Premij canoon
JF-Expert Member
- May 27, 2018
- 1,203
- 2,771
Salaam wakuu..
Poleni na mitikasi ya january nzima, natumai wewe family yako pamoja na jamii nzima inayokuzunguka ni wazima wa afya njema kabisa.
Naam mimi ni kijana mwenzenu kiumri ninamiaka 23, Nimekua nikijishughulisha na biashara ya forex tangu baada ya kijana ONTARIO kuitambulisha hapa jukwaani nakufungua macho ya wengi ambao tulikua hayuifahamu biashara hii.
Binafsi sikuwahi kusoma pale TMT kutokana na wakati huo nilikua hata pesa ya bando ni mtihani kwangu... Nilikomaa kwakusoma PDFs mbalimbali zilizopatikana free kabisa mtandaoni, nimepmbana kwa kiasi chake na nimeshachoma accounts nyingi hadi kufikia hivi sasa. Nilichogundua biashara ya FOREX bila ya kuwa na chanzo chochote cha mapato nje ya forex ni ngumu na stress mnoo.
Tangu mwaka jana nilikua naumiza kichwa sana kutafuta mtaji kwenye FOREX nije kuwekeza kwenye biashara ya kawaida inayoonekanika kwa macho lakini nimekua nikipiga hatua mbili mbele kwenye account na kurudi hatua nne nyuma, kifupi nilipata tabu sana kukuza account, lazikini sikuweza kukata tamaa kwasababu nilikua nikiamini mambo mazuri sikuzote hayataki haraka.
Sasa mwaka huu imekua ni kama muujiza, yaani sikutegemea japokua nilidhamiria kabisa either do or die.. Kifupi niseme nilijilipua (kwa wadau wa forex watanielewa hapa) maana nilishachoka kufuata risk management na bado unachoma account taratibu taratibu hadi mwisho wasiku balance 0.
Week iliyopita jumaatano nilifanikiwa kupata settup katika pair ya VOLATILITY 75 INDEX.. Nilikua na balance ya $723, sasa niliingia kwenye hiyo trade kwa kujilipua, nilitumia lot size ya 0.20 positions 5. Nilikaa na pressure kwa nusu saa nzima nikisubiri price isogee kidogo mblele ya entry yangu au balance yangu igeuke majivu, lakini mungu alikua upande wangu baada ya price kuchezapale kwenye entry yangu hatimae ikaanza kupanda kwenda juu nakuingia upande wa profit, fasta nika lock profit kisha nikaacha market itembee (lakini nilikua na kiherehere cha kuangalia chart, maana hii pair iko volatile sana[emoji23]). Basi hadi kufika saa 9 alasiri price ilitembea hadi pips 2000 nakupelekea kuingiza $20,000+ [emoji24].
Baada ya hapo sikuchelewa... Fasta nikaingia kuwithdraw hiyo pesa na leo ndio imeingia kwenye acc yangu benki, baada yakupata email tu nikaenda ATM kuhakiki balnce yangu ni ngapi, njia nzima nilikua na kimuhemuhe hadi nimemuachia konda nauli [emoji23]. Kufika ATM mapigo ya moyo yalikua yanaenda mbio kupita maelezo huku jasho likinitoka kama nimekimbizwa.
Basi baada ya kuingiza kadi na kufuata taratibu kadhaa hatimae nakuta balance ya 46,160,000/ na chenji kadhaa. Niliruka kwa furaha maana ndio mara yangu ya kwanza kuingiza kiasi hiki [emoji24].
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Naam turudi kwenye lengo hasa lililonifanya nije hapa.
Binafsi naishi nje kidogo ya jiji la dar, fursa niliyoiona huku ni biashara ya SPARE ZA PIKIPIKI lakini nilikua nataka kuwa na duka la jumla na reja reja ili nipate kuwauzia hawa wenye maduka madogo madogo wanaokwenda dar kariakoo kufwata spare. Sina ujuzi wala uzoefu wowote wa hii biashara lakini kujifunza ni sehemu yangu ya maisha.
Sasa nilikua nauliza ili niweze kukamilisha hii project je mzigo nitanunulia china au dubai? Na je nimeepanga kuwekeza 25,000,000/ kama mtaji kwenye hii biashara kwa kuanzia... Je, kiasi hiki kitajitosheleza kufungua duka la jumla? Naombeni ushauri na mawazo vijana wenzangu [emoji1431]
Nimeamua kuleta hapa kwanza kabla ya kwenda kutafiti kwa wanaofanya biashara hii.. Naamini JF ni pana na wapo watu wanaofanya biashara hii au wenye information kadhaa zitakazonipa ABC's pakuanzia.
NAWASILISHA.
Sent from my iPhone using JamiiForums
Poleni na mitikasi ya january nzima, natumai wewe family yako pamoja na jamii nzima inayokuzunguka ni wazima wa afya njema kabisa.
Naam mimi ni kijana mwenzenu kiumri ninamiaka 23, Nimekua nikijishughulisha na biashara ya forex tangu baada ya kijana ONTARIO kuitambulisha hapa jukwaani nakufungua macho ya wengi ambao tulikua hayuifahamu biashara hii.
Binafsi sikuwahi kusoma pale TMT kutokana na wakati huo nilikua hata pesa ya bando ni mtihani kwangu... Nilikomaa kwakusoma PDFs mbalimbali zilizopatikana free kabisa mtandaoni, nimepmbana kwa kiasi chake na nimeshachoma accounts nyingi hadi kufikia hivi sasa. Nilichogundua biashara ya FOREX bila ya kuwa na chanzo chochote cha mapato nje ya forex ni ngumu na stress mnoo.
Tangu mwaka jana nilikua naumiza kichwa sana kutafuta mtaji kwenye FOREX nije kuwekeza kwenye biashara ya kawaida inayoonekanika kwa macho lakini nimekua nikipiga hatua mbili mbele kwenye account na kurudi hatua nne nyuma, kifupi nilipata tabu sana kukuza account, lazikini sikuweza kukata tamaa kwasababu nilikua nikiamini mambo mazuri sikuzote hayataki haraka.
Sasa mwaka huu imekua ni kama muujiza, yaani sikutegemea japokua nilidhamiria kabisa either do or die.. Kifupi niseme nilijilipua (kwa wadau wa forex watanielewa hapa) maana nilishachoka kufuata risk management na bado unachoma account taratibu taratibu hadi mwisho wasiku balance 0.
Week iliyopita jumaatano nilifanikiwa kupata settup katika pair ya VOLATILITY 75 INDEX.. Nilikua na balance ya $723, sasa niliingia kwenye hiyo trade kwa kujilipua, nilitumia lot size ya 0.20 positions 5. Nilikaa na pressure kwa nusu saa nzima nikisubiri price isogee kidogo mblele ya entry yangu au balance yangu igeuke majivu, lakini mungu alikua upande wangu baada ya price kuchezapale kwenye entry yangu hatimae ikaanza kupanda kwenda juu nakuingia upande wa profit, fasta nika lock profit kisha nikaacha market itembee (lakini nilikua na kiherehere cha kuangalia chart, maana hii pair iko volatile sana[emoji23]). Basi hadi kufika saa 9 alasiri price ilitembea hadi pips 2000 nakupelekea kuingiza $20,000+ [emoji24].
Baada ya hapo sikuchelewa... Fasta nikaingia kuwithdraw hiyo pesa na leo ndio imeingia kwenye acc yangu benki, baada yakupata email tu nikaenda ATM kuhakiki balnce yangu ni ngapi, njia nzima nilikua na kimuhemuhe hadi nimemuachia konda nauli [emoji23]. Kufika ATM mapigo ya moyo yalikua yanaenda mbio kupita maelezo huku jasho likinitoka kama nimekimbizwa.
Basi baada ya kuingiza kadi na kufuata taratibu kadhaa hatimae nakuta balance ya 46,160,000/ na chenji kadhaa. Niliruka kwa furaha maana ndio mara yangu ya kwanza kuingiza kiasi hiki [emoji24].
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Naam turudi kwenye lengo hasa lililonifanya nije hapa.
Binafsi naishi nje kidogo ya jiji la dar, fursa niliyoiona huku ni biashara ya SPARE ZA PIKIPIKI lakini nilikua nataka kuwa na duka la jumla na reja reja ili nipate kuwauzia hawa wenye maduka madogo madogo wanaokwenda dar kariakoo kufwata spare. Sina ujuzi wala uzoefu wowote wa hii biashara lakini kujifunza ni sehemu yangu ya maisha.
Sasa nilikua nauliza ili niweze kukamilisha hii project je mzigo nitanunulia china au dubai? Na je nimeepanga kuwekeza 25,000,000/ kama mtaji kwenye hii biashara kwa kuanzia... Je, kiasi hiki kitajitosheleza kufungua duka la jumla? Naombeni ushauri na mawazo vijana wenzangu [emoji1431]
Nimeamua kuleta hapa kwanza kabla ya kwenda kutafiti kwa wanaofanya biashara hii.. Naamini JF ni pana na wapo watu wanaofanya biashara hii au wenye information kadhaa zitakazonipa ABC's pakuanzia.
NAWASILISHA.
Sent from my iPhone using JamiiForums