Ungekua Morogoro, ningekulekeza wapi pa kuanzia. Ila kama eneo ni lako na unataka kuuza mchanga, basi fanya yafuatayo;
-Anzia kwa mwenyekiti wa mtaa wako akuandikie barua
-Utaipeleka kwa mtendaji
-Ukitoka hapo nenda ofisi ya madini ambako utapewa surveyor
-Surveyor atakuja shambani kwako na kupima eneo la shamba unalotaka kulichimba mchanga. Kisha atanakili coordinates za eneo husika(zingatia utakapopata kibali cha kuchimba mchanga, hakikisha unachimba ndani ya eneo lililopimwa na surveyor kutoka ofisi ya madini)
-andaa picha za passport size
-Copy ya kitambulisho cha taifa au leseni ya udereva
-Uandae sh za kitanzania kati ya laki 4 hadi saba. Kuna vitu utatakiwa kulipia na gharama zake ni kwandola
-mwisho utalipia kitabu cha risiti na kuanza kazi ya kuchimba
-Uzuri wa barabara na upakiaji haraka wa mchanga ndo utakupatia pesa nyingi, maana gari nyingi zitakua zinakuja kwako
-Kwa sehemu nilipo mimi(Morogoro mjini). Fuso tipper ni sh 26000. Katika hiyo elf 26, gharama za wapakia mchango ni elf 10 na gharama za risiti ni sh 3000. Utabakiwa na elfub13,000 kwa kila gari.
-Kitabu kipya kinauzwa sh laki moja na nusu. Sijajua kama bei imepanda kwa sasa lakini haiwezi kushuka
ANGALIZO
-Hii biashara ni nzuri endapo ukifuata kanuni na taratibu zake. Ukileta ujanja ujanja, wale jamaa wa madini huwa wanafanya ukaguzi wa kushtukiza, huwa wanakagua kama unatoa risiti kwa kila gari linalopakia, kama unajaza muda sahihi wa gari kupakia(yaani sa ngapi na ni tarehe ngapi), jina sahihi la anaekatisha risiti. Wakija kukagua na wakakuta unakiuka hayo niliyokuelekeza, basi uwe umejipanga vizuri sana kipesa maana kesi yake wanai treat kama kuhujumu uchumi. Naongea haya from experience
-Nilikua naweza kuuza hadi vitabu 2 na nusu kwa siku na kila kitabu kina risiti 50. Biashara hii haichagui mvua wala jua. Hela utakayowekeza wakati wa ufunguzi wa mgodi huwa inarudi ndani ya wiki mbili tu. Cheza vizuri na madereva