Mkemia kay
Senior Member
- Jan 25, 2020
- 131
- 135
Nikiwa ni kijana mdogo nasoma kijijini kwetu nilikuwa nikisikia habari kwamba mjini kuna wanawake wanajiuza, sikuweza kuelewa kulingana na mazingira niliyokuwa nikiishi, nilitamani siku moja niwaone nipate uhakika na kwa mara ya kwanza nimefika mjini ilikuwa jiji la mwanza nilimuomba mwenyeji wangu anipeleke wanapopatikana kiujumla nilipata jambo la kujifunza ambalo mpaka sasa napata kitu cha kukuandikia wewe mdau wa Jamii forum.
Biashara hii imeshamiri sana kwa siku za hivi karibuni, Je umewai kujiuliza kwa nini, serikali inapiga marufuku sana Je watu wanaofanua hawaogopi serikali, nikagundua pia serikali yenyewe kuna watu ambao ni wadau wa biashara hizi kwani wananunua hawa dada poa au pia wao wanajiuza.
Sababu kubwa za hii biashara ni ugumu wa maisha unaowakumba wanawake na mabinti wengi wa kitanzania ingwa kuna watu wanaifanya hii biashara kama burudani kwa sababu hakuna jipya yaliwai kufanyika tangu kipindi cha sodoma na gomora kwa wale wenzangu na mimi wasomi wa biblia.
Asilimia kubwa ya wanaofanya hii biashara ni wanawake wenye mtoto mmoja au zaidi na hawana mme, hii inatoa tafsiri kwamba ugumu wa maisha ndo chanzo nilifanya utafiti katika jiji la Dodoma ambapo nilikutana na wanawake wanaofanya hii biashara zaidi ya 20 na wote walikuwa na mtoto na walisema wanafanya hivi ili mtoto wake aishi maisha mazuri. Kitu nilichopenda kutoka kwao ni kwamba hawakai na watoto wao kama ni mzawa wa Dar es salaam utakuta bishara ya kujiuza anaifanyia dodoma pesa anayopata anatuma kwa familia yake.
Katika asilimia izo kuna wanachuo pamoja na wahitimu wa vyuo mbali mbali, kwa mkoa wa Dodoma kuna vyuo vingi ambavyo vinatoa idadi kubwa ya hawa watu wanaojiuza hii ni kwa sababu ya ugumu wa maisha uliopo vyuoni pesa anayopata mtoto wa kike haiendani na uhitaji wake.
NINI KIFANYIKE?
Je, serikali inaweza kupambana kuondoa hii biashara ili kutunza taswira ya nchi jibu ni hapana.
Ni kweli kwamba dini na siasa vinategemeana lakini si kitu kimoja, nafikiri kisiasa hii biashara sio mbaya lakini kidini ni mbaya kwa sababu ni kinyume na maadili.
Hivi kwa nini serikali isiache hii biashara ifanyike kwa uhuru na viongozi wa dini husika wafanye kwa nafasi yao, kwa sababu uhalisia ni kwamba mtaani hali ni mbaya, kikubwa ni yatengenezwe mazingira sahii na sera nzuri ili bishara hii ifanyike salama ikiwa ni pamoja na kuzuia maambukizi ya magonjwa ya ngono kwa kasi zaidi.
Madhara ya hii biashara ni mengi kiafya na kimaadili lakini sera nzuri inaweza kuwa suluisho pamoja na viongozi wa dini kusimama katika zamu yao, inaweza kuondolewa bila ata kutumia nguvu ya dora.
Karibuni kwa mjadala kwa maswali na maoni pia
Biashara hii imeshamiri sana kwa siku za hivi karibuni, Je umewai kujiuliza kwa nini, serikali inapiga marufuku sana Je watu wanaofanua hawaogopi serikali, nikagundua pia serikali yenyewe kuna watu ambao ni wadau wa biashara hizi kwani wananunua hawa dada poa au pia wao wanajiuza.
Sababu kubwa za hii biashara ni ugumu wa maisha unaowakumba wanawake na mabinti wengi wa kitanzania ingwa kuna watu wanaifanya hii biashara kama burudani kwa sababu hakuna jipya yaliwai kufanyika tangu kipindi cha sodoma na gomora kwa wale wenzangu na mimi wasomi wa biblia.
Asilimia kubwa ya wanaofanya hii biashara ni wanawake wenye mtoto mmoja au zaidi na hawana mme, hii inatoa tafsiri kwamba ugumu wa maisha ndo chanzo nilifanya utafiti katika jiji la Dodoma ambapo nilikutana na wanawake wanaofanya hii biashara zaidi ya 20 na wote walikuwa na mtoto na walisema wanafanya hivi ili mtoto wake aishi maisha mazuri. Kitu nilichopenda kutoka kwao ni kwamba hawakai na watoto wao kama ni mzawa wa Dar es salaam utakuta bishara ya kujiuza anaifanyia dodoma pesa anayopata anatuma kwa familia yake.
Katika asilimia izo kuna wanachuo pamoja na wahitimu wa vyuo mbali mbali, kwa mkoa wa Dodoma kuna vyuo vingi ambavyo vinatoa idadi kubwa ya hawa watu wanaojiuza hii ni kwa sababu ya ugumu wa maisha uliopo vyuoni pesa anayopata mtoto wa kike haiendani na uhitaji wake.
NINI KIFANYIKE?
Je, serikali inaweza kupambana kuondoa hii biashara ili kutunza taswira ya nchi jibu ni hapana.
Ni kweli kwamba dini na siasa vinategemeana lakini si kitu kimoja, nafikiri kisiasa hii biashara sio mbaya lakini kidini ni mbaya kwa sababu ni kinyume na maadili.
Hivi kwa nini serikali isiache hii biashara ifanyike kwa uhuru na viongozi wa dini husika wafanye kwa nafasi yao, kwa sababu uhalisia ni kwamba mtaani hali ni mbaya, kikubwa ni yatengenezwe mazingira sahii na sera nzuri ili bishara hii ifanyike salama ikiwa ni pamoja na kuzuia maambukizi ya magonjwa ya ngono kwa kasi zaidi.
Madhara ya hii biashara ni mengi kiafya na kimaadili lakini sera nzuri inaweza kuwa suluisho pamoja na viongozi wa dini kusimama katika zamu yao, inaweza kuondolewa bila ata kutumia nguvu ya dora.
Karibuni kwa mjadala kwa maswali na maoni pia