Pagan Amum
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 1,932
- 4,403
Yeye mbona hakufanya hayo. Na anakufa ni masikini anategemea laki 7 mshahara wa Efm... Kuongea ni rahisiNdo mana namkumbuka Bikira wa KISUKUMA Kwa hizi Jumbe zake.
RIP Bro [HASHTAG]#RIPSeth[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Repost[/HASHTAG] @bikira_wa_kisukuma .
Laki tano, Mshahara wa Ma-Teller wa Benki hapa mjini Laki Tano, Bei ya TECNO PHANTOM mpya kabisa kwa kujishaua Snapchat na Istagram
Laki Tano, Bajeti ya Mafuta ya SUBARU mwezi Mzima.
Laki Tano , Bajeti ya HEINEKEN 100 KWA wanywaji wa Pombe.HELA FLANI MBUZI TU ambayo wengi wanaona HAINA ISHU.
.
Lakini , Laki Tano hii ina uwezo wa kukodi shamba Ekari 13 pale Kiteto au Mpwapwa na ikakutengenezea Million 15 baada ya Miezi MITATU kwa kulima Matikiti maji. Laki Tano hii hii ina uwezo wa kununua SIMTANK la lita 5000 ( ndoo 250 za lita 20) ambal inaweza kutumika kusolve shida ya maji mtaani kwako kwa kuuza ndoo 1 Sh 500 na ukaingiza 125,000 kwa kila SIMTANK unalouza.
.
Laki tano hii hii inaweza kulima Ekari 2 za Maharage pale Simanjiro na baada ya Miezi Minne ukavuna si chini ya Million 3 ambazo zitaexpand kilimo chako MARA 6 zaidi ya Mwanzo na Kuexpand Kipato chako mara 6 zaidi ya Mkupuo wa kwanza!
Laki Tano hii ina uwezo wa kulima Matikiti Maji Ekari 2 na zikakupa si chini ya Milion 2 na nusu baada ya SIKU 90!.
.
SHIDA NI: Kila mtu anataka akae mjini AONEKANE SAMAKI SAMAKI, aonekane Muvi Mlimani City, Apige Snapchat akiwa 777
MDADA yupo radhi aishi mjini kwa kuuza mwili wake kuliko kwenda Ruaha Mbuyuni Kuinvest kulima Vitunguu... Ataonyesha saa ngapi CROP TOP yake Mpya kutoka YAHYA BOUTIQUE? Sistaduu alime vitunguu?? Hapana, bora atafute Danga la Laki 2 akalale nalo!!
Big Up kwa wadada wote wajanja WALIOINVEST KWENYE KILIMO,kila Jumamosi wakati wewe unaona sifa kwenda HIGH SPIRIT LOUNGE Wadada wenzako wako RUVU wamekodi mashamba wanalima mpunga, unashangaa Huyu mdada anafanya nini kumbe mwenzio analima.
KUDOS kwa wanaume wenzangu ambao wamegundua siri kwamba kuuza Sura hakulipi ma wameinvest Shamba, kila weekend wanapotea kwenda kusimamia nyanya na pilipili Bagamoyo.
Utaendelea kuwashangaa wenzio wanatajirika na kudhani kila mtu anauza UNGA hapa mjini, Kilimo ndio unga mpya... Unadhani @mkandamizaj amenuunua ile BMW X6 kwa Episode za ORIJINO COMEDY? Thubutu, nenda MBARALI umkute amejaa Matope.....Huu ujumbe aliuandika miaka kadhaa iliyopita..
[HASHTAG]#RIPBro[/HASHTAG] [HASHTAG]#PumzikaKwaAmani[/HASHTAG]
[HASHTAG]#YourArticlesWillRemain[/HASHTAG]
sent from posta
Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app