kwashilingikashambeghyu
New Member
- Jun 11, 2019
- 2
- 0
Wanajamvi wasalaam,
Mimi ni kijana, mkulima mdogo wa matunda na mbogamboga, ninapambana na hali yangu yenye changamoto lukuki. Moja ya changamoto kubwa inayonielemea ni kuhusiana na soko la hizi bidhaa ninazozizalisha, mara zote nimefika karibu na kukata tamaa kwani sijapata bado yale mafanikio ninayoyaota na jambo kubwa linalonitupa ni kuwauzia wafanyabiashara (wachuuzi) wanaokuja moja kwa moja shambani lakini sasa nimepiga moyo konde nataka nikauze mwenyewe kwenye masoko yaliyopo mjini Dar es salaam (vetenari/Sterio) kwa sasa nategemea kuvuna tani mbili za tikiti maji.
Naomba wenzangu waungwana, wenye uzoefu na uelewa mnisaidie ushauri kuhusiana na haya yafuatayo, natanguliza shukrani.
i. Tozo/ushuru ambao utanikabili katika mageti ya maliasili wakati nimejitwika kamzigo kangu kuelekea sokoni.
ii. Gharama za ushuru wa soko na madalali endapo nitafikisha mzigo wangu salama sokoni (Vetenari/Sterio).
Naomba kuwasilisha, Ahsanteni..
Mimi ni kijana, mkulima mdogo wa matunda na mbogamboga, ninapambana na hali yangu yenye changamoto lukuki. Moja ya changamoto kubwa inayonielemea ni kuhusiana na soko la hizi bidhaa ninazozizalisha, mara zote nimefika karibu na kukata tamaa kwani sijapata bado yale mafanikio ninayoyaota na jambo kubwa linalonitupa ni kuwauzia wafanyabiashara (wachuuzi) wanaokuja moja kwa moja shambani lakini sasa nimepiga moyo konde nataka nikauze mwenyewe kwenye masoko yaliyopo mjini Dar es salaam (vetenari/Sterio) kwa sasa nategemea kuvuna tani mbili za tikiti maji.
Naomba wenzangu waungwana, wenye uzoefu na uelewa mnisaidie ushauri kuhusiana na haya yafuatayo, natanguliza shukrani.
i. Tozo/ushuru ambao utanikabili katika mageti ya maliasili wakati nimejitwika kamzigo kangu kuelekea sokoni.
ii. Gharama za ushuru wa soko na madalali endapo nitafikisha mzigo wangu salama sokoni (Vetenari/Sterio).
Naomba kuwasilisha, Ahsanteni..