Biashara ya mtumba, mtaji laki sita, (mauzo chini 4m). Nifanyeje kuepuka usumbufu wa watendaji?

Biashara ya mtumba, mtaji laki sita, (mauzo chini 4m). Nifanyeje kuepuka usumbufu wa watendaji?

Mkuu hivyo vitambulisho bado vipo tu? Havikuondoka na mwendazake?
Hivi vitambulisho bado vipo mkuu tena siku hizi vimeboreshwa vina picha ya mtumiaji na muda wa ku-expire kulingana na tarehe ya uliyokifyatua tofauti na zamani mwaka ukipunduka na chenyewe kimexpire hata kama umenunua Oktoba.


Pia siku hizi unatakiwa uwe na kitambulisho cha au namba ya NIDA.

Lakini ni kwamba vinatumika katika eneo husika tu. Mfano ukikitolea Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kitatumika katika eneo hilo tu la utawala.



Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Hivi vitambulisho bado vipo mkuu tena siku hizi vimeboreshwa vina picha ya mtumiaji na muda wa ku-expire kulingana na tarehe ya uliyokifyatua tofauti na zamani mwaka ukipunduka na chenyewe kimexpire hata kama umenunua Oktoba.


Pia siku hizi unatakiwa uwe na kitambulisho cha au namba ya NIDA.

Lakini ni kwamba vinatumika katika eneo husika tu. Mfano ukikitolea Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kitatumika katika eneo hilo tu la utawala.



Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
Nimeona hapa pia, nadhani wamehamia kidigitali sasa. Swali ni je, Wajasiriamali wangapi wenye hizi taarifa? Tunashuhudia namna wanavyosumbuliwa na Mamlaka za kodi na ushuru kila siku.

Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali
Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeandaa mfumo wa kusajili wajasiriamali na watoa huduma wadogo.

Mfumo huu unawawezesha wajasiriamali na watoa huduma wadogo kujisajili na kuomba vitambulisho kwa njia ya mtandao.

 
Hapo sina maana ya kukwepa, ila sijafikia kiwango stahiki ili niwe mlipakodi kwenye hio biashara, elewa basi mkuu
Kodi sh 200, 000 unalipa kwa awamu nne(march, June, sept na Dec) kila awamu sh 50,000.

Acha woga.

Ili uendelee ni lazima ulipe kodi na malipo mengine ya kisheria ya Serikali.

Ukilipa Kodi unapata na Leseni ya Biashara ambavyo unaweza kutumia kukopa benki kwa lengo la kuongeza mtaji wako.

Usiogope.
 
Mauzo ya mil. 4, kwa lengo la kodi ndio nini? Hueleweki ulichoandika na unachouliza.

Mtaji laki 6, mauzo mil 4, kuepuka watendaji, Duuuh!, I see!
Unaweza kuwa na mtaji wa sh 600,000 na ukawa na sales za zaidi ya 4mil
Ni hivi
leo belo ya kwanza umeuza kwa muda wa siku 30 na sh 800,000 juml
unafata belo lingine unauza tena siku 30 unapata 800,000
Kuzungusha belo say mara 12(kwa mwaka) unaweza kuwa na mauzo ya sh 800,000 x 12 = 9,600,000 (mauzo ghafi baada ya kuzungusha belo 1 mara 12)

Umeelewa?
 
Sasa ndugu, we kipi hujaelewa hapo, kwa elimu yako unataka ueleweshwe kama mtoto wa chekechea, niweke maandishi mareeeeefu

Soma vizuri MTAJI WANGU NI LAKI 6, ILA MAUZO YAKE HAYAWEZI FIKIA MILIONI NNE KWA MWAKA ILI NIKADIRIWE KUA MLIPA KODI HALALI

JE? NITUMIE NJIA GANI KUKWEPA USUMBUFU WA WATENDAJI... KWASABABU SIJAFIKIA HICHO KIWANGO CHA MLIPA KODI... LAKINI KULINGANA NA TAMAA YA WATENDAJI, USUMBUFU HAUTOKOSEKANA,.. JE? NI NJIA IPI NITUMIE ILI KUKWEPA USUMBUFU HUO

Ndugu kama bado huelewi, mmmhh basi niache na uzoba wangu, ila kama umeelewa ruksa kunishari
Weka mahesabu kiuhasibu unaokubalika kisheria. Kama hukuweka mahesabu kiusahihi watakukadiria wao, hapo utakuwa huna ujanja.
 
Unaweza kuwa na mtaji wa sh 600,000 na ukawa na sales za zaidi ya 4mil
Ni hivi
leo belo ya kwanza umeuza kwa muda wa siku 30 na sh 800,000 juml
unafata belo lingine unauza tena siku 30 unapata 800,000
Kuzungusha belo say mara 12(kwa mwaka) unaweza kuwa na mauzo ya sh 800,000 x 12 = 9,600,000 (mauzo ghafi baada ya kuzungusha belo 1 mara 12)

Umeelewa?
Nimeelewa ndugu, asante sana.
 
Wasiwasi ndio akili mkuu, kuna rafiki yangu anaishi Tanzania na Kenya, last wiki alitoka Nairobi tukakutana somewhere katika mazungumzo yetu alinishauri na kunishawishi ni join the chain kwenye biashara ya mahindi ana network nzuri Kenya tutapiga pesa Mingu na ndio siri ya ukwasi wake, ni kweli ana pesa mingi Sasa hivi.

Sasa imagine Mimi ningekurupuka nainvest million 50 mzigo haujafika border vibali vya kuexport mahindi vimefutwa na serikali, hapo kifuatacho ni nini? Kwenda kwenye huduma ya Mwamposa au Mzee wa upako?
Vibali vimefutwa au wameweka wazi zaidi masharti? Tafadhali msaada wako mkuu
 
Kodi sh 200, 000 unalipa kwa awamu nne(march, June, sept na Dec) kila awamu sh 50,000.

Acha woga.

Ili uendelee ni lazima ulipe kodi na malipo mengine ya kisheria ya Serikali.

Ukilipa Kodi unapata na Leseni ya Biashara ambavyo unaweza kutumia kukopa benki kwa lengo la kuongeza mtaji wako.

Usiogope.
Kaka mbona umenifungua macho, sasa hii 200,000/= ni kwa mwaka mzima? Na ndio kiwango cha chini cha mlipakodi au kuna cha chini zaidi, kwa mtu mwenye mauzo ya milioni 4... Naona una kitu broo nifafanulie vizuri mkuu

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza kuwa na mtaji wa sh 600,000 na ukawa na sales za zaidi ya 4mil
Ni hivi
leo belo ya kwanza umeuza kwa muda wa siku 30 na sh 800,000 juml
unafata belo lingine unauza tena siku 30 unapata 800,000
Kuzungusha belo say mara 12(kwa mwaka) unaweza kuwa na mauzo ya sh 800,000 x 12 = 9,600,000 (mauzo ghafi baada ya kuzungusha belo 1 mara 12)

Umeelewa?
Numekuelewa mkuu wangu, kwahio basi inaonekana wamachinga wengi wana uwezo wa kua walipa kodi sema ndo ivyo tumezoea kitonga... Hivi kwa Mwenye mauzo ya milioni 4 hua anatakiwa kulipa kodi kiasi gani kwa mwaka

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Weka mahesabu kiuhasibu unaokubalika kisheria. Kama hukuweka mahesabu kiusahihi watakukadiria wao, hapo utakuwa huna ujanja.
Biashara nyingi zina mauzo zaidi ya 11,000 kwa siku, ambayo ndio milioni 4 timilifu, sasa ukitaja zaidi ya hapo... Nadhani hata makadirio ya kodi yatakua makubwa

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Sasa ndugu, we kipi hujaelewa hapo, kwa elimu yako unataka ueleweshwe kama mtoto wa chekechea, niweke maandishi mareeeeefu

Soma vizuri MTAJI WANGU NI LAKI 6, ILA MAUZO YAKE HAYAWEZI FIKIA MILIONI NNE KWA MWAKA ILI NIKADIRIWE KUA MLIPA KODI HALALI

JE? NITUMIE NJIA GANI KUKWEPA USUMBUFU WA WATENDAJI... KWASABABU SIJAFIKIA HICHO KIWANGO CHA MLIPA KODI... LAKINI KULINGANA NA TAMAA YA WATENDAJI, USUMBUFU HAUTOKOSEKANA,.. JE? NI NJIA IPI NITUMIE ILI KUKWEPA USUMBUFU HUO

Ndugu kama bado huelewi, mmmhh basi niache na uzoba wangu, ila kama umeelewa ruksa kunishari
Ila hujaeleweka, nilisoma post yako mara mbili nikashindwa kuelewa unataka ushauri juu ya kitu gani hasa.
 
Hao ambao hawajaelewa hawana uwezo wa kushauri chochote hapa. Yani mtu unashindwa kuelewa sentensi za kitoto namna hii sasa utaelewa nini maishani.
Ana mtaji wa laki 6, anatarajia kufanya mauzo ambayo ni chini ya milioni 4 kisheria ambayo ndio subjected to tax. Kama angekuwa anafika milioni 4 ndio alitakiwa akatwe kodi ila sasa hajafika hapo, je afuate utaratibu gani ili asilipishwe kodi na viongozi wa chini ambao ndio hulazimisha kulipisha kodi bila kuzingatia sana sheria.

Maelezo utapewa na wazoefu wa biashara ndogo. Na huu sio ukwepaji kodi kama wanavyosema, sio kila kibiashara chochote hata kuuza maembe ukalipishwa kodi. Ushuru, manispaa, usafi itategemea na halmashauri husika
Sasa unaanza sentensi na kashfa unajiona mjanja sana, vijana mna shida sana. Yaani kuelewa hilo ndo unaona wenzio hawataelewa kitu maishani? Mwandishi mwenyewe hatoi maelezo yaliyonyooka, kama hufikii Milioni 4 unalazimisha nini ukadiriwe kodi, kwa nini watendaji wa chini wakusumbue na sheria iko wazi.
 
Biashara nyingi zina mauzo zaidi ya 11,000 kwa siku, ambayo ndio milioni 4 timilifu, sasa ukitaja zaidi ya hapo... Nadhani hata makadirio ya kodi yatakua makubwa

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
Kama unaweka mahesabu yako vizuri na yanafata kanuni za uhasibu unaokubalika na TRA, hakuna sababu ya kukadiriwa, kama ni halali kulipa kodi, unailipa tu.
 
Back
Top Bottom