Sasa zile Software za Dangerous Prayers Tayari.
mwenye moyo wa chuma aniandikie
Mkuu, na mimi pia naomba soft copies za hizo Dangerous Prayers.Sasa zile Software za Dangerous Prayers Tayari.
mwenye moyo wa chuma aniandikie
Twende kimombo, a witch na witchdoctor. Umegundua kitu gani?jamani naomba kujuzwa,tofauti kati ya mchawi na mganga! Mganga anaweza kuwa mchawi?
nilivyomwona thru prayers, siyo mwanachama wa illuminat-freemasons wala devil worshipper. bali kipa huyu maarufu wa kilabu kikubwa tu nchini,yeye ni devil Disciple. anapokuwa langoni yaani golini, anayasambaza mapepo [vishetani vidigo] zaidi ya ,MIA MOJA ndani ya penati-box. ili kuwachanganya timu pinzani. ingawa amepewa masharti magumu sana na wakala wa CHINI YA MAJI, anajitahidi kwa bidii zake zote kuyatimiza [sipendi kuyataja masharti hayo.-yana kinyaa sana] LAKINI kila anapojiunga na timu yoyote ni lazima yale Madudu aliyobebeshwa yamshambulie sana Golikipa atakayemkuta mpaka akimbie sasa nimesikia anataka kwenda azam fc. watahadharisheni sana, wasije umia
NB; zile software za Dangeruos prayers tayari kwa 3000. nitakujulisha namna ya kupata ili ujisimamie wewe mwenyewe kataka kusambaratisha makafara, mazindiko, maajini na kazia za Lusifa kwa jina la YESU
Mkuu lakini mbona huwa anafungwa? anafungwaje kama huwa ana majini ya kumlinda? Na juzi tu tumefungwa 2?
Sasa hivi zipo shule kabisa za kufundisha uchawi nchini Tanzania, Shule moja ipo Temeke masomo yake huchukua miaka saba hadi unahitimu.
Ukimaliza Temeke, unaweza kujiunga na elimu ya juu katika fani ya uchawi, chuo kipo Tanga hapo wanatoa digrii ya kwanza ya uchawi kwa miaka mitano.
Wanatoa pia digrii ya pili ya elimu ya ulozi ambapo utakaa darasani kwa miaka mingine mitano.
Master digrii ya ulozi, bado hapa nchini hakuna chuo, inapidi uende Mombasa nchini Kenya ndipo kilipo chuo kikuu cha elimu ya ulozi.
jamaa yangu mmoja aliwahi simulia habari ya kgm inatisha, anasema aliingia chini ya maji ziwani na kumkuta mwenyejiwao lakini sehemu hiyo ya chini ilikuwa kavu tu -
alipelekwa na kigagula kilichokuwa kimemuhusudu tu kwa kuona aina ya mabangili aliyokuwa anavaa mkono wa kushoto(kama wamaasai), jamaa yangu huyo ana asili ya south africa, aliondoka kwao kipindi cha machafuko ya 76 akawa mkimbizi. kwa sasa yupokwao serikali imemsaidia kuseto.
simulizi hiyo ni ndefu na ya kusisimua sana.
Amani yetu inatumiwa vibaya.
Mkuu lakini mbona huwa anafungwa? anafungwaje kama huwa ana majini ya kumlinda? Na juzi tu tumefungwa 2?
Usafiri wa ungo upo wa aina nyingi, upo usafiri wa ungo unaotumia wanyama, upo usafiri wa kutumia fagio, upo usafiri wa kutumia fimbo, upo usafiri wa kutumia ungo.
Wachawi wote wana roho ya uchawi, roho ya uchawi ni roho inayokufanya uweze kupita eneo ngumu na kutokeza upande wa pili, kwa mfano wachawi wanapowanga usiku roho hizi huwafanya kuingia katika nyumba yoyote na kuwafanyia uchawi usiku watu waliolala ndani ya nyumba hizo bila ya kuonekana. Isipokuwa nyumba za walokole haziingiliki kabisa.
Roho za uchawi zinawawezesha wachawi kujibadilisha maumbo yao, kutoka maumbo ya kibinadamu na kugeuka kuwa paka, panya, kunguru n.k.
Wanapotaka kusafiri anakuwa na vifaa vyake vya kichawi, kisha huomba dua akinuizia majini yampeleke sehemu fulani, roho yake ya uchawi na majini humuinua juu angani kwa kasi hadi eneo alilokusudia. Usafiri wa aina hii ni hatari kwani unaweza kutunguliwa kirahizi ukiwa angani.
Usafiri wa kutumia wanyama kama fisi, hutumika kwa nchi kavu tu, hawawezi kuvuka bahari kwenda visiwani au nchi za mbali.
Usafiri wa kasi sana ni wa kutumia fimbo, kabla ya kuanza safari, unaomba dua ya manuizo na kukanyanga incha moja ya fimbo, roho ya uchawi na majini hukuinua juu angani, kama unataka kwenda Nigeria kutoka Dar, utaonyeshwa njia yote ilivyo, kama kuna hatari yoyote huonekana, na inabidi uhairishe safari, kama njia ni nyeupe, unatakiwa ukanyage incha ya pili ya fimbo, na safari huanza kwa kasi ya sauti. Kwa sababu safari ni ya kasi sana na upepo ni mkali sana, kiasi kuwa huwezi kufika ukiwa hai, majini huchomoa roho yako ndani ya mwili wako na roho kukutangulia mbele, mwili wako huikimbiza roho yako ukiwa katika hali ya umauti, unaweza kutumia sekunde 10 kufika Nigeria, lakini ni usafiri wa hatari kuliko zingine, usafiri huu hujulikana kama usafiri wa kujichinja.
Wachawi wa Marekani na bara Ulaya wao hutumia sana usafiri wa fagio.
I had an experience once when my spirit confirmed to me the person whom I had contract with na akataka kunirusha na kushindwa siku ananipa hizo pesa zangu basi hazikuwa salama...something was telling me that its not all well..Then ikawa kama nawaza vile kwamba I am protected but my drivers who worked for the contract were not safe..So nika enda nakuwaeleza of course kama you are a non believer si rahisi uamini and one of my driver told me usijali mimi hawezi kunifanya jambo lolote. Atfter a less than a week the same driver akaanza kuugua akalazwa hospitali...things turned to be very bad kabla hajatoka mkewe akalazwa na baadaye mtoto wake mdogo..then hatuja kaa vizuri the other driver things were not going through yeye sikuile ninawaambia aliniangalia tu lakini nikamsoma kanielewa but anajua atakacho fanya siyo vile mm na mwambia..baada ya mwezi akaacha kazi naona akaona mmh mambo si mambo kwa shetani hayuko sawa sawa na kwa Mungu hataki kuja....
Some how I have learnt on some of the things unazoeleza hapa..I realy know what you are talking about; Lakini uchawi ni power ya chini kabisa kwenye Kingdom of darkness, marine waters ndo wanaongoza ila wanapokutana na moto wa roho mtakatifu ambao ni utakaso kwa watakatifu na ni moto ulao kwa waovu basi ni kama kumuua nzi kipande cha gazeti tu chini....dada mmoja alikuwa mchawi and was shown into spirit siku ile nimemfuata kabla sijaongea akaanza kupiga kelele na kuniambia yote anayojua kuhusu uchawi; it was my first experience kumsikia mchawi live niliona kama vile naota vile everybody was surprised...From then nikaamini kumbe ni kweli uchawi upo, I used to doubt very much about the existence of it. One year later niko ulaya ndani ya train mbele yangu alikwepo binti so akanigeukia kwa hasira kwanini unanipulizia pumzi ya moto nikawa na shangaa imagine nchi ya watu mzungu anakupigia kelele, nikadhani ni racist mara akafungua mlango wa train (zile kama daladala) bado ilikua haijaondoka kilichofuata duuh akavua nguo hadharani hapo hapo akaanguka chini akajikojolea maskini and the lady was in her days it was a disaster na mm kumwendea na ogopa nisije funguliwa mashitaka, mara akapata fahamu akaja akaniambia what powers do you have nikamwambia holly spirit...akaondoka bila kuaga mtu...Kila mtu akabaki ananishangaa kama sinema vile na mimi nikabaki kimya kama siyo mm vile; it was realy a bad experience for me lakini nika comfirm kumbe siyo wote waliobarabarani ni wema....
Asili ya uchawi na majini ya nchi za Kiafrika ni kutoka Arabuni, ndiyo maana utakuta majini mengi yana majina ya Kiarabu. Miji au vijiji walivyokaa Warabu ndivyo vinaongoza kwa uchawi na havina maendeleo. Lakini utashangaa pia kuwa mtu kama Osama Bin Laden ambaye ni Mwarabu amefundishwa uchawi na Mtanzania wa Kigoma.
Hebu tufafanulie hapo kwenye wino mweusi ndugu tupate kuelewa .Nchi ya Japan ni mojawapo ya mataifa yanayoongoza duniani kwa maendeleo.
Wajapan wanazo dini kuu mbili ambazo ni Shinto na Buddha, asili ya dini ya Shinto haijulikani sana lakini imekuwepo nchini Japan kuanzia miaka 400 kabla ya Kristo. Buddha iliingia nchini Japan mwaka 538 ikitokea China, Wajapan wengi hawakuipokea hii dini hadi mwaka 587 wakati ufalme wa Mononobe uliposambaratishwa kwa kipigo, walikuwa ni wapinzani wakubwa wa dini ya Buddha, kuanzia kipindi hicho dini hiyo ilienea kwa kasi ya ajabu.
Baada ya karine mbili Mfalme Shomu's aliamuru ujenzi wa nyumba ya ibada ya Todaj-ji ijengwe kuanzia mwaka 752. Ni jengo kubwa la mbao duniani likiwa na urefu wa mita kumi na tatu, ndani yake waliweka sanamu ya shaba ya Buddha, baadaye ilibadilishwa na kuitwa The Great Sun Buddha au Dainichi Nyorai, Dainichi Nyorai wana uhusiano na Amaterasu na Shinto Sun Goddess.
Asili ya Japan ni nchi inayokumbwa na matetemeko makubwa ya ardhi ambayo yamekuwa yakisababisha maafa makubwa kwa raia wa Japan, kupitia dini zao kuu mbili Shinto na Buddha, ambazo asili yake ni kuzimu, waliazimia kuwa kila familia ya Kijapan ni lazima watoe Yen 3,000 kila mwezi kama sadaka kwa mizimu, kuwalinda na matetemeko ya ardhi yanayowakumba mara kwa mara.
Sadaka hiyo inapokusanywa hupelekwa kwenye hekalu lao la Todaj-ji, na watu wenye miili kabisa kutoka kuzimu hufika ndani ya hekalu hilo na kuchukua magunia kwa magunia yalijaa pesa za Yen, na kupeleka kuzimu. Inapotokea maafa kama haya ya jana, Mabuddha huanza ibada zao za kishetani na mizimu iliyovaa miili ya binadamu hufika na kuwaeleza ni kwa nini wameadhibiwa.
Kimsingi malalamiko ya mizimu wanapinga kuanza kuenea kwa dini nyingine zisizoamini mizimu katika taifa lao, ambao wanaona ni tishio kwa uchumi wa taifa la kuzimu kimapato, endapo Wajapan wataacha dini zao za Buddha na Shinto.
Aliyekuwa mchawi mkuu wa serikali ya Tanganyika na baadaye kubadilishwa jina na kuitwa Tanzania Yahaya Huseini amefariki dunia leo tarehe 20 Mai 2011.
Yahya aliingizwa kwenye system ya nchi na Waziri mkuu wa kwanza wa serikali ya Tanganyika marehemu Julius Kambarage Nyerere, baada ya kushauriwa na waganga wa kishenzi wa Bagamoyo, kabla ya kupata uhuru wa Tanganyika. Siku hiyo Nyerere alizuru lango kuu la kuzimu la Zazuni, Bagamoyo alipokwenda kufanyiwa uganga. Yahaya alikuwa bado kijana mdogo aliyependwa sana na viongozi wake, na alikuwa na kipaji kikubwa cha mambo ya unajimu na ulozi. Yahaya akiwa ndani ya ikulu ya Dar es Salaam, alitengeneza jini aliloligeuza umbo na kuwa fimbo, Yahaya kwa msaada ya lango la kuzimu la Mustallah waliomba watengenezewe saa ya kijini pia ambayo, kama kuna jambo lisilokuwa la kawaida saa ilikuwa inabadilika rangi kwa ndani na kuwa nyekundu.
Nyerere ambaye kwa asili yake ya kabila la Kizanaki, ushirikina ni jambo la kawaida na mara nyingi alikuwa akihudhuria matambiko yote yaliyokuwa yakifanyika kijijini kwake. Jina la Kambarage ni jina la mzimu wa mvua, marehemu ndiye alikuwa kiongozi wa mzimu huo, na ndiyo maana aliamua aitwe jina la muzimu huo wa mvua, KAMBARAGE.
Yahaya akitumia ujuzi wake wa unajimu wa kuchukuwa kichawi nyota za watu zenye vipawa vikubwa, alimsaidia sana Nyerere, baada ya kumpatia nyota ya utawala, kuongea kwa ufasaha na mvuto. Kwa kawaida kipawa chochote kutoka kwa Mwenyezi Mungu hasa kwa kiongozi, mtu unakuwa umekamilika kila idara, ndiyo maana leo hii ukisikiliza hotuba za Nyerere, unabaki kushangaa, kama mtu huyu na mawazo kama haya alishindwa vipi kuyatekeleza kwa vitendo, wakati serikali yote ilikuwa chini yake na maamuzi yake mbona hayakuwa yanatekelezwa. Binadamu tunazaliwa na vinasaba vinavyofanana kifamilia kutoka mababu wa zamani na vinasaba hivyo huendelea kuridhiwa na watoto na wajukuu, ndiyo maana kwa bahati mbaya vinasaba hivyo havisikiki kwa watoto wake wala wajukuu.
Yahaya aliendelea na nafasi yake ya mchawi mkuu wa taifa baada ya uongozi wa nchi kuwa chini ya Ali Hasani Mwinyi, majukumu makubwa ya wachawi ni kudidimiza na kuharibu maisha ya watu, hivyo kwa kutumia lango la kuzimu la mustallah la upanga, siku zote mipango yao ilikuwa ni ya uharibifu, ndiyo maana mzee Mwinyi kila akijitahidi kubadilisha hali ya maisha ya wananchi, alikuwa akiishia kubomoa misingi ya uchumi wa taifa.
Yahaya baada ya kumudu kuwadhibiti watawala hawa, kuzimu walimpandisha cheo, na kuwa mkuu wa lango la kuzimu la mustallah. Nyumbani kwake Mkwajuni Kinondoni alichimba bwawa la kuogelea, lakini hiyo ni geresha, siyo bwawa la kuogelea, bali ni lango kuu la kuingilia kuzimu, ndiye mchawi pekee, kama anavyosifiwa wa Afrika Mashariki na Kati kuwa na lango binafsi la kuingilia kuzimu. Usiku alikuwa akiingia ndani ya bwawa lake na kutambaa chini kwa chini ya ardhi hadi anaibukia juu ya lango la kuzimu la mustallah, upanga. Wachawi karibu wote hupaa angani kwa ungo, lakini mkongwe wa ulozi alikuwa anapasua udongo na miamba chini ya ardhi na njia inatokea.
Awamu ya tatu ya Benjamin, aliendelea na cheo chake kile kile cha mchawi mkuu wa taifa, jukumu kubwa likiwa ni uharibu wa maisha ya wanadamu, kipindi hiki yalijitokeza mambo makubwa ya uharibifu huko kuzimu, na kafara kubwa kubwa zilitakiwa, kafara kubwa mara zote zinatakiwa damu za binadamu kunyamazisha kuzimu. Kumbuka ajali ya meli ziwa victoria, kumbuka ajali kubwa kubwa zilizomaliza maisha ya Watanzania barabarani, kumbuka ajali za treni za abiria kila wakati kipindi chote cha utawala wa Mkapa. Mpango mkubwa ulioshindikana ni wa kuangusha ndege ya abiria ya precisios iliyokuwa inatoka Mwanza kuelekea Dar, kuzimu walishapanga mwezi, tarehe, siku na saa ya kuiangusha ndege hiyo juu ya soko kuu la kariakoo. Ilikuwa ni bahati mbaya sijui, ilikuwa ni bahati nzuri sijui lakini waliingia abiria wawili ndani ya hiyo ndege, abiria hao kuingia kwao ni baada ya abiria wengine wawili kuahirisha safari yao ya kwenda Dar hivyo tiketi zao zikapatiwa ruhusa ya kusafiri na ndege hiyo, watu hao walijulikana kama walokole, ndege ilipofika katika anga na eneo la maafa, mitego ya kichawi iliteketezwa, kwenye ulimwengu usioonekana moto ulilamba wachawi waliokuwa wamejipanga na madumu ya kuchukulia damu, misingi ya kuzimu ilipasuka, tangu siku hiyo makafara yaliyohitaji damu yalipugua sana.
Awamu ya sasa ndiyo aliwathibitishia Watanzania kuwa yeye ndiye mchawi mkuu wa taifa, anayetoa ulinzi usioonekana. Kumbuka mwaka 2005 nyota ya kilozi ilivyokuwa iking'aa kwa kiongozi wetu, inashangaza nyota imefifia kwa kasi ya ajabu, haijulikani kesho itakuwaje. Uchumi wa taifa upo kitandani Muhimbili, wananchi wamekosa matumaini makubwa baada ya ahadi kubwa kubwa walizopewa.
Ni lini taifa litapata viongozi wanaomuogopa na kumtegemea Mwenyenzi Mungu na kuzivunja laana hizi za kichawi zinazolitafuna taifa tangu mwaka 1961 ?
Je nafasi ya mkuu wa wachawi wa taifa itafutika, au ipo wazi kwa muda?
Wachawi huwa wanajigeuza maumbo ya miili yao wanapofanya ulozi nyumbani kwa watu. Wapo wanaojigeuza maumbo yao na kuvaa maumbo ya mbu, mijusi, nyoka, panya, paka, chura n.k.
Wachawi wengi hupendelea sana kuvaa maumbo ya paka, ndiyo maana unaweza kusikia paka analia nje ya dirisha lako usiku, lakini unapotoka humuoni huyo paka, au unasikia paka analia ndani ya nyumba lakini unapomtafuta humuoni. Wapo paka waliozoeleka kuingia nyumbani kwa watu, wenye nyumba wakifikiri ni paka mnyama, kumbe siyo.
Ipo sababu moja kubwa inayofanya wachawi wengi wa nchi kupendela sana kuvaa maumbo ya paka. Paka ana tabia ya pekee kabisa anapolala usingizi, paka kwa muda wa masaa 24, hulala masaa 13 bila kupungua wala kuzidisha, na masaa 11 huwa yuko macho bila usingizi. Kulala kwake ni dakika 3 kisha huamka, analala tena dakika 4 au 5 na kuamka hadi anafikisha masaa 13 kamili ya usingizi kwa siku.
Tabia hii ya paka ndiyo inawafanya wachawi wengi kupenda sana kuvaa umbo lake, kwani muda wa kulala ni mfupi mfupi kiasi kwamba, mchawi anaona matukio yote yanayotendeka eneo alilokusudia kuwanga.
MAMA POROJO na Majimoto waitwa hukuHapo nakubaliana na wewe, ile ajali ilikuwa imekaa kikiini macho sana, ninaamini kabisa kuna uhusiano wa hiyo ajali na nguvu za kuzimu. Swali langu kwako ni nini mustakabli wa kiroho wa watu walio poteza maisha yao kwenye ajali ya MV Bukoba? I mean je walienda kuzimu ama peponi au sehemu zote mbili kulingana na uhusiano wao na Mungu?. Je walichukuliwa misukule au ? Tafadhali nahitaji kujua hapa
Asa'rile, naomba hizo software
Sosi pliiiiiiiiiiiizi, ni own research findings(tupe ststisticalsuport) au uliota usiku?.