Biashara ya majengo ya kupangisha

The boss himself

New Member
Joined
Jun 28, 2019
Posts
2
Reaction score
3
Poleni na kazi wadau,

Mungu atusaidie kupata zaidi katika miangaiko yetu ya kila siku. Mungu ni mwema nyakati zote, nikiwa kama kijana Nipo mwaka wa pili udsm katika familia wanandugu tumeuza jengo flani la mzee na kufanikiwa kugawana kila mmoja million 386.

Plan yangu kubwa ni kuwekeza katika majengo ya kupangisha, kwa heshima kubwa ya wadau mbalimbali mlio humu nilikua naomba mawazo yenu ni jinsi gani naweza fanikisha lengo langu na niwekeze hasa katika majengo ya aina gani na yatayonilipa pesa nzuli (niwekeze Dar, Kilimanjaro, Arusha au Dodoma)


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Safi sana


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ni vizuri ila kuhifadhi pesa yako kwenye majengo maana naonaga iko salama.
Ila utambue faida huchelewa sana.

Labda wataalamu waje watujuze zaidi.
 
Uwekezaji wa Majengo ya Kupangisha ni mzuri, lkn kwa maeneo kama Daaslam kwa sasa majengo mengi yako tupu kutokana na Uhamisho wa Serikali kwenda Dodoma.
Nashauri pia angazia Jicho lako kwenye hii Mikoa mipya ya Simiyu, Njombe na Katavi huko Taasisi nyingi zinazoenda kufungua matawi ya Ofisi zao zimekosa Majengo ya kuanzia kabisa. Hivyo ktk uwekezaji wako maeneo hayo yape nafasi.
Hongera kwa mawazo mazuri mkuu
 
Kuna majengo makubwa makubwa hapa town sijui hata kama yamepata 1/4 ya wapangaji.
 
Biashara hiyo ni nzuri. Uzuri wake ni kwamba inakuhakikishia kupata kipato kila mwezi na kinakuwa constant na cha uhakika na pia huhangaika kukimbizana na miruko ya wafanyabiashara. Kuna members wamesema kuwa nyumba ziko nyingi kwa sasa ila mimi nina wazo tofauti. Opportunity kwenye biashara ya nyumba za kupanga bado ipo lakini wewe inabidi ufanye tofauti na wengine. Usipende kuiga nyumba zilizopo kwenye market kwani itasababisha kuingia kwenye ushindani na pengine nyumba kukosa wapangaji. Ufanyeje tofauti? Jenga nyumba za bei rahisi na kodi chukua kwa mwezi. Unaweza kuweka sharti kuwa mpangaji analipa fedha sawa na kodi ya mwezi mzima ambayo wewe mwenye nyumba utaiweka kama dhamana na baada ya hapo anakuwa analipa kila mwezi. Hapo hata wakati wa kutoka akiwa anadaiwa au amefanya uharibifu basi ile dhamana unaichukuwa. Lenga kwenye nyumba za kodi ya sh laki moja na kushuka chini au ikiwa ghali sana basi iwe laki tatu.
 
Nafuu kuwekeza kwenye Ardhi,
jengo linachukua miaka kurudisha pesa hasa kipindi hichi.
 
Hongera mkuu

Ushauri wa kwanza, ukiitwa PM shtuka, usiende, kimbia kabisa

Pili Nakushauri wekeza kwenye miji/majiji ya kibiashara, Dar, Arusha, Mwanza, Mbeya, Kibaha, Morogoro ni pazuri.

Nakushauri usiweke mtaji wako wote kwenye mkoa mmoja.

Jenga katika miji ambayo bado haipo peak ila imechangamka

Jenga frames za biashara na nyumba za kupanga na nyumba hizo ziwe zile standard za wastani (hizi nyumba zina wateja wengi). Aina ya 3 ya majengo ya kuwekeza, jenga guest. Ukijenga nyumba complex sana, kwanza utatumia mtaji mkubwa sana na wateja wa hayo majengo hawapo wengi sana, na majengo makubwa ni vulnerable sana inapotokea economic crisis.

Nakushauri majengo yawe ya variation hizi, sio zote guest houses, au zote frames au nyumba za kupanga tu

Tenga kama 50 milioni kwa ajili ya kununua na kuuza viwanja. Yaani ukisikia sehemu ina kiwanja kizuri kwa bei nzuri unanunua leo, kesho akipatikana mteja kwa bei ya faida unamuuzia.

Kwenye hii biashara Jenga urafiki na Maafisa kwenye Ofisi za ardhi za wilaya, Maafisa Watendaji wa Mitaa au Kata ili kuwa na taarifa current za viwanja

Jenga majengo/nyumba karibu na shule, vyuo, hospitali, Ofisi za Halmashauri, center za biashara au taasisi yoyote inayovuta watu wengi

Hongera mkuu kwa kuwa na kibunda ulicho nacho. Pongezi zaidi ni kuwa na akili ya kuomba ushauri kabla ya kuanza kuzitumbua
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii corona ndo italeta balaa maana wapangaji watashindwa kulipa kodi kwa wakati na serikali itawatetea.
Hifadhi kwanza hela yako usikilizie upepo unaendaje.
Inatakiwa kuona mbali mkuu, Corona haitadumu miaka yote
 
Mkuu hiyo biashara inalipa sana huko wilayani Kahama,

Tena utapata viwanja vizuri utajenga na wateja utapata wakutosha,
Ninaongea kitu ambacho nakijua vizuri kabisaa....

Kila la kheri mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salam wadau wa JF
Kwa wenye uzoefu wa kupanga Frame hapa Dar Es salam, bei za kupanga kwa maeneo yafuatayo :-
Mwenge
Tegeta
Bunju
Ubungo
Buguruni
Sinza
NB: Nitafurahi kama nitapata bei za kupanga Mkabala na barabara au umbali kidogo (200m toka barabarani)

Ahsante
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…