Biashara ya Dagaa: Mjadala wa Uendeshaji, Masoko, Faida, Hasara na Changamoto zake

😳😳😳😳 mkuu kumbe huku mjini ilikua nipigwe kinoma yani eti ndoo elf 70 mwisho 65 . Ngoja nijipange niende, vp gharama za usafiri kuanzia mzigo namimi mwenyewe?
Jaribu kufika Happ mwaloni pale wanapandia hizo meli ziendazo visiwani uulize Bei,kwasasa,,haiwezi kuwa kubwa maana na wewe mzigo wako haitakuwa Tani kadhaa,Bali box mbili tatu au mifuko michache.
Ila Kama unataka kuchukulia Happ kwa elfu 40,Kuna jamaa Happ mwaloni alikua nao hao dagaa juzi tu waweza kumcheck
 
Ahsante sana mkuu kwa ushauri muruaaa. Ngoja niende visiwani kama alivyonishauri mkuu hapo juu ninunue mzigo kiasi ili nije nao dar kama kupata experience hata nikipata hasara Kama ulivyosema itakua imenijenga sana nakujua makosa yangu. Nakubaliana nawewe kabisa hawa waandishi wa vitabu wapo kibiashara tuu hamna lolote nimeamini, ila nimeamua kutake risk nipo tayari kuanguka ata mara kumi sio mbaya but am sure one day nitasimama. Thanks again mkuu kwa ushauri mzuri.
 
Nipe namba yake mkuu, ila ningependa niende mwenyewe kisiwani niweze kujifunza zaidi. Kwasababu naanza na mtaji wangu sio mkubwa kiivyo isitoshe sina soko la uhakika inabidi nipate mzigo kwa bei rahisi ili hata nikija dar niuze kwa bei pungufu nirudishe hela yangu huku nikizidi kukomaa zaidi na zaidi kibiashara. Ngoja nije niende mwaroni nipate abc zote mkuu
 
Haya nakupa screen shot Kama una Twitter account unaweza kubonga nae,ila namba Ni hizo,angalia tu asiku discourage kwenda chimbo mwenyewe ili ununue kwake.
 
Yani kwanza dagaa kununua kwa hiyo bei ni kubwa sana kama unaanza biashara, kama upo mwanza nenda Igombe, mwaloni,bwiru jiwe kuu ukanunue dagaa kutoka kwa wavuvi moja kwa moja ndio uzikaange mwenyewe. kwenye kuuza jiulize unataka kuuza jumla au rejareja hii itakupa muongozo wa kufanya biashara yako. Pia usiache kutumia mitandao ya kijamii hasahasa facebook kule kuna wateja wa kila aina. All the best
 
Kitu kingine kwenye dagaa hasa hasa huku mwanza angalia sana ni dagaa gani wa kukaanga unanunua, kuna wanaokaangwa wakiwa wabichi kabisa hawa soko lake lipo juu, kuna wengine wanaanikwa kidogo juani then wanakaangwa, na wengine wanapigwa jua kabisa halafu wanakaangwa haya makundi mawili ya mwisho kama biashara ni ngeni kwako mzigo unaweza kukufia maana afta sometime dagaa huanza kuwa wachungu.
 
Duh nilikua siijui hii mkuu. Shukran sana asee
 
Shukran sana mkuu
 
Daaaah ume ongea mpaka nimeanza kuvutiwa na mm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wadau waki kujibu uni tag

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maeneo gani ulipo?
 
Unacho taka kufanya nazani kinafanywa na watu wengi sana, so kinacho takiwa aisee ni kuumiza akili sana ki chekecha wanaita.

Kwa sasa kwa sababu ya Ushindani anaye umiza akili sana ndo anaye toka,

Lazima uwe mbunifu, kama gharama ni kubwa unafanyaje? Hakuna njia bandala?

Jaribu kuumiza sana kichwa, make wenzako wanao uza utakuta wana njia zao ambazo hawawezi kamwe kukuambia so ni juu yako na wewe kuja na zako na kuziwekea password.

 
Kule ulikuwa unadanganya kwanini?
Hahaha,we umejichanganya,,naration ya watu wawili tofauti,,

Haya mrejesho vipi wakuu,huu mwaka wa nne sasa,tumetengeza bilionea wangapi hapa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…