Biashara ya YouTube na faida zake

BLOGER10

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2017
Posts
267
Reaction score
172
Habari,

Lengo la uzi huu ni kufahamu namna ya biashara ya youtube inavofanyika, maana tumeona kuna wimbi kubwa sana la channel za habari kwenye mtandao wa YouTube.

Binafsi sio mtaalamu ila naomba wale waliofanikiwa kupitia biashara hii ya kuuza maudhui YouTube watupe shuhuda zao, jinsi walivofanikiwa.

Karibuni.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapiga kimya kimya tu...Mbongo fursa ya hela kabisa akushirikishe!!!? Akikuita kwenye fursa wewe ndo fursa.
 
Wengi hapo hawajui mkuu, kuanzia huyo aliesema inalipa sana.
Kwa haraka mkuu ni biashara ambayo inahitaji kujituma sana ili ufikie mafanikio.Youtube malipo yao ni kidogo na inategemea idadi ya matangazo ambayo yameonekana au kutangazwa katika video yako.Kwa maana nyingine kwa mfano kama una views 1M na hakuna tangazo limetazamwa probably hautalipwa kabisa(huu ni mfano).
Pia kuna ka shughuli ka kufikia vigezo; subscribers 1000 na kuendelea pia masaa 4000 ya channel kutazamwa katika miezi 12 iliyopita.
USHAURI: Usitarajie pesa ya haraka, ila kama ukifanikiwa kuna malipo mazuri...na kuna mambo kama ya affiliate marketing unaweza kuyatangaza ukapata pesa nzuri.
 
Ukipata time tazama channel ya inaitwa PewDewPie...huyu kuna time alilipwa mamilioni ya dollar na youtube.Angalia ana video ngapi na subscribers wangapi, pia total views katika channel yake.Hii channel ina views zaidi ya 4000
 
Shukran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukipata time tazama channel ya inaitwa PewDewPie...huyu kuna time alilipwa mamilioni ya dollar na youtube.Angalia ana video ngapi na subscribers wangapi, pia total views katika channel yake.Hii channel ina views zaidi ya 4000
Shukran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…