Manchester Ship Canal ndio chanzo cha uhasama kati ya jiji la Liverpool na Manchester.
Baada ya kujengwa wa huo mfereji meli ziliweza kupita moja kwa moja kutoka baharini hadi jiji la Manchester ambalo kijiografia lipo inland tofauti na Liverpool lililopo katika pwani ya Kaskazini Magharaibi.
Kitendo cha kujengwa mfereji huo kiliwakosesha ajira wakazi wengi wa Liverpool kutokana na kupungua kwa biashara na idadi ya meli zilizoleta malighafi na bidhaa jijini Liverpool kwakuwa sasa meli ziliweza kufika moja kwa moja Manchester bila kuitegemea Liverpool.
Hapo ndio chuki ilipoanzia baina ya majini haya mawili.