Biashara ya vyakula afrika kusini na south sudan.

SOUTH AFRICA wanahitaji alizeti,dagaa,mchele,viungo,karafuu etc

Wanahitaji alzeti Mbegu? Ila nijuavyo kuingiza kitu kinaitwa chakula South Africa kuna Process za kutosha, wale jamaa hawako tofauti na Nchi za Ulaya, unahitaji kibali kutoka kwenye Shirika lao la Viwango, so ni bora watuwajikite South Sudani, Africa kusini kuna Ugumu fulani hasa kwenye maswala ya Vyakula,
 
Kama uko tayari kusacrifice sehemu fulan ya maisha yako kwa ajili ya kusaka opportunities, basi unaweza kwenda na si vibaya. Nachosema ni kuwa kama wewe ni mtu ulie na familia hapa na unadhani utakuwa unakwenda na kurudi kama unavyoutoa mchele Mbeya na kuuleta Dar-es-salaam, ni vyema ukachukua muda kuchunguza hali ya kibiashara na kisiasa ya huko kabla ya kufanya maamuzi usiyoweza kuyareverse kwa sababu kuna taarifa pia kuwa Wasudan nao wanadhulumu sana ingawa kwa kweli bei ya mazao huko ni nzuri sana, hasa nafaka na mihogo mikavu a.k.a Makopa. Nasema haya kwa sababu nayafanyia kazi
 
Lakini inakuwaje Wakenya,Waganda na Waghana wenyewe wapo huko?

Kama uko tayari kusacrifice sehemu fulan ya maisha yako kwa ajili ya kusaka opportunities, basi unaweza kwenda na si vibaya. Nachosema ni kuwa kama wewe ni mtu ulie na familia hapa na unadhani utakuwa unakwenda na kurudi kama unavyoutoa mchele Mbeya na kuuleta Dar-es-salaam, ni vyema ukachukua muda kuchunguza hali ya kibiashara na kisiasa ya huko kabla ya kufanya maamuzi usiyoweza kuyareverse kwa sababu kuna taarifa pia kuwa Wasudan nao wanadhulumu sana ingawa kwa kweli bei ya mazao huko ni nzuri sana, hasa nafaka na mihogo mikavu a.k.a Makopa. Nasema haya kwa sababu nayafanyia kazi
 
Chipukizi,unalink yoyote South Africa ya Viungo?
Au kama unajamaa au unataarifa zozte tusaidiane ndugu yangu
 
unataka peleka biashara gani? nipe list yako ntakupa list ya posible buyers


Asante Chipukizi!

Kama una mtu/suppiler au kwa una connection yeyote tutashukuru kwa maelekezo tafadhari.
 
Mie ninae rafiki yangu pale Juba, alichonieleza ni kwamba fursa ipo kubwa sana kibiashara.
Hususan supply ya Mchele, Sembe, Vitunguu pamoja na Asali.

ingekuwa vizuri mkuu ungeeleza kwa kina juu ya supply sudan ungemuuliza huyo rafiki yako hizo fursa zinapatikana vipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…