Biashara ya mpunga

Biashara ya mpunga

Ngoja tupeane uzoefu kidogo.
2015 - 2017 niliwahi kujihusisha na kilimo cha Mpunga huko Mkoani Morogoro, Wilaya ya Mlimba, Kijiji cha Ngalimila na kupata kuishuhudia biashara hii pasipo kusikia.

Mahitaji
1. Viroba

2. Ndoo za kupimia mpunga

3. Mahali pa kuhifadhia mpunga (godown)

4. Vibarua wa kukununulia mpunga wenye utaalam wa kutosha kuweza kung’amua mpunga mzuri.

5. Mahali pa kuhifadhia mpunga (sehemu unayokusanyia mpunga)

6. Usafiri kusafirisha mpunga kupeleka godown

7. Vituo vya kukusanyia mpunga. Lazima uwe na kituo zaidi ya kimoja kuongeza nafasi ya kukusanya mzigo kwa wakati na kupunguza ushindani kwa wenzako wanaofanya biashara hiyo.

8. Fedha za kuwalipa wanunuzi kwa kila kituo ulichoweka.

Changamoto
1. Kupata mtu muaminifu wa kusimamia upatikanaji wa vijana wa kufanya kazi hiyo kwa idadi ya vituo utakavyoweka kukusanya mpunga.

2. Uaminifu wa wanaokununulia mpunga kukataa mpunga usio mzuri (Mind u that utawalipa kwa idadi ya gunia wanazokusanya so mwingine anaweza asiwe muaminifu ili apate malipo mazuri)

Ushauri
Vema kwenda mashine kusubiri wakulima wanaokuja kukoboa mpunga wao na kupatana nao bei na kukuuzia mchele, still bei yao ipo chini na gharama zitatofautiana kidogo sana na za wewe kwenda huko vijijini kukusanya mpunga.

Huko vijijini unaweza kusumbuka zaidi na mchakato mzima na mwisho wa siku ukapigwa na kitu kizito kichwani ukajikuta umenunua mpunga halafu ukikoboa unakutana na chenga kumbe mpunga ulikauka sana shambani.
Hii mbinu kuna mwamba alinifundisha mwaka 2018 kule mbingu morogoro
 
Vip ulijalbu kuifanya Na ww ndugu
Kiukweli sikuwa na mtaji ndugu nakumbuka nilichukua gunia 3 tu .... kati ya hizo moja nilipeleka kwangu kwa matumizi zilizo baki niliuza ..... ila nlijifunza kama una taka kupata mchele mzuri unaenda pale mashineni una tega kwa pale .... sema wakulima wanajuana na wanunuzi inabidi uwe na mwenyeji ......
 
Kiukweli sikuwa na mtaji ndugu nakumbuka nilichukua gunia 3 tu .... kati ya hizo moja nilipeleka kwangu kwa matumizi zilizo baki niliuza ..... ila nlijifunza kama una taka kupata mchele mzuri unaenda pale mashineni una tega kwa pale .... sema wakulima wanajuana na wanunuzi inabidi uwe na mwenyeji ......

Oky sawa sawa ... mwanzo mgum bt I wll and ntaleta feedback hapaaa
 
Habar wapendwa naomba nilete feedback hapa km nilivyo haid


Kwa bahat mbaya mda ulipofika cku kufanikiwa kuchukua kwani nilie kuwa namtegemea alipata changamoto kubwa hali iliyopelekea kushindwa kufanya kile tulichopanga so nikaamua kufanya plan b

Plan B ———> BODA BODA
niliamua kununua boda na kuingiza mtaaan kwa makatab
27/6/22boda yang ya kwanz ingawa nilie mpatia hakwenda vile itakavyo ikabd nibadlishe mtu

Huyu nilienda nae Vzr san mpaka mkataba kuisha kwa miez 10 kila cku elf 15k nikanunua ya 2 used mwez wa 9 hii nayo niliapata changamoto kwan alie itaka baadae hakutaka kuendelea na mkataba boda nilinunua kwa 1.2m jamaaa akakataaa ikabd niiuze kwa bei ya hasara
650k ndo iliuzika nilipata hasara ya 700k ikiwa pamoja na matengenezo iliniuma sana sanaaaaaa sanaaaaa

Mwez wa 1 nikanunua nyingne ,mwez wa 4 nikaongeza tena ,mwez wa 5 nikaongeza , mwez wa 9 na wa 12 nikaongeza ten ila kipnd chote nilikuwa na ongeza Pesa kweny mtaji pamoja na ile ninayokusanya

Changamoto nilizo experience

1-kuchelewa kwa hesabu mfano kila juma pili ya wk but wakat mwngne mpaka j5

2-kununua used ambayo atakae itumia c yule mwenye nayo

3-kuibiwa ingawa inaweza kuzuilika km utapata taalifa mapema coz unaweza kui lock hii km umefunga na GPRS


Faida
Faida inategemea na mkataba mlio ingia na Pesa uliyo nunulia
Ila mara nying huanzia 130-150k per moth


Mapendekezo
1) mpe mkataba mtu utakae mmudu
2) ufatiliaji Hii n ether kwa sim au kwa ana kwa ana
3) siku ya malejesho hakikisha analeta/kutuma km hana atoe taalifa siku 2 kabla
4) vijana wako wawe kalbu na unapo ish ili iwe rahc ku fatilia na kuonana mara kwa mara

Shukran [emoji120]

Ingawa ile project ya MPUNGA bado wazo lipo
 
Hiyo biashara kwa mgeni itakusumbua sana, kwani kununua mpunga kuna hitaji uzoefu wa kujua kilichomo ndani(mchele) ni mzuri?lasivyo utajikuta umenunua biliani tupu, ikawa bonge la hasara, kama utakuwa na mzoefu sawa!!kingine miaka ya siku hizi kununua mpunga na kuutunza store, haina tija kabisa, mfano unaununua kwa tsh.30, 000 wakati wa mavuno, unaweza ukauweka hata mwaka mzima ukakuta umepanda sana ni 45, 000!!!bado kuna gharama za store humo!!bora biashara ya mchele.
Upo sahihi mkuu,huku kwetu walionunua mpunga Mwaka Jana matumbo joto,walionunua Kwa 105000 na kutunza,Kwa Sasa bei ni 95000,Hali ni tete
 
Upo sahihi mkuu,huku kwetu walionunua mpunga Mwaka Jana matumbo joto,walionunua Kwa 105000 na kutunza,Kwa Sasa bei ni 95000,Hali ni tete

Duu hii hali inataka kujiludja km ile ya mwaka 2020 kama sijakosea
 
Upo sahihi mkuu,huku kwetu walionunua mpunga Mwaka Jana matumbo joto,walionunua Kwa 105000 na kutunza,Kwa Sasa bei ni 95000,Hali ni tete
Na kama hivi mvua zikipungua kwa sasa watu wakapanda fresh, msimu huu watu watalia balaa mavuno yatakuwa mengi mno!!
 
Na kama hivi mvua zikipungua kwa sasa watu wakapanda fresh, msimu huu watu watalia balaa mavuno yatakuwa mengi mno!!

Dooh mvua jana na leo dar inapga baadh ya maeneo nackia na moro nako inaendelea kunyesha
 
Back
Top Bottom