Mkuu labda ungefafanua kwanza ktk biashara hiyo uta deal na nini,
Mfano 1. kuagiza mitambo mbalimbali(uwakala) +after sale services kama wafanyavyo CMC, D.T DOBIE,MANTRAC n.k
2. Kutoa huduma ya matengenezo na uuzaji wa vipuri kama wafanyavyo MPOMABIVA
3. Kuuza mitambo mbalimbali,vipuri,matengenezo, vipya na vilivyotumika.
Ushauri wangu kwa MINING & HARBOUR equipments ni bidhaa zisizo na mzunguko hapa kwetu,kwa kuwa ni wateja ni wachache na uagizaji wa vifaa ni wa kutoa order si wa moja kwa moja.
Kwa vifaa kama REACH STACKER, FRONT END LOADERS,SIDE LOADERS,FOLK LIFTS, hizi wateja wameshaanza kuwa wengi,uwakala au uuzaji wa mitambo na vipuri ni biashara nzuri kwa sasa na pia ni mawakala wachache tu wapo nchini,pia ni vizuri kama ungeangalia pia vifaa kama EXCUVATORS,WHEEL LOADERS, GRADERS,TOWER CRANES NK.
Kwa hivyo basi ni bora ungejikita katika uagizaji na utoaji wa huduma wa vifaa hivyo nilivyovitaja.