Biashara ya Uchawi Tanzania


Mkuu simulizi zinatisha... unafanyeje kupona na haya majitu?
 
Usijali jicho langu litakupa ulinzi.

We Majimoto ni kwamba haya mambo unaexperience nayo au na wewe ni wakusimuliwa na kusoma vijarida na kuamini? Kama alivyosema VoiceofReason kila umuulizae atakwambia kuwa na yeye anasikia hebu tupe nyuzi za uhakika kwa mfano labda ulishawahi kuwa mchawi then umeamua kutoboa siri za kichawi au bado umo kundini ila umeamua kuvujisha data!
Mi binafsi sina uhakika na haya mambo sijui kuna magari ya kichawi sijui kuna watu wanatembea barabarani halafu hawaonekani, sijawahi kuona wala kushuhudia tukio lolote la kichawi so siamini kabisa hayo mabo,,, truth is never told but must be realized!
 
Haya mambo yapo mimi wakati mdogo (late eighties or early nineties) pale viwanja vya mnazi mmoja nilishuhudia Emmanuel Eni (yule Mnigeria aliyekuwa mchawi ila baadae akaokoka) akihubiri (akielezea maisha yake) jinsi alivyoishi maisha haya. Alisimulia hivyo vyou alivyopelekwa kusoma (INDIA) na jinsi alivyokuwa anasababisha ajali.

Pia alieleze jinsi alivyolishwa maji ya maiti (yaani maiti inafukuliwa halafu inamwagiwa maji ili mchizi uwe na harufu ya maiti) ili anywe. Nakumbuka hata tuliwahi kununua kitabu chake na nilikisoma japo kuwa ni miaka mingi imepita (kama 20+) bado nakumbuka vipande vipande vya huo mkasa. (Mwenyewe nime shangaa kukumbuka hata jina lake na kugoogle)

Haya mambo yanatisha sana ila ukiwa na Yesu huwezi kuogopa kwasababu aliyashinda yote hayo.

Kuna link hii nimeipata toka google ambayo ni kitabu alichoandika yeye mwenyewe Emmanuel Eni kuhusu maisha yake kinaitwa:

Delivered From The power Of Darkness
 
LANGO LA KUZIMU LA PANGANI, TANGA

Pangani ni mmoja ya miji ya zamani sana, upo kiasi cha kilomita 35 kutoka Handeni, kama unauwezo wa kuchapa mguu sawasawa itakuchukuwa muda wa masaa matatu hadi manne kufika Pangani. Maendeleo ya mji huu yamedumaa, sawasawa na miji mingine mingi iliyokaliwa na Waarabu, licha ya kuwa na vivutio vingi vya utalii.

Ushirikina ndiyo shughuli kubwa katika mji huu, na hapo lipo lango la kuingilia kuzimu linalojulikana kwa jina la RAJUNI, lango hili lipo ndani ya bahari ya Hindi. Na linahudumiwa na majini makali kumi na mawili yafuatayo. (inashangaza sana kuwa malango yote ya kuzimu yanahudumiwa na majini kumi na mawili)

1. Shadirun hili ni jini linalosimamia magonjwa ya ngozi, na fungus zisizosikia dawa na zinazowasha sana hasa katika sehemu za siri.

2. Fadhan ni jini wanalotumiwa sana na wachawi kutambua kinga ya mtu, kabla ya wachawi hawajaenda kumfanyia ulozi. Hutumwa sana kwa walokole na huweza kutambua walokole feki na walokole wasioingilika.

3. Baraji ni jini linalosimamia uvivu hasa kwa wanawake. Jini hili likitumwa kwa mwanamke anakuwa mvivu kweli kweli kwa kazi za nyumbani hadi kitandani.

4. Shamsu ni jini linalo vaa umbile la binadamu. Utakuta msichana ni mzuri sana kwa sura na tabia lakini haolewi. Akitokea mvulana kumchumbia hili jini humwingia msichana na kumvika sura bandia, mvulana anapomtizama msichana anachanganyikiwa kwani anaona siye yule aliyekuwa anamtaka, hivyo anapigwa chenga hadi uchumba unavunjika. Akijitokeza kijana mwingine hali huwa ni ile ile ya kuachwa. Wasichana wengine hufunikwa kwa sura bandia kiasi kwamba tangu azaliwe hajawahi kukutana na mvulana walao wa kumtakia neno nakupenda.

5. Amri ni jini linalosimamia hasira. Utakuta mtu anakuwa na hasira hadi anatetemeka na mapovu yanamtoka mdomoni.

6. Tahimu anashughulika na kutambua nyota za watu, kisha wachawi huzichukuwa na kufanyia biashara.

7. Tajirin hili ni jini linalosimamia utajiri. Masharti ya kulimiliki ni lazima uwape mtoto wako wa kuzaa au mke wako apooze upande au ufanye mapenzi na mama yako mzazi. Kisha ni lazima usaini mkataba wenye masharti magumu sana kama usilale kitandani, usipande gari, usile aina ya vyakula nk.

8. Al Taliki hili ni jini la kupoteza watu. Kama kuna watu wanamtaka mtu fulani, wachawi hutuma hili jini nalo huvaa mwili wa binadamu na kwenda eneo au sehemu anapoishi huyo mtu. Likimwona huwita kwa vidole na watu wengine wanakuwa hawamuoni isipokuwa mlengwa peke yake, kisha huanza kumfuata jini kwa nyuma,jini akikimbia na huyo mtu naye hukumbia hadi anamfikisha kwa wachawi.

9. Naruju ni jini linalosimamia lugha, wapo wanao nena lugha kwa kupagawa na majini na wapo wanao nena lugha kwa nguvu ya Mungu ambayo inawapa taabu sana kuzimu kwa moto unaounguza.

10. Janjatus ni jini linalotumwa kuwafanya watu walale usingizi mzito wakati wa adhana na wakati wa mahubiri kanisani.

11. Riaru jini hili likimwingia mtu anataka afanye kila kazi peke yake.

12. Zaituni ni jini linalosimamia watoto wa kike kutembea kwa maringo na mikogo.
 

Kumbe kuna biashara inaendelea hapa
 

Kwenye red hapo, hao lazima watakuwa ni FFU wa Bongo tu.
 

Nimesoma hiyo link aisee nimeogopa kumbe kuna mambo yanafanyika mengi sisi hatuna habari, Mungu na Atusaidie
 
nasikia kikwete ana mchawi wake bagamoyo....pale jk unavyomuona ana hilizi kama 5 anatembea nazo....
 
Mkuu MMoto, wewe ni msaidizi wa sheikh YY nini? naona umebobea kwenye hili :A S-coffee::A S-confused1:
 

Hapo kwenye nyekundi mapigo ya moyo yameruka, ukizingatia niko ofisini alone
 
Jamani members! nilipoanza kusoma hii thread, Hili jicho kwenye avater ya majimoto lilikua linablink. sasa hivi liko kimya. au ndio majini yenyewe?
 
kaazi kwelikweli kama utaenda kijiji kimoja ukajumuisha mkoa basi gt imepata maana mpya , no reserch no data jamaa kamwaga matokeo cjui ya nini:decision:
 
We ni Shehe Yahya, au mwanae au msaidizi wake?
 
We mchawi Majibaridi.... Dowans wamelipwa? Wanafunzi wa shule wanaokaa chini tuwasaidieje waondokane na shida hiyo? Kina mama hospitalini wanaokosa dawa na matibabu?
 
Baada ya biashara ya mitumba kuruhusiwa hapa nchini, wafanyabiashara wamekuwa wakiingiza kila aina ya nguo na vyombo vya aina mbalimbali.

Moja wapo ya bidhaa ambayo inaingizwa kwa wingi nchini ni wanasesere (midoli) zikiwa katika maumbo mbalimbali kama mbwa, paka, watoto, nyoka, chura nk.

Shetani akisaidiwa na wachawi wa nchi siku zote huwa wanatafuta milango ya kuingilia ndani ya maisha ya mtu, mara nyingi wachawi na majini huwa wanavaa maumbo ya panya, paka, mbu, nzi, mjusi kafiri kuingia kwenye makazi ya watu na kuwafanyia ulozi.

Siku hizi baada ya watu wengi kununua na kumiliki madoli, utakuta chumba cha mapumziko kimepabwa kwa madoli aina mbali mbali, kama wana watoto, utakuta chumba cha kulala watoto kimejazwa madoli, watoto wakicheza nayo. Magari nayo yamekuwa yakipambwa kwa midoli ya kila aina.

Wachawi wa nchi wakiingia ndani ya nyumba yako, wanachofanya ni kuweka majini yao ndani ya hiyo midoli au midoli sasa hivi ndiyo makazi ya wachawi na majini ndani ya nyumba yako, ndiyo maana tangu ununue hiyo midoli maradhi ya ajabu hayaishi nyumbani kwako.

Huu ni ushauri wa BURE kwa yeyote mwenye kuwa na sikio la kusikia na asikie, mwenye macho ya kusoma na akasoma hii habari na kuielewa, ataamua mwenyewe linalokupasa kutenda.
 
 
ZAZUNI Lango la kuzimu la Bagamoyo

Mji wa Bagamoyo ni mji wa kizamani uliokaliwa na Waarabu, na maendeleo yake yalikuwa duni sana hadi siku za hivi karibuni, wageni walipoanza kuingia na kuwekeza katika mji huo.

Lango la kuzimu la Zazuni liko ufukweni mwa bahari ya Hindi, likihudumiwa na majini kumi na mawili.

1. Ruyat ni jini linalosimamia ndoto mbaya

2. Al-Rahab ni jini linalosimamia shoti ya umeme na majanga ya moto, mfano wa majanga ya moto yaliyotokea katika mabweni ya kulala wanafunzi katika shule nyingi, jini hili lilihusika na kuwachukua watoto kuwapeleka msukuleni. Watoto hawa wote wapo hai, tangu vita hivi vya shetani vilipoanza mkoani Kilimanjaro katika shule ya wasichana ya Shauri Tanga, watoto hawa wanaishi katika mateso makubwa makubwa ajabu.

3. Hadarash ni jini katili sana linaloua kwa kukata shingo na kunyonya damu ya mtu

4. Anazihad ni jini linalokamata roho ya mtu, kisha mtu anaonekana amekufa, baada ya mazishi, wachawi huja na kusoma dua kaburi funguka na jini huiachia roho ya marehemu, ufahamu unapomrudia, wachawi huondoka naye.

5. Zuzuk ni jini la maafa. Jini hili likiingia mtaani au kijijini, hutokea vifo vingi sana, kila siku watu wanazika.

6. Munkar ni jini la makaburini. Jini hili linakutokea kwenye ndoto kama babu, bibi au mzazi wako waliokufa zamani, likiwataka mfanye jambo fulani au familia itaangamia. Kimsingi unapotekeleza maelekezo ya jini, mtakuwa mumejifunga wenyewe kwa kamba ya kifo toka kuzimu, na matatizo makubwa ya magonjwa na vifo huanza kwa familia.

7. Tatazu ni jini la uasherati, unafanya tendo la ndoa bila kujali magonjwa au uko kwenye kipindi cha hedhi.

8. Rabdi ni jini linalotumwa kwa Waislamu peke yake, kwa ajili ya kufanya fujo.

9. Balshebe ni jini linalosimamia magonjwa na madhaifu ya mwili

10. Sajidur ni jini linalosimamia pesa. Likitumwa kwako mshahara wako unapotea katika matumizi ya ajabu ajabu.

11. Subrah ni jini linalosimamia mafarakano, na kutokuelewana kwa viongozi wa Makanisa.

12. Lair Labi ni jini linalosimamia hofu na kukata tamaa.
 
Maji Moto!
Where the hell do you get all this information?
Do you dream, are you getting it from your sunday school?
Please come up with an answer. Am deadly scared.
my bed is full of dolls. my sitting also. Ina maana naishi na majini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…