Emmathias
JF-Expert Member
- Jan 22, 2018
- 681
- 958
Asante sana kwa ushauri mzuri mkuu, barikiwa sana sana.Mie nafanya kwa huku kwenye Duka langu.
Nitakupa kwa ninavyojua mie.
Kwanza unaenda kwao wanakupa Bei ya Jumla.
Faida sio kubwa sana ila lazima duka lako liwe na vitu vya ziada na sio kutegemea Ice cream peke yake unless uwe na flow kubwa.
-Fridges:-
Kwanza hakikisha una Fridges zenye uweo mkubwa,chukua kopo la Azam na usome na kujua inatakiwa iwe kwenye Baridi ya degree ngapi.Jaribu kuwauliza wao kuna kipindi walikuwa wanayauza yale ya kwao.Kama upo Dar nasikia bado utaratibu huo upo.Yale yao ni makuubwa sana na ni Heavy duty na pia ni dhamana kwa kazi hii.Ila lazima ununue na bei yake sio ya kitoto.Milioni na kitu kama sikosei.
Angalizo,Ice cream zina contents ambazo zinafanya usichanganye na kitu chochote katika uhifadhi,kuwa makini sana na hili.Huwa hazipendi kabisa kuwekwa ndani na kitu kingine,la sivyo utaona kila kitu kina ganda ila zenyewe hazigandi,fundi atakula hela hapo mpaka basi.So,Fridge ukiweka Ice cream zile basi weka zenyewe tu au pamoja na chockstik.Na umeme ukikatika muda mfupi tu basi zinayeyuka kulingana na vitu vingine vilivyomo humo.
Kama utakosa kwao basi nakushauri nunu Fridge Jipya kwa ajili ya Ice cream.
-Umeme
Umeme ukikatika,hapa itabidi iwe tatizo sana,hasa kwenye baadhi ya bidhaa,sasa lazima uwe mjanja kwenye upangaji wake,ili usiwe unalifungua muda muda mrefu kutafuta size ya Ice cream anayoitaka mteja,maana hewa ya nje ni ya mvuke wa joto,sasa hufanya kuyeyuka haraka sana pindi umeme ukiwa hakuna.Lakini ukipanga vizuri itakusaidi kwamba kama umeme haupo basi unafungua tu na ku pick anachotaka mteja.Tatizo kubwa ni pale itakapofika masaa kuanzi 6 - 8 bila umeme ndio issue.Hasa kwenye chocksick.
-Bidhaa:
Mbali na Ice ceam jaribu pia kuuza chockstik kwa jina maarufu,huwa zinatoka vizuri kwenye biashara,mie kwangu ndio zinaoongoza kwenye mauzo,maana nipo karibu na shule International School
Nikikumbuka jingine nitakuja.Ila kwa ufupi ukipata sehem nzui ni biashara nzuri.
Mie nimeweka,Ice cream,chockstic,nauza Fruits,Juices,Coffee maana nina coffee maker,na pia Maji.Na Vitafunwa mbalimbali.
Na katika vitafunwaa mbalimbali imenifanya nipate mpaka order za maharusi mbali mbali na shughuli mbali mbali,yaani bila kutarajia nayo imekuwa biashara kubwa.Mfano upande wa orders nyingi ni Sambusa,Katless,chapati za maziwa,bagia,Cakes nk,na pia huwa baadhi ya siku navamia dayoutings za watu na kuwashauri niwafanyie picnic lunches,maana biashara nyingine lazima ujifanye hamnazo ili yako yaende.
Ni biashara nzui,zingatia sana usafi.
Mie mwakani natarajia kufungua kama hii huko Dar es Salaam.
Vipi faida yake ikoje mkuu? I mean Ice cream