Biashara zangu zimegeuzwa kuwa za ukoo

pesa haina undugu wala urafiki,biashara iwe ni biashara tuu,waambie wakitaka pesa waje kwako na atakaye toa pesa dukani yeye ndio ataifidia/atailipa.
 
Sawa tu mkuu ulitaka hizo hela uje uwanunulie majeneza ya 1.5m wakifa? Thamini furaha ya ndugu zako mda huu wangali hai.
Kama unabahati ya utajiri unayo tu mkuu!
we jamaa utakuwa huelewi,anachosema ndugu wanafilisi biashara sio hataki kuwasaidia,au uko kwenu mtaji ndio mnakula/mnagawa!?
 
Hapa ndio unapoona faida ya kuoa mwanamke mpambanaji?Ushaifanya ya familia kwanza kwa kumuweka mama yako, fungua nyingine iwe ya kwako na mtu yoyote asitie mguu kwa kigezo cha kutaka msaada labda kama wanakuja KUNUNUA bidhaa
 
Hongera kufungua biashara

Nafikiri hakuna kitu rahisi kama kudhibiti pesa kwenye biashara, hata nyumbani. Inaanza na wewe. Kama una tabia ya kutuma ndugu wakachukue pesa kwenye biashara zako acha.

Inabidi ujue matumizi yako kwa wiki/mwezi uwe unachukua mara moja kwa wiki/mwezi kulingana na ukubwa wa biashara yako, kama vile unajilipa mshahara. Uache kudokoa kidogo kidogo.

Usipende kukaribisha ndugu kwenye biashara. Kama kusalimu waje nyumbani. Mama nae umfungulie kibiashara kidogo azuge nacho,hiyo yako akae nayo mbali.
 
Hapa ndio unapoona faida ya kuoa mwanamke mpambanaji?Ushaifanya ya familia kwanza kwa kumuweka mama yako, fungua nyingine iwe ya kwako na mtu yoyote asitie mguu kwa kigezo cha kutaka msaada labda kama wanakuja KUNUNUA bidhaa
Sawa nitatafuta mwanamke mpambanaji nione
 
nani anasimamia hizo biashara?
utaratibu wa kutoa kwenye biashara pesa ukoje?
ikitokea utaratibu ulioupanga umekiukwa ni hatua gani za kuchukua?

naomba ujibu hayo.
Nakupa ushauri wa bure huu kijana, biashara/kampuni ambayo itafanikiwa na kudumu ni ile ambayo haitakua na muingiliana na matatizo yako au ya familia yako, wewe na biashara yako ni vitu viwili tofauti. Ukiweza kuweka mpaka wa biashara zako na matatizo yako binafsi basi lazima itafanikiwa vinginevyo subiri kufirisika tu. Ulishawahi Jiuliza kwa nini biashara/kampuni za watu wngi masikini hufirisika???
 
Tripp,


Piga marufuku mtu yoyote kwenda hapo kuchukua pesa, waambie wafanyakazi wako hamna kutoa pesa, atakayekaidi anafukuzwa / kusimamishwa kazi haraka sana. Simple.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…