwa 2.3M Kwa Faida wewe Utapata sio chini ya 1M Kwa miezi 11 au 1.3M Kwa miezi 12. Ambayo ni sawa na faida ya 100,000/= Kwa Kila mwezi Kwa Pikipiki Moja.

Mwaka Huu nataka nijaribu Kwa kununua Pikipiki USED na nianze kuwapa vijana Pikipiki USED za 1.2M -1.5 Millions Kwa Mikataba ya miezi 7 mpka miezi 8. Ili nitengeneze Faida nyingi Kwa muda mchache na Kwa kutumia Hela ndogo badala ya kununua Pikipiki mpya ya 2.3M.

Changamoto zipo lakini usikate Tamaa, Kila Biashara inachangamoto zake.

Vijana wapo mtaani kwako ni swala la kupeana Mkataba mbele ya mashahidi wa pande zote mbili na Kwa kusainiwa na Mwenyekiti au Mjumbe Wa Kijiji/ mtaa husika.
Nahtaj mkataba na mm
Namba yangu 0713491359
 
NATAFUTA PIKIPIKI YA MKATABA
AU BAJAJ
NIPO KIMARA
0713491359
 
Bro Kuna watu wanafikiria wanachofanya wao ndio wengine wafanye hikohiko.

Mtu anajenga nyumba ya milioni 20 na Kodi anakusanya 200,000/= Kwa mwezi sawa na 7,000/= Kwa Siku lakini hata hawazi kabsa anaona anachofanya ni sahihi. Na hapo anawaza kurudisha hiyo pesa baada ya Miaka 8.
Sasa nyumba si unakusanya mpaka unakufa
 
Kuna kitu hapa watu wanashindwa kuelewa Sina mtaji Wa 34.5 Millions, nimesema nilianza na mtaji Wa 9 Millions Kwa kuanza na Pikipiki 4 tu mpka kufika sasa zipo zaidi ya Pikipiki 15.

Concept hapa ni kwamba Kwa marejesho haya haya ya Pikipiki nilizonunua mwanzoni ndio nilitumia kununua Pikipiki nyingine zilizofuata huku nikiongeza 30% ya sehemu ya Mshahara wangu Kila mwezi.

Mtaji wangu ni 9 Millions + 30% ya Mshahara wangu Kila mwezi mpka kufika hatua hii Kwa muda wa miezi 13 mpka Leo hii.

Kukosoa sio jawabu nipeni ushauri Wa Biashara ambayo inatakiwa kuingiza Faida ya zaidi ya 50,000/= Kwa Siku Kwa mtaji Wa 9 - 10 Million's.

Kukosoa Kwa sababu ulisikia mtu mwingine akishindwa hiyo biashara sio jambo jema, Nina zaidi ya mwaka mmoja sasa na sijaona shida yyote katika hii Business.

Kushindwa kwako sio kwamba na mwingine asifanye hiyo Biashara, TUKOSOE Kwa kutoa USHUHUDA Wa Biashara unayofanya wewe na KIPATO/FAIDA unayopata Kwa Siku itapendeza.

🟢Mfano Mimi Kwa Siku sikosi REJESHO La 150,000/=. Katika hii Hela 50,000/= ni kama Faida yangu Kwa Siku na 100,000/= ni Hesabu ya hela inayorudi kutokana na uwekezaji wangu ndani ya siku Moja Kwa mwezi mmoja (30 days) nitarudisha 3M ya mtaji wangu.

🟡TUPEANE IDEA ZA BIASHARA ZA KUFANYA, TOA USHUHUDA KAZI/BIASHARA UNAYOFANYA NA FAIDA UNAYOPATA ILI TUPATE MOYO WA KUFANYA BIASHARA NYINGINE PIA, ILI NlWEKEZE KATIKA BUSINESS NYINGINE.
well said bro
 
NATAFUTA PIKIPIKI YA MKATABA
AU BAJAJ
NIPO KIMARA
0713491359
Tafuta watu Wa hukohuko Kimara watakuunganisha na watu wanaotoa bajaji au Pikipiki Kwa mkataba. Sio rahisi mtu hakufahamu halafu akakupa Mkataba, wengi wanatoa Mkataba baada ya kujiridhisha Kwa Mwenyekiti wa Kijiji/mtaa akutambue na lazima na yeye awepo eneo husika iwe rahisi kufatilia baadhi ya mambo.
 
Sasa kweli yaani pikipiki 15 ni sawa na milioni 34.5 unaona faida ya 49,500 kwa siku ni sawa kweli?!!Hapanaaa hiyo kwa hesabu za kibiashara ni hakuna kitu hapo!!
Mimi pia sijaona biashara hapo, yani uwekeze 34.5M (pikipiki 15) kisha upate faida ya 45K per day?

Anyways kila mtu na maisha yake na namna anavyoona inafaa.
 
Back
Top Bottom