Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Mkuu me pia nahitaji kufanya hii biashara ila cjui pa kuanzia boss, nipo dar ila nilifikiria kukodi fremu then nakuwa nafata mpunga Morogoro na kuja kukoboa dar na kuuza.

Naomba ushauri wako mkuu.
 
Mkuu naweza kukutafuta, nahitaji kufanya hii biashara nipo dar
 
mkuu me pia nahitaji kufanya hii biashara ila cjui pa kuanzia boss, nipo dar ila nilifikiria kukodi fremu then nakuwa nafata mpunga Morogoro na kuja kukoboa dar na kuuza

Naomba ushauri wako mkuu
Ushaur wang ni vema ukafata mchele afu uje kuuza uku,wazo la flemu ni zuri sana lkn ukfata mpunga itakupa shida
 
Maelezo mujarabu

Gunia la kg 100
Mpunga wakati wa mavuno huwa linauzwa bei gani?
 
Maelezo mujarabu


Gunia la kg 100
Mpunga wakati wa mavuno huwa linauzwa bei gani?
Wakati wa mavuno huuzwa tsh 40000 hadi 60000 inategemeana na msimu kama kuna mafuriko ya mpunga ila pia hua bei inapanda mpaka kufikia 120000 kwa gunia
 
Wakati wa mavuno huuzwa tsh 40000 hadi 60000 inategemeana na msimu kama kuna mafuriko ya mpunga ila pia hua bei inapanda mpaka kufikia 120000 kwa gunia

Vipi kiongozi kuhusu utofauti wa ubora wa mchele kutoka kanda ya ziwa mikoa ya shinyanga,geita kulinganisha na mikoa ya Mbeya,Rukwa na katavi kwa kuzingatia soko la Dar
 
Hongera kwa kutaka kujuajiri kupitia biashara ya nafaka. Nikwambie tu kila biashara unayoiona watu wanafanya ujue inalipa ndio maana watu wanafanya. Kusema inalipa vipi hapo kila mtu anakuwa na siri yake na utofauti unakua katika kujiongeza tu. Kitu kikubwa fanya utafiti na nikwambie tu ukweli hakuna utafiti mwepesi.

Usifanye utafiti kwa kuuliza watu tu, hakika hauta pata taarifa zote na hawata funguka mambo yoote, kuna vitu vidogo vidogo sana watu huwa wanasahau kueleza na wewe katika hesabu zako unaviacha na mwisho wa siku unakumbana na vyo gafla, na kama hauko makini unaweza kukimbia.

Katika tafiti zako uliza mambo ya msingi mfano unapo kaa na wauzaji kwanza usioneshe interest kama unatarajia kufanya biashara hiyo kwani wengi hudhani kuwa unapo muuliza basi umesha mchiunguza na kugundua anafaidika na hivyo atahisi unataka kuleta ushindani na uue hayo ni maisha kwake na hato ruhusu umvuruge kwa kuleta bidhaa sawa na yeye, hofu zaidi huwa ni kugawa wateja.

Anza urafiki na huyo unayetaka kumpeleleza na unaweza amza kama mteja tu wa hata kilo moja na kabla ya kununua ndipo vistori vyako vianzie hapo. Katika maswali yako yanaweza mpa picha kama unataka kujua kitu na anapo gundua ni vema umuonesha kuwa hilo ni ambo ungependa kufanya baadae na pia hauna mpango wa kufanyia mkoa huo na mauanjanja mengine ujuavyo wewe.

Unatakiwa kuchukua kiasi kidogo kama robo tu ya mtaji wako na kuanza nao na safari ya kwanza usitarajie faida maana kutaibuka vimbwanga ambavyo hukuambiwa na hapo ndio utaanza kujifunza na kujua ufanyeje. Kasoro unazo kutana nazo kila wakati ndio kujifunza huko na mwisho wa siku utakuja kuwa mtaalamu na kushauri wengine. Usianze na mtai wote "usipime kina cha mto kwa miguu yote".

Vinginevyo mi naona kila biz inalipa ni wewe tu uchague unaanza na nini.
 
Wakuu nimesikia mahindi yapo mengi sana nchini na mpaka sasa debe ni elfu 8 lakini pia nimeambiwa kusini debe ni elfu 15 kuna ukweli juu ya hili.
 
Utaifanyia wap ndugu. maana mm nahitaji kufanya msimu huu na sijajua wap pazuri.
 
Ebana hata mm nataka niulize jinsi ya kuchagua mpunga bora ili nipate mchele mzuri. Sijui jinsi ya kufanya...naomba msaada!
 
Jaman mie naomba msaada jinsi ya kuchagua mpunga mzuri...unafanyaje. Nimeasikia wengine wanasema unafikicha mpunga kwenye kiganja...
 
Habari wana JamiiForums

Natokea maeneo ya mkoa wa Katavi-Mpanda. Aisee napenda kufanya biashara ya mazao lakini nakosa misingi jinsi ya kuanza. Naombeni mawazo kutoka kwa wahenga. Sijapenda kuanza kwa kuulizauliza huku maana naijua hulka ya watu wa maeneo ya huku wanapoona mtu anawazo la kufanya biashara kama yao. Asanteni, napokea mawazo yoyote. Nitayapembua mwenyewe.[emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…