Bila CCM kutoka madarakani hatuwezi piga hatua ya maendeleo ya kuonekana

Bila CCM kutoka madarakani hatuwezi piga hatua ya maendeleo ya kuonekana

maganjwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2012
Posts
2,800
Reaction score
2,339
Habari wakuu.

Mimi nimetafakari sana kuhusu jinsi mambo yanavyokwenda hapa kwetu. Yaani unaweza kupata hasira hawa jamaa hatua waliyofikia ni mbaya sana.

Kwanza wamejua hawapendwi na uchaguzi bila kutumia nguvu ya dola hawashindi.

Pili wanawaza mambo ya kuwakomoa watu kuwalit uhuru awamu hii waliaanza na kuzuia bunge live, ikapitishwa sheria kali ya mitandao, kusikiliza simu za watu kuwatesa wanaowakosoa, watu kupotea bila maelezo na sasa kupandisha bei ya vifurushi na gharama utumiaji wa simu. Haya yote ni kwa faida ya nani au ukiangalia ni kwa maslahi ya nani? unashindwa kuelewa kwani haya yote.

Tatu ukija kwenye siasa wameharibu kabisa hakuna siasa safi badala yake wanawaza kusalia madarakani kwa gharama yoyote ile na kutengeneza vijana na kuwafundisha ugaidi na kuwaaminisha kuwa wapinzani eti siyo wazalendo. Uzalendo ndugu zangu siyo kuisifia serikali na viongozi wake hilo ni lazima ijulikane. Sasa vijana wao wamevalishwa makofia yenye nembo ya chama kama maaskari fulani na wanajiona nao maaskari kila kiongozi wa CCM utaona kuna kijana yuko nyuma yake. Hii ni ajabu sana na wameachwa kwa muda sasa.

Nne ukwapuaji wa fedha za umma kwa hawa jamaa ni jadi yao. Wanalindana hawawezi wajibishana kwa kuwa huo ndo jadi yao wamefikia hatua mbaya kwa sasa wanaamini hela inaweza kufanya kila kitu mtu wa ccm huwa hajiandai kwa hoja anajiandaa kwa hela na wameharibu nchi kuwaaminisha watu wakati wa uchaguzi watu wanasema huu ni wakati wetu kula. Utamaduni mbaya sana

Kuendelea chama hiki kutawala ni kuendelea kudidimiza taifa tangu uhuru mpaka leo tuna hali mbaya ni aibu sana umaskini unawaandama watu. Hakuna mpango wa poverty reduction

Ebu tujadiliane ila haya ni maoni yangu shida kubwa sana kwangu mimi ni hiki chama siku ikiondoka madarakani tunaweza pata direction mpya
 
Shida viongozi wa upinzani nao hawaeleweki ndio maana wananchi wanaona bora haohao CCM
uchaguzi wa wananchi unapigwa chini jeshi linaamua aliyechaguliwa anaachwa aliyeshindwa anachaguliwa
 
Kama marehemu alikuwa mzalendo wa kweli angebadili katiba hii ya sasa na kutumia katiba mpya ili azihirishe uzalendo wake mbele ya umma. Na Kama alikuwa msafi kweli kipengele cha kumshitaki rais akishatoka madarakani kingekuepo kama kawa.
Unajiita mzalendo hafu unakombatia takataka.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama marehemu alikuwa mzalendo wa kweli angebadili katiba hii ya sasa na kutumia katiba mpya ili azihirishe uzalendo wake mbele ya umma. Na Kama alikuwa msafi kweli kipengele cha kumshitaki rais akishatoka madarakani kingekuepo kama kawa.
Unajiita mzalendo hafu unakombatia takataka.


Sent using Jamii Forums mobile app
kile kipengele cha rais kutoshtakiwa inawapa kiburi sana na kufanya mambo ya hovyo

Pia kuna kingine iliyopo kwenye ccm kuwa mwanachama wa ccm ni lazima ajue chama kwanza siyo nchi hii ndo vipengele vya hatari
 
watu wana viapo kuwa chama kwanza mwizi analindwa kwa kuwa ni mwenzao sasa ndo nini
 
kile kipengele cha rais kutoshtakiwa inawapa kiburi sana na kufanya mambo ya hovyo

Pia kuna kingine iliyopo kwenye ccm kuwa mwanachama wa ccm ni lazima ajue chama kwanza siyo nchi hii ndo vipengele vya hatari
Mzalendo ameondoka lakini one day hukumu itamfata huko huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tukitaka kujua tunaelekea wapi,na kwa kasi gani,fanya tadhimini ya vipindi kuanzia 1995yr-2005,2005-2015yr,2015-2020yr.
 
watanzania wamefurahi kwa kuondoka yule mtu maana aliwafundisha watu wapinzani sio wazalendo
Ni ukweli usiopingika, mfano rahisi ni wakili msomi tundu lisu yule wa ubelgiji
 
Hii nchi ishakuwa ya kisengerema sana. Mawasiliano ya simu imekuwa Anasa siku hizi
Bila kutoka chama cha mboga mboga madarakani, wanyonge watatengenezwa wengi sana.
 
Wakati mwingine shida si kumuacha mke kwa madhaifu yake bali huyó mbadala wake yuko bora kiasi gani!???

CCM kuitoa madarakani si shida sana endapo wananchi tukiamua, lakini changamoto iliyopo ni hawa tunaodhani ndio mbadala wa CCM wana ubora kiasi gani..!!

CCM kuendelea kuwa madarakani unatokana na ulelemama walionao upinzani

Kwa upinzani huu tulionao nchini itachukua miaka dahali kuitoa CCM madarakani, isipokuwa tu labda itokee CCM isambaratike yenyewe
 
Ninahisi hii nchi cha muhimu inahitaji wazalendo tuu..

Watu wanaangalia maslai zaidi.

Waliopo upinzani ni binadamu kama waliopo chama tawala.
 
Back
Top Bottom