Biashara ya Delivery

Usimpe mtu mzigo kabla hajakupa pesa mkononi. Sio eti mtu anakwambia niletee mzigo niko hapa jengo la NSSF ukifika unishtue nije nichukue mzigo. Unafika unampigia anatoka nje, anapokea mzigo halafu anakwambia ngoja niingize huu mzigo nilete na hela. Ndio humuoni. Unajaribu kuulizia unaambiwa hatumjui mtu unayemtafuta....ndio ushaibiwa hivyo
 
Hahah watu hawana huruma
 
1. Umefika eneo husika mteja kaingia mitini , inabid urud na mzgo hapo mafuta umechoma
2. Kutapeliwa , mteja anapokea mzgo kabla hajakupa pesa then anaingia ndani , hafu anapotea mazima
3.usalama , Mteja anakuelekeza umletee mzgo eneo ambalo usalama wako ni mdogo anaweza akawaandaa watu wakakupora
4.Umepeleka mzgo amekulipa fresh , baada ya Muda anakupigia simu mzgo labda haufanyi kazi , inabid urud Tena kwenda kuangalia na kuset vizur ,
5. Bidhaa kukataliwa na mteja , ile umepeleka mteja anakuambia bidhaa na picha hazifanani[emoji16] hiyo inakuwa imekula kwa mtu
 
Asante kwa kutujulisha hayo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…