Biashara ya Korosho imenishangaza

Pilim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
228
Reaction score
152
Najua kunamfanya biashara mpya ambaye ndiye anayenunua korosho kwasasa!
Hofu yangu ni kama kweli mfanya biashara huyo anajiamini na biashara yake!
1. kama biashara anayoifanya anategemea kupata faida kwa nini anaogopa kununua mzigo wa korosho kutoka nje?
2. Je mfanya biashara huyo anauhakika na soko atakako kwenda kuuza mzigo huo?
Nilidhani kama mfanyabiashara huyo anamtaji wa kutosha na bidhaa zikapatikana kwa wingi kutoka kokote kule, hiyo ndiyo ingekuwa furaha yake!!!
Naomba kueleweshwa hapo!!!
 
Tangu lini jiwe na mwanae daudi wakafanikiwa kwenye maamuzi yao!
 
anaeshangaza ni tajiri na mwenye kaya,anajua kuwa iyo biashara inakata ila kaamua kununua kwa bei ya juu kuliko bei ya soko kwa ajili ya kutaka sifa kwa ya kodi za watanzania wote.bei ni 3300 ukijumlisha na running cost inaweza fika 3600 per kg.sasa uuuuataenda uza kwa bei gani ili apate faida?na soko gani?lakin alishasema ikishindikana tutaanga na kugawana kg 2 kwa kila mtz.
 
Birashaka walishafanya upembuzi yakinifu!
au huwa ni Kiswahili tu?
 
Birashaka walishafanya upembuzi yakinifu!
au huwa ni Kiswahili tu?
Hamna kitu ni muendelezo wa kukurupuka tu,siku alipotangaza kuwa jeshi litatumika kununua dk chache nyuma waziri mkuu alisema yapo makampuni yaliykubali kununua lakini Bwana mkubwa hakutaka ata kumpa nafasi.
 
kwa utaratibu unaotumika leo kumuokoa mkulima wa korosho bila kujali uhalali wake kisheria usiwe wa zimamoto,utengenewe utaratibu kama ilivyo kwa mataifa ya ulimwengu wa kwanza na wa pili kuwafidia wakulima bei zinapoteteleka.wasiwasi wangu je uwezo wa kifedha tunao?pia usiishie kwenye korosho bali mazao yote .
 
Kupanga ni kuchagua, embu ona wiki ijayo watu wanajaa mapesa ya kuuza korosho alafu wiki hiyo hiyo form foo wanamalize necta, watu wanajitwaalia wake kwa pesa ya korosho.

Mwakani tunaendelea kulia umasikini [emoji3]
 
Hamna kitu ni muendelezo wa kukurupuka tu,siku alipotangaza kuwa jeshi litatumika kununua dk chache nyuma waziri mkuu alisema yapo makampuni yaliykubali kununua lakini Bwana mkubwa hakutaka ata kumpa nafasi.
Alimpa nafasi na akaelezaea vizuri kabisa lkn Mh akayakataa hayo makampuni. Pengine ulikua husikiluzi au ulikuta kipengele hicho kimashapita.
 
Alimpa nafasi na akaelezaea vizuri kabisa lkn Mh akayakataa hayo makampuni. Pengine ulikua husikiluzi au ulikuta kipengele hicho kimashapita.
maana yangu walitakiwa kuelezana huko ndani na kukubaliana nn kifanyike ndio watoke na msimamo mmoja.
 
Nawapa pole wafanya kazi wa taasisi za serikali.
hizo korosho wafanya kazi wa taasisi za serikali watazinunua kwa lazima kilo mtu kilo 2 watake wasitake,
na kila kilo watauziwa siyo chini ya 4,000.
Yangu macho
 
Serikali haitafuti faida bali inaepusha hasara kwa wakulima hata kama korosho hiyo itauzwa 3300 kumbuka hiyo korosho kama itauzwa nje kuna export levy inaweza fidia gharama nyinginezo, na kama korosho itabanguliwa na kuuzwa katika soko la ndani serikali itapata VAT ambayo ni 18% juu ya bei ya bidhaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…