Biashara ya chips: Faida na Changamoto zake

Mkuu, Huyo jamaa yako wa Mbeya, hiyo Elfu 50 ni FAIDA au ni makusanyo ya jumla?

Mkuu hiyo ni makusanyo ya jumla,ambapo faida yake ni kati ya 20,000/- hadi 25,000/-,kwa siku ambayo ni sawa na 600,000/- hadi 750,000/-,kwa mwezi.hiyo ni kwa mwaka 2009.
 
Kama biashara yako unataka iwe bora zaidi na kufanya biashara yako kwenda kwa kasi zaidi, unahitaji vifaa hivi.

Wakati wa mabadiliko hata katika biashara yako. potatoes peeling, ya kutoa maganda ya viazi kule kwetu visiwani tunasema mbatata. cutting chips 🍟 hii ya kukata viazi vyako kwa haraka zaidi bila ya kuumiza mikono na kupoteza muda wa wateja wako.
chicken plucking ya kunyonyoa manyoya ya kuku, kwa haraka sana, kwa wafugaji wa kuku wa kuuza hii ndio inawafaa. chicken plucking
Hivi vinapatikana China, natumai Tanzania vipo.
 

Attachments

  • 1444641869413.jpg
    10 KB · Views: 316
Mkuu naomba uniulizie bei ya hizo Mashine na lile jiko la gesi la kipikia chipsi na chapati
 
Mkuu naomba uniulizie bei ya hizo Mashine na lile Huko la gesi la kipikia chipsi na chapati

Mimi sipo China mkuu, ispokuwa nipo katika research zangu tu, ndio nimeona bisara kuwaletea hapa ili wasio elewa wafahahamu haya, bei zipo tofauti inategemea ukubwa wa machine hizo, hapa UK zipo hizo za kutoa manyoya ya kuku bei yake about 499 pounds.
Hio potatoes peeling China kuanzia dollars 640 ninavyo ona online. pengine zipo chini ya hapo.
Kuhusu jiko la kuchoma chips la gas ni mp email yako ghalib@live.ie nitakuulizia used hapa UK, mpya hapa very expensive vitu vya commercial
 
Kwa muenekano wa haraka bila wa kitakwimu katika jiji la Dar es Salaam Biashara ya chips inakuwa kila siku.

Hali hii inaonesha wakazi wengi wa jiji la DSM ni wavivu na si wapenzi wakupika Hususan ma bachelor.

Wakati huo huo inaonekana kuwa wapenzi hasa wa chakula hicho ni wasichana (wanawake).

Hali hii inapelekea kuongezeka kundi la wavivu DSM na kupunguza nguvu kazi katika utendaji kazi kulingana na chakula kinacholiwa kuonekana kulemaza kwa upande mwengine wa virutubisho.

NB:Tudumishe asili kwa kupenda vyakula vya asili, na tujizoeshe kutouendekeza uvivu katika maeneo yote yani majumbani na maofisini.

KAZI TU.
 
Nina mtaji wa laki 3 na nusu, wakati natafuta ajira nimeona nijiajiri niuze chips, vipi mtaji unatosha? Any idea ya how to make them in a way it suits me (kisomi)?

Ushauri wenu unahitajika.
Hellow

mie pia nna wazo la kujihusisha na uuzaji wa chips....tafadhali naomba msaada ako
 
Hellow

mie pia nna wazo la kujihusisha na uuzaji wa chips....tafadhali naomba msaada ako
mkuu rejea huu uzi kuanzia namba 1,kila kitu kimezungumziwa kwa kadir ya uzoefu wa wadau ktk hii biashara
 
Habarani waheshimiwa, nipo hapa kuomba ushauri na mtazamo wa kitu ninchotamani kufanya, mfukoni nina mtaji wa laki 7 na ninataka kufungua biashara ya kuuza chipsi, kwa eneo lolote la dar ambalo ninaweza kufanya kweli hiyo biashara, najua changamoto ni nyingi lakini bila kupambana nazo huwezi kufika mbali.. Na kama huo mtaji ni mdogo je kwa hiyo pesa naweza kuongezea shilingi ngapi ili niweze kutimiza azma yangu?
 
Mtaji wa laki saba unatosha sana mkuu, kuna jamaa yangu yeye huwa anaanza na laki mbili tu, anachofanya anatafuta vijana wanaoaminika wa kitaa ambao hawana kazi, anatafuta location nzuri na kuilipia ,anawanunulia jiko na vikoro koro kibao, na mtaji wa kuanzia anawakabidhi kwa maandishi kwa sharti la kila siku wanamletea Tshs 10,000 tu.

Jamaa anapiga sana hela, na bahati nzuri hawa vijana nao huwa wanafurahia kazi maana jamaa huwa hawabani wala nini,na wanakula hapo hapo, wengi chipsi hizo hizo ndio msosi wao wa mchana, jioni ndio wanahangaika kula magetoni kwao, yeye anachotaka ni Tshs 10,000 yake daily na kazi isife, ukipata hata millioni kwa siku yeye hana habari ilimradi umpe mwekundu wake.

Ukiwa na nia nzuri tafuta location hasa maeneo ya vyuo au sehemu zenye muingiliano wa kibiashara au gesti nzuri ambayo kuna wazinzi wengi, utapiga sana hela.

Kwa uswahilini maneno ya Sinza, Mabibo NIT sokoni, Manzese barabara ya kutokea tiptop kuelekea Mabibo jeshini, Kigamboni chuo cha mwalimu Nyerere, Mabibo Hostel, Tabata yote, Kawe Ukwamani, Temeke sokoni, Kinondoni mkwajuni, Kinondoni studio, Mikocheni maeneo ya Kisiwani pale karibu na shoppers yana biashara kubwa sana ya chipsi.

Nimeona pia watu wanaingia mpaka kwenye shule za msingi na sekondary wanatengeneza chipsi kavu kidogo za 200 wanazifunga, watoto wanakula sana, na kwa kuwa wanaofanya hivi wanaongezeka kila siku inaonekana mfumo huu wa mashuleni unalipa sana.
 
Thanx sana mkuu..nimejifunza kitu hapo.. Na nitakifanyia kazi..unajua napiga chuo mwaka wa pili huu so natafuta kitu cha kufanya ili kuepuka kuhangaika pindi nitakapohitimu maana ajira zenyewe tabu sana za kusubiria halafu ukiangalia kitu kinacho matter sana ni kipato na sio ajira so nitalifanyia kazi lakini pia unaweza kunipatia kitu kingine mbadala wa huo maana life popote cha msingi ni kupigana na changamoto za hapa na pale
 
Ubarikiwe mkuu,umeleeza vizuri sanaa,na jamaa ana bonge la Idea aisee.
Hawa watu wa Namna hii ndio wanfaa kuishi jiji la Dar,lazim akili iamke
 
Mungu atakusimami,maana Umejitambua katika hatua ya awali saana.
Kaza buti na fuata ndoto zako na pambana na changamoto na utafanikiwa tu
 
WAkuu humu jamvini, nina mtaji wa laki saba mfukoni na nina fikiria kufungua biashara ya chips katika moja ya maeneo ya dar es salaam ambayo naweza kuendesha hii biashara kwa ufanisi zaidi, kama kuna yeyote mwenye kujua maeneo ambayo naweza kupiga hii busness kwa ufasaa naomba nijulishe na kama mtaji wangu mdogo, je hapo inahitajika kiasi gani.? Nipo chuoni kwa sasa ninampango nikimaliza semester mwezi wa saba. Mwishoni nikachakarika.. Nategemea sana ushauri wenu kwa maana mambo mazuri hayaji kwa pupa asanteni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…