Biashara ya Usafirishaji kwa Bajaji: Ueandeshaji, Changamoto, Faida na Ushauri

Biashara ya Usafirishaji kwa Bajaji: Ueandeshaji, Changamoto, Faida na Ushauri

Biashara ya Bajaj ni nzuri kama utaendesha wewe mwenyewe.

Tena ndani ya muda mfupi utarudisha fedha zako, lakini bajaj za hesabu ni pasua kichwa maana kuna madereva ni mchwa hatari.

Yaani hesabu iwe kubwa au ndogo mambo ni yaleyale.

Wengine watakuja kuamsha asubuhi akipiga round 2 za mwanzo then anampa Nyoka wake (deiwaka) anaipiga hadi saa usiku then dereva wako ndio anairudisha.

Na ubaya kila dereva ana mkono wake so mwisho wa siku utasikia Clutch inasumbua mara Block imetanuka mara hiki mara kile.

Bora hiyo ela ya Kununua Bajaj ufungulie duka la kuuza Spare za Bajaj na Pikipiki maana utapata Return ya Maana ambayo ni zaidi ya 20,000 ya hesabu ya Bajaj kwa siku.

Chamsingi weka vitu vinavyouzika haraka kama Filter Oil, Rubber, Seal, taa, shock ups, urembo urembo, valve nali, plug, betri, matairi na tube zake, compressor ya upepo.

Utaiona hela na utashangaa kikubwa upate Location ya Maana yenye vyombo hivyo vingi..
Chukua hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni Mwalimu kwa ngazi ya degree nataka nianze biashara ya bajaji dodoma ya kusafirisha abiria ndani ya jiji la Dodoma mjini, naombeni ushauri juu ya hili, nataka nichukue mkopo wa milioni 14 ili nichukue bajaji 2 ili niweze kujikwamua kimaisha maana maisha ya kutegemea mshahara tu sio kabisa, naombeni mniambie Bank ipi nzuri naweza chukua mkopo huo wa milioni 14.

Pia naomba kujua changamoto za hii biashara pia namna ya kupata bima kwa ajili ya hizo Bajaj kwa taadhari ya wizi au ajali za barabarani ili niweze kuwa upande salama maana marejesho ya hela za watu nitakatwa kwenye mshahara wangu.
 
Biashara ni nzuri tatizo no hao vijana wa kufanya kazi. Tafuta wale wachamungu. Tafuta kijana mwenye mke au yeyote mwenye majukumu ya kulea awe amesajiliwa na kituo cha bajaji chochote. Hakikisha unajua bajaji zako huwa zinapaki wapi na usiku huwa zinalala wapi.

Service kubwa sana ni kumwaga oil kila baada ya week mbili, kama pea ipo mwaga kikaa baada ya week1
Bajaji inafanya kazi siku6 ya saba unamuachia atafute pesa zake.

Isiyo ya mkataba kwa siku ni 20000 *6 =120000 kwa week kwa mwezi ni 480000 na kwa miezi kumi ni 4800000 bajaji isiposumbua, wala dereva asipokusumbua kwa visingizio vya misiba, ugonjwa.
 
Biashara ni nzuri tatizo no hao vijana wa kufanya kazi. Tafuta wale wachamungu. Tafuta kijana mwenye mke au yeyote mwenye majukumu ya kulea awe amesajiliwa na kituo cha bajaji chochote. Hakikisha unajua bajaji zako huwa zinapaki wapi na usiku huwa zinalala wapi.

Service kubwa sana ni kumwaga oil kila baada ya week mbili, kama pea ipo mwaga kikaa baada ya week1
Bajaji inafanya kazi siku6 ya saba unamuachia atafute pesa zake.

Isiyo ya mkataba kwa siku ni 20000 *6 =120000 kwa week kwa mwezi ni 480000 na kwa miezi kumi ni 4800000 bajaji isiposumbua, wala dereva asipokusumbua kwa visingizio vya misiba, ugonjwa.
Nashukuru sana kwa mawazo yako mkuu.
 
Biashara ni nzuri tatizo no hao vijana wa kufanya kazi. Tafuta wale wachamungu. Tafuta kijana mwenye mke au yeyote mwenye majukumu ya kulea awe amesajiliwa na kituo cha bajaji chochote. Hakikisha unajua bajaji zako huwa zinapaki wapi na usiku huwa zinalala wapi.

Service kubwa sana ni kumwaga oil kila baada ya week mbili, kama pea ipo mwaga kikaa baada ya week1
Bajaji inafanya kazi siku6 ya saba unamuachia atafute pesa zake.

Isiyo ya mkataba kwa siku ni 20000 *6 =120000 kwa week kwa mwezi ni 480000 na kwa miezi kumi ni 4800000 bajaji isiposumbua, wala dereva asipokusumbua kwa visingizio vya misiba, ugonjwa.
,
Huu uzoefu ni wa mkoa gani mkuu? I mean upo mkoa gani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kuna mwalimu mwenzetu nae kanunua bajaji huwa anaendesha jioni tu akitoka shule ....inamlipa sana hakika hutojuta kufanya biashara hii!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwenyewe nataka za kupiga Kikuyu Dom mjini kuna mwalimu mmoja namfahamu pia anafundisha wela Sekondari ana bajaji pia huwa namuona nayo akipiga kazi jioni.
 
Na kuna mwalimu mwenzetu nae kanunua bajaji huwa anaendesha jioni tu akitoka shule, namlipa sana hakika hutojuta kufanya biashara hii.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mi naomba unifanyie tafiti juu ya biashara ya kirikuu (suzuki carry truck) kwa Dodoma kwa siku wanalaza bei gani..?? Na je kuna wateja wengi hapa nataka kufahamu ushindani wa kibiashara.
 
Nipo Dodoma na nimefikiria sana hii biashara ya suzuki carry....kwa siku hesabu ya bosi wengi wanapeleka 20k.

Nadhani kuanzia mwezi wa sita hiiv nitaingia kwenye biashara hii kama dereva ili niweze kufanikisha mishe zangu zingine
Mi naomba unifanyie tafiti juu ya biashara ya kirikuu (suzuki carry truck) kwa Dodoma kwa siku wanalaza bei gani? Na je, kuna wateja wengi hapa nataka kufahamu ushindani wa kibiashara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwaupande wangu kuliko Bajaji 1 tuchukulie mpya, ya milioni 7.2 bora ukanunua pikipiki aina ya Boxer 3, kwa milioni 6 na laki 6. Zitakulipa zaidi hasa kama unazitoa kwa mkataba.
Mimi mwenyewe mkuu kila nikiwaza kutoa 7.2m kwa ajili ya Bajaj akili inakataa kabisa.
Ni afadhali ninunue pikipiki nyingi najua ikitokea bahati mbaya moja imepata ajali zingine zinaendelea kupiga mzigo.
 
Mimi mwenyewe mkuu kila nikiwaza kutoa 7.2m kwa ajili ya Bajaj akili inakataa kabisa.
Ni afadhali ninunue pikipiki nyingi najua ikitokea bahati mbaya moja imepata ajali zingine zinaendelea kupiga mzigo.
Kuna kuibiwa/kutapeliwa pia.

Ushauri wangu, kama ndyo una anza biashara achana na biashara za mitaji mikubwa. Wekeza kwenye biashara za kawaida zisizo zidi mtaji wa 1 Mill ndipo ujiimarishe taratibu. Lkn c kwa mkupuo ununue pkpk zote hizo au bajaji, kaka utalia aisee na kujuta pia.
 
Kuna kuibiwa/kutapeliwa pia.
Ushauri wangu, kama ndyo una anza biashara achana na biashara za mitaji mikubwa. Wekeza kwenye biashara za kawaida zisizo zidi mtaji wa 1 Mill ndipo ujiimarishe taratibu. Lkn c kwa mkupuo ununue pkpk zote hizo au bajaji, kaka utalia aisee na kujuta pia.
Sasa kwa mtaji wa milioni moja utafanya biashara gani mkuu? Maana yake milioni moja ukilipia kodi ya fremu jumlisha kodi ya TRA utabakiwa na kitu hapo kweli?
 
Back
Top Bottom