Biashara ya mabasi ya mwendokasi (UDART) ikadhibiwe Sekta Binafsi kabla haijafia mikononi mwa Serikali na kuitia aibu kubwa

Biashara ya mabasi ya mwendokasi (UDART) ikadhibiwe Sekta Binafsi kabla haijafia mikononi mwa Serikali na kuitia aibu kubwa

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Waziri mkuu wa JMT leo ametembelea biashara ya UDART katika eneo la Gerezani amekuta mfumo wa kutoa tiketi na kuhakiki wa kielektroniki hautumiki badala yake tiketi zinaprintiwa, zinawekwa pembeni, abiria akigaiwa tiketi hakuna uthibitisho kama ni ya serikali kweli au za wajanja nje ya Serikali.

Amekuta gari iliyokuwa na ubovu wa gia boksi tu ikiwa imeng'olewa viti na vitu vingine ambavyo inaonekana vimeenda kutumika kama vipuri kwingine! Waendeshaji waliona ni bora zaidi kufanya hivyo kuliko kuagiza spea nyingine!

Waziri mkuu amechukuziwa sana na hali ya kujifia mradi kama alivyoikuta aliyoukuta gerezani. Tangu 2019 mpaka leo bado wako wanajenga mfumo wao wa kielektroniki, miaka 2.

Serikali ya JK ilifanya jambo zuri sana kuja na mradi wa UDART. Ilikuwa sahihi sana kujenga miondombinu yote ya mradi kwa kiwango cha juu. Serikali ilikosea sana kuendelea hadi kushiriki biashara yenyewe ya usafirishaji, kununua mabasi na kuwa mwendeshaji.

Mabasi ya mwendokasi ni kama daladala tu. Tofauti yake ni kuwa na upendeleo wa kuwa na barabara zake maalum. Zipo kampuni na watu binafsi wengi wanaoweza kuendesha biashara ya daladala kwa ufanisi na tija kubwa kuliko UDART ya sasa inavyoendeshwa.

Serikali ifanye utaratibu haraka wa kuipeleka hii biashara kwenye sekta binafsi na yenyewe ibaki na majuku yake ya msingi ya udhibiti na ukusanyaji mapato kama inavyofanya kwenye mabasi, magari ya mzigo na daladala.
 
ATCL Mjini Moroni imevunjwa na kuibwa fedha zaidi Milioni 400 za Kicomoro Jumapili ya tarehe 18/4/2020 Taarifa zinabaini Ofisi hizo hazina ulinzi wala kamera.

Dulu zinabaini milango minne ya ofisi hizo hadi kuifikia Safe imevunjwa inaamika wafanyakazi wa kampuni ya uwakala wa Shirika hili la Ndege la Tanzania wameucheza mchezo huo na hii ni mara ya pili.
 
Kwanini bado ina mkurugenzi na menejimenti inayoteuliwa na serikali. Biashara ni usimamizi, mkuregenzi na menijimenti yake ni watumishi wa umma wasiofahamu chochote jinsi ya kuendesha biashara sasa hiyo biashara utasemaje iko katika mikono ya sekta binafsi?
Kitu usichokijua ni kuwa huo mradi unaendeshwa na sekta binafsi.

Tatizo ni jinsi hiyo sekta binafsi ilivyopatikana.

Simon group ni Scam
 
Kwa nini wanakaa na pesa nyingi kiasi hicho ofisini badala ya kuzipeleka benki?
ATCL Mjini Moroni imevunjwa na kuibwa fedha zaidi Milioni 400 za Kicomoro Jumapili ya tarehe 18/4/2020 Taarifa zinabaini Ofisi hizo hazina ulinzi wala kamera. Dulu zinabaini milango minne ya ofisi hizo hadi kuifikia Safe imevunjwa inaamika wafanyakazi wa kampuni ya uwakala wa Shirika hili la Ndege la Tanzania wameucheza mchezo huo na hii ni mara ya pili.
 
Muda mwingine unaona bora ukae kimya kuliko na ww kuchangia ukaonekana Mzandiki bure.
 
Kitu usichokijua ni kuwa huo mradi unaendeshwa na sekta binafsi.

Tatizo ni jinsi hiyo sekta binafsi ilivyopatikana...
Kuna vibanda vya kukatia tiketi kule Kimara - Mbezi vimefunikwa na majani mwaka sasa. Havina Dirisha, AC system na havikaliki badala yake Maafisa wa tiketi wanatumia vibanda vya mbao na nyasi kuanzia asubuhi hadi 12 noon.

Baada ya hapo hakuna tena tiketi hadi kesho yake. Waliacha kutumia e-cards miaka minne iliyopita sasa ni tiketi za kuprinti na sijui zinaprintiwa wapi na nani. Acha PM ashangae tu, huenda akachukua hatua. MAAJABU YA MWENDO KASI!
 
ATCL Mjini Moroni imevunjwa na kuibwa fedha zaidi Milioni 400 za Kicomoro Jumapili ya tarehe 18/4/2020 Taarifa zinabaini Ofisi hizo hazina ulinzi wala kamera.

Dulu zinabaini milango minne ya ofisi hizo hadi kuifikia Safe imevunjwa inaamika wafanyakazi wa kampuni ya uwakala wa Shirika hili la Ndege la Tanzania wameucheza mchezo huo na hii ni mara ya pili.
Kiasi chote hicho cha fedha kinafanya nini hapo?
 
ATCL Mjini Moroni imevunjwa na kuibwa fedha zaidi Milioni 400 za Kicomoro Jumapili ya tarehe 18/4/2020 Taarifa zinabaini Ofisi hizo hazina ulinzi wala kamera.

Dulu zinabaini milango minne ya ofisi hizo hadi kuifikia Safe imevunjwa inaamika wafanyakazi wa kampuni ya uwakala wa Shirika hili la Ndege la Tanzania wameucheza mchezo huo na hii ni mara ya pili.
Hela zenu badala ya kutulipa mkaenda kununua midege na bado
 
Huo mradi utawasumbua sana na hautafanysa kile ulichojengwa kufanya.
 
Tuache siasa za changa lamacho, Serikali ya JPM ndiyo imeua utendaji wa UDART.

Barabara za UDART kweli ni mali ya serikali lakini mradi wa mabasi mwendo kasi ulikuwa toka mwanzo ni mradi binafsi(private investment) uliowekezwa na mnganzania, Nd Kisenha.

Serikali ilifanya kila njia kumnyima pumzi mwekezaji huyu wa UDART. Alipoagiza mabasi alinyimwa katakata kuyatoa bandarini mpaka hela yote ipatikane Kulipa Kodi. Huku ni kukosa ushirikiano kwa muwekezaji, ambapo wale wa kigeni hupewa Tax Holiday au Mkataba maalum kwa malipo ya kodi kubwa.

Hii ingewezesha huduma iendelee, biashara iendelee na kodi ilipwe. Hili ni kosa, maana serikali haikuwa na msaada wowote kwa muwekezaji.

Pili, tunasikia tetesi kuwa sasa UDART ni mali ya Serikali maana baada ya Nd Kusenha kufunguliwa madai ya Uhujumu uchumi, kwawaida ya modus operadi ya Awamu ya 5kwa wafanyabiashara, serikali imejimilikisha uendeshaji.

Serikali zote toka Awamu ya kwanza hadi nafikiri Mwinyi (miaka zaidi ya33) mfupa wa DMT (Da es salaam Motor Transport) na UDA(Usafiri Dar es Salaam), ziliwashinda. Sasa sijui Awamu ya 5 ndio wangeweza Kuendesha UDART?

Mbaya zaidi serikali inaua moyo wa wazalendo kuingia miradi mikubwa kiuwekezaji, kinyume cha wanachoongea majukwaani.

Ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa kwa UDART kweli sioni mantiki yake zaidi ya kusema Serikali imachukua na kuanza mradi huu on a false start.

Sana sana ni kujikosha kwa wananchi kwa failures za serikali yenyewe, kusaidia wazalendo kuwekeza nchini mwao.
 
Nilikuwa siamini kwamba kwenye kila analogusa Magufuli huwa ana haribu Ila kwenye Mwendokasi ndo sehemu niliyokuja kuamini kwa Mara ya kwanza!

Kwanza inabidi wote tujiulize mwendokasi ilianzia wapi?

Mradi wa mabasi ya mwendokasi ukianzishwa na kuasisiwa na Rais wa Awamu ya nne. Kwa Jinsi mradi ulivyokuwa umeandaliwa ulitakiwa kusimamiwa na kampuni binafsi na tangu mwanzo ulisimamiwa kwenye mfumo huo. Mradi huu ulikuwa chini ya Kampuni na Kisena na wakati unaanza kila kitu kilikuwa kinaendeshwa katika dunia ya kisasa. Ticket zilikatwa kielectronic na watu waliweka hadi kuwa na kadi ya kutumia mwezi mzima.

Alipokuja Magufuli kwanza alianza ku deal na kisena kwa sababu kisena hakuwa kwenye kundi la watu waliomuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Alimtesa kisena kumpa kesi za uhujumu uchumi na mkewe na baadae kumnyang’anya mradi na hatimaye akaondoa utaratibu wote mzuri uliokuwa umewekwa kwa ajiri ya kuendesha mradi.

Matokeo yake akawapa wanajeshi, na hapo ndo Tatizo lilipoanza. Mradi ulianza kuendeshwa kwa tabia za kiswahili na watu wakaanza kukata ticket kama daladala.

Mradi huu hadi kufikia sasa ulitakiwa uwe umeshaanza kujiendesha kwa faida Ila kwa roho mbaya ya magufuli na tabia zake za kuchukia matajiri ndo amefanya mradi ule uwe kituko na usifike popote.

Polee kisena. Buriani Mwendokasi.
 
Mradi Ule kwanza haukuzingatia Ukweli Wa Hali halisi ya usafiri na mm huwa najiuliza ni lini nchi hii itaamua kupanga mkakati wa miaka 100 mbeleni. Hii bomoa, lipa fidia, jenga.

Lipa fidia, Bomoa na Jenga tena itaisha lini?

Hivi tuna Idara za mipango ya hii miji kweli? inawezekanaje kila mradi lazima uwe na fidia fidia sasa tukilipa wala hatujali tena kujua hawa wametoka hapa wanaenda wapi tusianzishe gogoro lingine tena mbeleni.
 
Back
Top Bottom