Biashara ya madini ya dhahabu

Mkuu, hebu fafanua kidogo hiyo ya kuhudumia wachimbaji small scale. Mchakato wake ukoje?
 
Jifunze pia kuichezea ile scale, halafu ununue nitric acid ukiuziwa mbichi unaimwagia kwanza kama ni feki ina Sambaa, hakikisha unayafahamu majiko ya siri siri ya kuchoma dhahabu na uzifahamu pia identified illusion,
Illusion au elution NI NINI?
 
Jifunze pia kuichezea ile scale, halafu ununue nitric acid ukiuziwa mbichi unaimwagia kwanza kama ni feki ina Sambaa, hakikisha unayafahamu majiko ya siri siri ya kuchoma dhahabu na uzifahamu pia identified illusion,
Mbichi ni dhahabu ambayo haijapita jikoni au ambayo haijapita mwaloni?
 
Na Karasha huwa gharama zake zikoje wakuu? Je karasha moja kubwa linaweza ku accumulate rudio la kama tani ngapi kwa mwezi ikiwa vijana 8 wanafanya usiku na mchana? Na je, price ya kila tani inaweza ikawa roughly sh ngapi ukiuza kama rudio tu bila kupeleka plant.
 
.
 

Used complete mil 3 na kuendelea kulingana na hali yake, gololi mil 1. Mpya mil 8-10 inategemea na thickness ya crusher na load capacity
Mawe ya kawaida unasaga mfuko kwa dk 30 kelembe mpaka saa 1. Bei kipimo ni tipper likijaa au mnapatana kwa lundo zima... Bei inategemea njaa zako, muda, competition, chemical properties/composition ya rudio, location et la
 
Inawezekana kabisa kununua rudio ikawa inalipa zaidi then, baada ya kujiridhisha na vipimo vya purity ya rudio though.
 
Wadau, habari za wakati huu... Kuna mtu yeyote yuko tayari tuungane tuanze harakati ya ukusanyaji na uchenjuaji wa mchanga wa madini (Marudio). Sina uzoefu wowote ila nina taarifa za awali na nia ya kazi. For 9 months only. Kitakachopatikana tugawane.

Kuanzia kukusanya kwa kununua mawe, kusaga mwaloni kukuza kifusi mpaka kupeleka plant.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mimi niko tayari. Nina karasha ,mwalo nk rasilimali pesa ndio imekata napatikana geita.
 
Nimeoenda ufafanuzi wako.
Unaweza kutoa mchanganuo wa bei wa vifaa ulivyotaja?
 
Hello natumai wote ni wazima kabisa na wa afya iliyo bora kabisa,

Jamani mimi nataka nijue haswa biashara ya madini ya dhahabu ni shilingi ngapi kwa gram1?

Na je ukiwa na 3million unaweza kuianza.

Gram moja nitainunua kwa Tsh 50k. hadi Tsh 120k kwa gram kutegemea na ubora: 24k, 22k, 18k, 14k au 10k.
Kwa pesa yako hiyo, 3m unaweza kununua 50g hadi 100g.
 

Upo tayari kupoteza pesa kiasi gani??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…