Biashara ya uwakala wa simu na benki (M-Pesa, Airtel Money, Tigo Pesa, fahari huduma na NMB Wakala) unaweza kuanza kwa mtaji wa shilingi ngapi?

Duh, hii kwangu ni mwiko...biashara hii ni haramu kwa mujibu wa imani yangu ya kiislamu mkuu, ila shukrani..huwenda ukawasaidia wengine wasiokuwa mimi.

Kama lipo chaka jengine tujuzane boss!
Poa poa mkuu
 
TAHADHARI!.

. Kwa namna yeyote usitoe simu ya miamala kwa mteja. Chana makaratasi, mteja akuandikie namba, jina pamoja na kiasi cha pesa anachokiweka. Usimruhusu ashike simu kwa namna YEYOTE.

. Usipokee simu kupitia simu za miamala. Namba special za kampuni zinajulikana. Pokea endapo tu ni namba 100 au +255100. Usipokee kabisa. Ukienda kusajili till ya M-PESA, opt kusajili line nyingine mpya ambaye mtu yeyote haifahamu.

. Usisave namba yeyote kwenye simu ya miamala. Hata namba yako. Wasiliana na wafanyakazi wako au ndugu kupitia simu zingine za kawaida.

. Usimruhusu mteja atolee fedha akiwa mbali. Mteja atatoa fedha alafu ukishampa pesa, anapiga simu huduma kwa wateja kuomba kurudishiwa muamala alioukosea. Wakiangalia ulipo na alipotolea mteja, wanarudisha fedha kwa sababu si ruhusa kutolea fedha mbali.

. Kuwa na connection na watu wanaofanya kazi VODACOM au mitandao husika. Hii itakusaidia kwenye miamala iliyokosewa. Utaratibu ni kuwa, muamala uliokosea utarudishwa pale tu endapo hela itakuwa kamili. Ikipungua hata Tsh 50, haiwezi kurudishwa. Hivyo, mtu huyo atakusaidia kuangalia kwenye system kiasi hicho kilichopungua, ingia hasara uijazilishie kama itakusaidia kurudisha sehemu kubwa. Bora hasara ndogo kuliko kubwa.

. Funga biashara mapema kama ulinzi wako ni wa kusua sua. Wateja ni wengi usiku (mjini) ila risky ni kubwa sana.
Kuwa makini sana na wateja wa usiku. Mara nyingine kataa kuhudumia wateja wenye hela nyingi usiku. Commission ya 5,000 ni ndogo sana kusababisha kuibiwa fedha nyingi. Mwingine atakuuliza nataka kutoa million saba, napata? Sema sina. Maana hata ukimuambia ndiyo anakuambia nakuja. Mzee unapangiwa njama.

.Kama cash ni nyingi, ziondoshe mapema kabla ya kufunga. Kazihifadhi, alafu utarudi baadae kufunga. Wajuba wakikukamata kuna cha kubaki nacho.

. Hela zinatafutwa ndugu. Using'ang'anie. Waachie hela wakuachie roho.
 
Ufafanuzi mzuri Sana nimeupenda, kinacho nisikitisha Ni kua huu ufafanuzi unasaidia kukuepusha kupoteza pesa kwa 90% ila zile kumi zilizo naki lazima tu ki vyovyote hasara uipate. Mpaka mda huu nipo ofisini kwangu hapa natoa hii huduma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
@Tate Mkuu mweshimiwa Soma hii thread itakusaidia:

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamfano leseni halimashauri za kawaida huanzia shingapi?
 
TANGAZO

Kwa wahitaji wa laini za uwakala zenye majina yao natengengeza hizo kwa muda muchache inakamilika ndani ya masaa 24.

Laini zinatengenezwa ni kama zifuatazo:

NB malipo ni baada ya kazi[emoji736][emoji736]
Upo wapii?
 
Hi biashara bure kabisa, wastage of resources!! yaani una invest 20mil commission ukijumlisha haizidi 500K (uzoefu wangu), watu wakiona movement za wateja in and out wanafikiri unatengeneza faida kumbe ukweli unaujua mwenyewe. Lakini ukipata location nzuri unaweza piga pesa
 
Eleza ilikuaje????
 
Boss mtaji 20M upate commission ya sh 500k? Kuna tatzo mahali au huenda ndo kwnz umeingia kwenye game. Hyo 500k ilitakiwa ipatikane ktk line mojawapo ya unazofanyia dukan. Kwangu line zinazofanya vbaya ukitoa t-pesa ni halopesa na airtel money, ila nikijumlisha commission ya halopesa +airtel money =500k. Na hapo mtaji wangu haujafika hata nusu ya huo mtaji. Imagine nina uwakala wa crdb, nmb, tpb, nbc, equity, akiba +maendeleo Bank. Narudia mtaji wangu haujafka hata nusu ya 20M.
 
Mkuu naomba msaada wa kujua commision za nmb na crdb zimekaaje
 
Mkuu naomba msaada wa kujua commision za nmb na crdb zimekaaje
Hazina tofauti sana na za simu japo za benki ziko chini kidogo. Uzuri wa benki wateja wengi wanatoa na kuweka hela ambayo inakupa commission nzuri. Maana yangu ni kwmb unaweza kupata wateja wengi wa benki wa kutuma na kutoa average nzuri kuliko simu
 
Hazina tofauti sana na za simu japo za benki ziko chini kidogo. Uzuri wa benki wateja wengi wanatoa na kuweka hela ambayo inakupa commission nzuri. Maana yangu ni kwmb unaweza kupata wateja wengi wa benki wa kutuma na kutoa average nzuri kuliko simu
Ahsante sana mkuu
 
Kila business Ina risk hamna business isiyo na risk Cha mcngi ni kupamban na kuwa jasiri pia hakunaga shortcut kwenye mafanikio
 
Kuwa makini....kama umeweka wafanyakazi au mfanyakazi wenzako wanakuwa na lain mbili zote za miamala moja ya kwako nyingine ya kwake,,,,wengine wanatumia lipa.
 
Nasikia lipa kwa tigo zinaenda kufungiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…