Bibi Titi Mohamed Mwanamke Shujaa

Bibi Titi Mohamed Mwanamke Shujaa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
BIBI TITI MWANAMKE SHUJAA

Labda kama ingekuwa si Bibi Titi Mohamed nisingefahamiana na Mh. Mohamed Mchengerwa.

Mh. Mchengerwa ndiye muasisi wa Tamasha la Bibi Titi.

Labda kama isingekuwa Tamasha la Bibi Titi Mohamed nisingefahamiana na Mh. Mchengerwa na pengine wengi tusingefika Ikwiriri hadi leo.

Inahitaji kuona kwa macho yako mwenyewe Tamasha la Bibi Titi katika Uwanja wa Ujamaa ndiyo utaelewa ushawishi wa Bibi Titi kwa watu wa Rufiji.

Hili ni tamasha langu la tatu mimi kuhudhuria na kila tamasha linazidi lililotangulia.

Wakati wa Tamasha Ikwiriri yote inasimama.

Wafanyabiashara zote wanakuwa wamesimama wima kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora na wao wananufaika na ugeni unaoingia mjini.

Huu unakuwa wakati wa nema kubwa Ikwiriri na Rufiji yote.

Haijatokea kiongozi mpigania uhuru wa Tanganyika akaenziwa namna leo Bibi Titi anavyoenziwa Rufiji.

Hakika hii ni kumbukumbu ya pekee na inayomtendea haki kiongozi huyu mwanamke aliyeingiza katika TANU jeshi kubwa la wake kwa waume kwa namna yake ya hotuba zake za kuwahamasisha ujasiri Watanganyika wasimame katika umoja wao hadi Mwingereza arudi kwao.

Naam Mwingereza alirejea kwao kwa amani na salama.

Bibi Titi aliinufaisha TANU katika uhai wake.

Bibi Titi ameinufaisha pakubwa historia ya uhuru wa Tanganyika leo wakati hatunae tena duniani.

Historia ya Bibi Titi huwezi kuihadithia bila kueleza historia yenyewe kama ilivyokuwa TANU ilipoanza kudai uhuru wa Tanganyika.

Ukipenda unaweza ukarudi hadi mwaka wa 1950 wakati vijana wa wakati ule walipofanya mapinduzi ya kutoa katika uongozi kizazi cha Wajerumani na kuingiza kizazi kipya cha utawala wa Waingereza.

Bibi Titi ni sehemu ya viongozi vijana walioingia katika siasa za kudai uhuru wa Tanganyika kuanzia kipindi hicho.

Inastaajabisha kuwa aliyesimamia mabadiliko haya Schneider Abdillah Plantan hajatajwa popote katika historia ya uhuru ingawa yeye ndiye aliyewaleta katika TANU Bibi Titi Mohamed na shoga yake kipenzi Tatu bint Mzee.

Kabla yake ni huyu Schneider Plantan aliyewapigania Dr. Vedasto Kyaruzi na Abdulwahid Sykes kuingia katika uongozi wa TAA mwaka wa 1950 kuchukua nafasi ya uongozi wa Thomas Saudtz Plantan na Clement Mohamed Mtamila.

Kupitia maisha ya Bibi Titi ndipo inapopatikana historia ya kweli ya TANU na historia ya Julius Kambarage Nyerere.

Wangapi wanajua kuwa Bibi Titi alipanda jukwaani kuhutubia mkutano wa TANU Mnazi Mmoja sura ya Nyerere haijui inafananaje?

Huyu ndiye Bibi Titi ambae anaeanziwa Ikwiriri kila mwaka.


View: https://youtu.be/I6TFC3QIeWQ?si=ez3cHccJaMgzoEgV
 
Haijatokea kiongozi mpigania uhuru wa Tanganyika akaenziwa namna leo Bibi Titi anavyoenziwa Rufiji.
Mkuu Alamaa Mohamed Said , asante kwa hii.

Siku za usoni tuandae makala ya compare and contrast jinsi wapigania uhuru mbalimbali wanavyoenziwa, anyeongoza kwa kuenziwa vizuri ni Nyerere na Karume, lakini wengine wengi bado, ila naamini wapigania uhuru wote wameenziwa kwa majina ya mitaa.

Je bado wanaenziwa?, jee bado wanakumbukwa?, michango yao inathaminiwa?
Nguvu zao, machozi, jasho na damu zao zimeinufaisha Tanzania, je wananufaika?.

P
 
BIBI TITI MWANAMKE SHUJAA

Labda kama ingekuwa si Bibi Titi Mohamed nisingefahamiana na Mh. Mohamed Mchengerwa.

Mh. Mchengerwa ndiye muasisi wa Tamasha la Bibi Titi.

Labda kama isingekuwa Tamasha la Bibi Titi Mohamed nisingefahamiana na Mh. Mchengerwa na pengine wengi tusingefika Ikwiriri hadi leo.

Inahitaji kuona kwa macho yako mwenyewe Tamasha la Bibi Titi katika Uwanja wa Ujamaa ndiyo utaelewa ushawishi wa Bibi Titi kwa watu wa Rufiji.

Hili ni tamasha langu la tatu mimi kuhudhuria na kila tamasha linazidi lililotangulia.

Wakati wa Tamasha Ikwiriri yote inasimama.

Wafanyabiashara zote wanakuwa wamesimama wima kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora na wao wananufaika na ugeni unaoingia mjini.

Huu unakuwa wakati wa nema kubwa Ikwiriri na Rufiji yote.

Haijatokea kiongozi mpigania uhuru wa Tanganyika akaenziwa namna leo Bibi Titi anavyoenziwa Rufiji.

Hakika hii ni kumbukumbu ya pekee na inayomtendea haki kiongozi huyu mwanamke aliyeingiza katika TANU jeshi kubwa la wake kwa waume kwa namna yake ya hotuba zake za kuwahamasisha ujasiri Watanganyika wasimame katika umoja wao hadi Mwingereza arudi kwao.

Naam Mwingereza alirejea kwao kwa amani na salama.

Bibi Titi aliinufaisha TANU katika uhai wake.

Bibi Titi ameinufaisha pakubwa historia ya uhuru wa Tanganyika leo wakati hatunae tena duniani.

Historia ya Bibi Titi huwezi kuihadithia bila kueleza historia yenyewe kama ilivyokuwa TANU ilipoanza kudai uhuru wa Tanganyika.

Ukipenda unaweza ukarudi hadi mwaka wa 1950 wakati vijana wa wakati ule walipofanya mapinduzi ya kutoa katika uongozi kizazi cha Wajerumani na kuingiza kizazi kipya cha utawala wa Waingereza.

Bibi Titi ni sehemu ya viongozi vijana walioingia katika siasa za kudai uhuru wa Tanganyika kuanzia kipindi hicho.

Inastaajabisha kuwa aliyesimamia mabadiliko haya Schneider Abdillah Plantan hajatajwa popote katika historia ya uhuru ingawa yeye ndiye aliyewaleta katika TANU Bibi Titi Mohamed na shoga yake kipenzi Tatu bint Mzee.

Kabla yake ni huyu Schneider Plantan aliyewapigania Dr. Vedasto Kyaruzi na Abdulwahid Sykes kuingia katika uongozi wa TAA mwaka wa 1950 kuchukua nafasi ya uongozi wa Thomas Saudtz Plantan na Clement Mohamed Mtamila.

Kupitia maisha ya Bibi Titi ndipo inapopatikana historia ya kweli ya TANU na historia ya Julius Kambarage Nyerere.

Wangapi wanajua kuwa Bibi Titi alipanda jukwaani kuhutubia mkutano wa TANU Mnazi Mmoja sura ya Nyerere haijui inafananaje?

Huyu ndiye Bibi Titi ambae anaeanziwa Ikwiriri kila mwaka.


View: https://youtu.be/I6TFC3QIeWQ?si=ez3cHccJaMgzoEgV

WATANZANIA TUACHE UPUMBAVU HUYO BIBI TITI HANA USHUJAA WOWOTE NI MPUUZI TU KATI YA WANAWAKE WAPUUZI WA TZ
 
Mkuu Alamaa Mohamed Said , asante kwa hii.

Siku za usoni tuandae makala ya compare and contrast jinsi wapigania uhuru mbalimbali wanavyoenziwa, anyeongoza kwa kuenziwa vizuri ni Nyerere na Karume, lakini wengine wengi bado, ila naamini wapigania uhuru wote wameenziwa kwa majina ya mitaa.

Je bado wanaenziwa?, jee bado wanakumbukwa?, michango yao inathaminiwa?
Nguvu zao, machozi, jasho na damu zao zimeinufaisha Tanzania, je wananufaika?.

P
P
Pana tatizo kubwa katika historia za viongozi wetu baada ya historia za kweli kuandikwa.

Viongozi wetu wanatazamwa kwa jicho lingine kabisa.

Jiulize Bibi Titi katokea wapi hii leo kuenziwa kiasi hiki?

Hujajiuliza?

Hushangai leo Sheikh Takadir na wenzake wanasomewa khitma kurehemewa tena na BAKWATA?

Huoni kitu hapo?
 
images (5).jpeg
 
P
Pana tatizo kubwa katika historia za viongozi wetu
dawa ya tatizo ni kulitafutia ufumbuzi。
baada ya historia za kweli kuandikwa.
kwenye ukweli,uongo hujitenga
Viongozi wetu wanatazamwa kwa jicho lingine kabisa.
Mungu bariki
Jiulize Bibi Titi katokea wapi hii leo kuenziwa kiasi hiki?
Nimejiuliza sikupata jibu, ila Mtaa wa Al Haj Mnamdi Azikiwe ulibadilishwa jina na kuitwa Bibi Titi Mohammed siku nyingi tuu,
Hili la kufanyiwa hadi tamasha ndilo jipya,ukiondoa Nyerere Day na Karume Day ,sikuwahi kusikia tamasha la kiongozi mwingine yeyote, hivyo this could be ni individual personal initiatives za Mchengerwa for political capitalization。
Hujajiuliza?
Hushangai leo Sheikh Takadir na wenzake wanasomewa khitma kurehemewa tena na BAKWATA?
sishangai kwasababu sikuwahi kujua kuwa zamani hawakuwa wakisomewa hitma
Huoni kitu hapo?
Kitu ninachokiona ni series za political capitalizetion ya viongozi wa zamani,juzi kati alikuwa Sokoine,bado Simba wa vita, sijui kama kuna kitabu chochote cha Karume。

All and all, keep on the good work you are doing kuhifadhi historia ya kweli。
P
 
dawa ya tatizo ni kulitafutia ufumbuzi。

kwenye ukweli,uongo hujitenga

Mungu bariki

Nimejiuliza sikupata jibu, ila Mtaa wa Al Haj Mnamdi Azikiwe ulibadilishwa jina na kuitwa Bibi Titi Mohammed siku nyingi tuu,
Hili la kufanyiwa hadi tamasha ndilo jipya,ukiondoa Nyerere Day na Karume Day ,sikuwahi kusikia tamasha la kiongozi mwingine yeyote, hivyo this could be ni individual personal initiatives za Mchengerwa for political capitalization。

sishangai kwasababu sikuwahi kujua kuwa zamani hawakuwa wakisomewa hitma

Kitu ninachokiona ni series za political capitalizetion ya viongozi wa zamani,juzi kati alikuwa Sokoine,bado Simba wa vita, sijui kama kuna kitabu chochote cha Karume。

All and all, keep on the good work you are doing kuhifadhi historia ya kweli。
P
P
Kitabu cha Dr. Harith Ghassany, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," na cha Mohamed Said, " Maisha Nyakati za Abdul Sykes..." vimebadili mengi.
 
Lwiva,
Ikiwa Bibi Titi ni mpuuzi wengi sana tutakuwa pia wapuuzi:

View: https://www.facebook.com/reel/1039738977917777

Tatizo lenu waisiharamu hamna cha maana cha kujivunia kilichopo active hivyo mnatafuta hadi wapumbavu wa kale na kuwatukuza ...huo ndiyo ukweli pia mmepandikiza siasa za kinafiki na kishabiki ndani ya dini ...ndiyo maana mnatukuza watu wapumbavu kama huyo bibi titi ..bi kidude nk sasa hivi mtaanza kutukuza hadi machoko ya kiisiharamu ...upumbavu unaofanyika makanisani umekuja kwenu kwa kasi kubwa sana ni kama mnalaana...
NAKUHUSU WENGI SANA KUWA WAPUMBAVU NDIYO UKWELI ASILIMIA 99 YA WATANZANIA NI WAPUMBAVU WALIO TUKUKA....UPUMBAVU WENU MNAUTENDA HADI NDANI YA DINI ZENU MLIZO ZIBADILI NA KUUNDA MADHEHEBU SAWA SAWA NA UPUMBAVU WENU
 
Mchengerwa baada ya kuharibu uchaguzi, KAAMUA KUJIFICHA KWA BIBI TITI.
 
Back
Top Bottom