Biashara ya kutengeneza na kuuza "Askrimu" (Ice Lollies)

mpushi

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2011
Posts
280
Reaction score
77

Salam Wakuu,

Ninapenda kujua ni mtaji kiasi gani unaweza kutosha kuanzisha biashara ya kutengeneza na kuuza icecream.

Mchanganuo huo uhusishe gharama za kununua mashine ya utengenezaji, mashine ya kuhifadhia pamoja na mali ghafi.

Asante kwa msaada.

WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUFAHAMU BIASHARA HII
Hellow wana JF,

Mimi napenda kuuliza mtaji unaofaa kwa biashara ya kuuza ice cream, naomba mwenye uwelewa anisaidie.

Siku njema wote

MICHANGO NA MAONI YA WADAU
 
Nataka nianzishe biashara ya kuuza icecream kama za bakhresa na juice fresh wadau nani keshawahi kuifanya hii biashara?

Nahitaji nini na nini/vifaa?

Mtaji ni kama shilingi ngapi?

lol:israel:
 
Kiwanda cha kuzalisha ice cream kama za bakhresa ni dola 400,000.

Lambalamba ni laki 4. Hizi za kunyonya kwenye vifuko vya plastic mtaji elfu 40. Wewe unataka kipi fafanua. Mfano Ice cream ngapi per day? ni aina ngapi za ice cream unataka kuzitengeneza? Malighafi zako ni zipi? Distribution network yako. Je, una mtaji kiasi gani? umeipangaje? Please fafanua tukupe majibu unayotaka.
 

Hapo nilipo bold, ndio hela/mtaji alioanzia? Embu changanua, vitu gani vinahitajika vyenye gharama hio. Mtu mwenye mtaji mdogo hawezi kuanza hio business baadae akapanua?
 
sarah6, hongera sana kwa nia yako.

Sijawahi fanya hii biashara ila nimeifikiria sana na bado ipo kwenye mikakati yangu. Nina imani ukiwa na tshs 5m - 10m unaweza kuanza. afrika kusini zipo mashine za ice cream (ukiwa na usd 2500 unawezapata mashine nzuri tu).

Kama mfanya biashara mdogo basi eneo la biashara ni muhimu sana. Ukipata karibu na kituo kikubwa cha mabasi, karibu na shule za sekondari au chuo itakusaidia sana.

Aidha ukifungua hiyo biashara mikoa yenye joto mwaka mzima ni bora kuliko mikoa ambayo kuna miezi kuna baridi kali mfano Mbeya, Arusha, Iringa n.k. (miezi ya baridi utapoteza biashara).

Nakutakia mafanikio mema. mimi nipo njiani.
 
Habari zenu wakuu,

Nilikua naomba msaada wa kununua/upatikanaji wa vitu vifuatavyo:-

1-Guta/Toyo (Honda ya maringi matatu)

BEI GANI: Mpya na Used?

MAHALA: Wapi naweza kuzipata (maduka) katika sehem hizi- Dar na Zenji?

2-Ice cream machine (ya kibiashara) {{km ya apo chini}}

BEI GANI: Mpya na Used?

MAHALA: Wapi naweza kuzipata (maduka) katika sehem hizi- Dar na Zenji?

NB: Kama kuna importers pia sio mbaya

 
Habari wana JF,

Mimi naitwa Dennis. Jana nimeanza biashara hii ya aisikrimu za vifuko za shilingi mia mtaani. Changamoto niliyoipata ni hii; kuna mteja alivyoanza kuila alilalamika kuwa ni ngumu na anapata shida kuitafuna na akanishauri nitafute ujuzi unaotumika na wengine kutengeneza kwani wapo wanaotengeneza laini kabisa na wakati huohuo zinakuwa zimeganda.

Sasa naomba mwenye ujuzi anisaidie hapa, zinatengenezwaje laini, vitu gani vinawekwa na kwa utaratibu gani. Aisikrimu ninazotengeneza ni za ubuyu.

Ahsanteni kwa elimu wakuu
 
Nasikia wanawekaga ngano, ila sina huo utaalam
Wajuzi mjuzeni..

Kaka nashukuru kwa idea nitaifuatilia zaidi ila ukiweza kuja na maelezo ya kina jinsi gani inachanganywa na ice cream ya ubuyu itakuwa msaada mkubwa sana. Nasikia wapemba wataalamu wa hivi vitu ila sina friend mpemba anayefanya hii bness.
 
Please wadau kwawale ambao wameshawahi au wanao fanya biashara ya ice cream za Azam nahitaji kujua taratibu zake namna ya kuwa wakala.

Je, ina faida na ni zipi changamoto zake?
 
Mie nafanya kwa huku kwenye Duka langu.
Nitakupa kwa ninavyojua mie.
Kwanza unaenda kwao wanakupa Bei ya Jumla.
Faida sio kubwa sana ila lazima duka lako liwe na vitu vya ziada na sio kutegemea Ice cream peke yake unless uwe na flow kubwa.

-Fridges:-
Kwanza hakikisha una Fridges zenye uweo mkubwa,chukua kopo la Azam na usome na kujua inatakiwa iwe kwenye Baridi ya degree ngapi.Jaribu kuwauliza wao kuna kipindi walikuwa wanayauza yale ya kwao.Kama upo Dar nasikia bado utaratibu huo upo.Yale yao ni makuubwa sana na ni Heavy duty na pia ni dhamana kwa kazi hii.Ila lazima ununue na bei yake sio ya kitoto.Milioni na kitu kama sikosei.

Angalizo,Ice cream zina contents ambazo zinafanya usichanganye na kitu chochote katika uhifadhi,kuwa makini sana na hili.Huwa hazipendi kabisa kuwekwa ndani na kitu kingine,la sivyo utaona kila kitu kina ganda ila zenyewe hazigandi,fundi atakula hela hapo mpaka basi.So,Fridge ukiweka Ice cream zile basi weka zenyewe tu au pamoja na chockstik.Na umeme ukikatika muda mfupi tu basi zinayeyuka kulingana na vitu vingine vilivyomo humo.
Kama utakosa kwao basi nakushauri nunu Fridge Jipya kwa ajili ya Ice cream.
-Umeme
Umeme ukikatika,hapa itabidi iwe tatizo sana,hasa kwenye baadhi ya bidhaa,sasa lazima uwe mjanja kwenye upangaji wake,ili usiwe unalifungua muda muda mrefu kutafuta size ya Ice cream anayoitaka mteja,maana hewa ya nje ni ya mvuke wa joto,sasa hufanya kuyeyuka haraka sana pindi umeme ukiwa hakuna.Lakini ukipanga vizuri itakusaidi kwamba kama umeme haupo basi unafungua tu na ku pick anachotaka mteja.Tatizo kubwa ni pale itakapofika masaa kuanzi 6 - 8 bila umeme ndio issue.Hasa kwenye chocksick.
-Bidhaa:
Mbali na Ice ceam jaribu pia kuuza chockstik kwa jina maarufu,huwa zinatoka vizuri kwenye biashara,mie kwangu ndio zinaoongoza kwenye mauzo,maana nipo karibu na shule International School

Nikikumbuka jingine nitakuja.Ila kwa ufupi ukipata sehem nzui ni biashara nzuri.
Mie nimeweka,Ice cream,chockstic,nauza Fruits,Juices,Coffee maana nina coffee maker,na pia Maji.Na Vitafunwa mbalimbali.
Na katika vitafunwaa mbalimbali imenifanya nipate mpaka order za maharusi mbali mbali na shughuli mbali mbali,yaani bila kutarajia nayo imekuwa biashara kubwa.Mfano upande wa orders nyingi ni Sambusa,Katless,chapati za maziwa,bagia,Cakes nk,na pia huwa baadhi ya siku navamia dayoutings za watu na kuwashauri niwafanyie picnic lunches,maana biashara nyingine lazima ujifanye hamnazo ili yako yaende.
Ni biashara nzui,zingatia sana usafi.
Mie mwakani natarajia kufungua kama hii huko Dar es Salaam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…