Pre GE2025 Bila kura za Kanda ya Ziwa, CCM inaweza kubaki madarakani?

Pre GE2025 Bila kura za Kanda ya Ziwa, CCM inaweza kubaki madarakani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Baada ya kifo cha Magufuli na Samia Suluhu Hassan kuanza kuachana na yule aliyemtengeneza, kumekuwa na juhudi za makusudi kwake na chama cha Mapinduzi kushikilia dola. Hata hivyo, wawili hawa wanajua kuwa bila ya kura za Kanda ya Ziwa, hakuna anayeweza kushika madaraka nchini.

Tokana na utendaji na ushawishi aliokuwa nao Magufuli, yeyote anayejitahidi kumweka kapuni ataishia mwenyewe. Kuepuka balaa hili, Samia alipinda katiba na kumteau Dotto Biteko kuwa naibu waziri mkuu cheo ambacho ni upotezaji wa fedha za umma mbali na kutokuwamo kwenye katiba.

Janja ya pili ni kumpa Stephen Wasira umakamu mwenyekiti wa CCM mbali na kuteua mawaziri kama Innocent Bashungwa na Stagomera Tax wanaotoka mikoa ya Mwanza na Kagera wakati Biteko anatoka Geita. Kwa vile mkoa wa Mara mmoja wa mikoa ya Kanda ya Ziwa haukuwa na waziri. Hivyo, wameamua kumpa umakamu mwenyekiti Wasira ili kuirubuni mikoa husika isiwapige kibuti.

Je hii janja itafanikiwa na kuiwezesha CCM kuendelea kushika dola mbali na uchakachuaji wa uchaguzi? Je hii janja itaepusha mgawanyiko ndani ya chama baada ya magwiji kama Makamba na Kinana kuonekana kujiweka mbali nayo?

Je janja hii itazima hasira za wale waliokuwa wakimuunga mkono Magufli walioutupwa nje ya ulaji?
Je bila Kanda ya Ziwa, ccm inaweza kuendelea kushikilia dola?

Je bila Kanda ya Ziwa, Samia anaweza kuwa rais tena baada ya kuupata kwa mkono wa Mungu?
Karibuni tujadili na kudadavua pamoja.
 
Samia ametengenezwa? Hata kama ametengenezwa aliyemtengeneza ni Kikwete na siyo Magufuli..... ACHA UKABILA KAMA FISI.
Nawe acha uongo na ujinga. Kwani alikuwa makamu wa Kikwete au Magufuli? Mbona Kikwete aliwahi kukiri kuwa alikuwa akitaka makamu awa mwanaume lakini Magufuli akatengeneza huyu anayewasumbua sasa kwa uroho wa madaraka hata kama hana uwezo wowote?
 
Samia ametengenezwa? Hata kama ametengenezwa aliyemtengeneza ni Kikwete na siyo Magufuli..... ACHA UKABILA KAMA FISI.
Mkuu ndio maana mnafeli mitihani kwa kutoelewa kilichoandikwa, wapi pameandikwa Magufuli ndie aliyemtengeneza huyo unayemsema? rudia tena kusoma ndio utajua aliyeandika anamaanisha mtu huyo uliyemuandika na sio Magu! Unakurupuka na mambo ya ukabila wakati hata andiko hujalielewa.
 
Hata hivyo, wawili hawa wanajua kuwa bila ya kura za Kanda ya Ziwa, hakuna anayeweza kushika madaraka nchini
Nani kakudanganya CCM inategemea kura? Hata bila kampeni au msipige kura usishangae tu kusikia Mama Samia kupata 90% hiyo mikoa ya kanda ya ziwa.

Kukiwa na tume huru ndio unaweza leta mjadala wa kura.
 
Mkuu kwani CCM wana wasiwasi gani wakati inawekwa madarakani na Tume ya Uchaguzi kwa usimamizi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama?
Yaani hata makabila yote yakimkataa Mama,akiamua kuchukua fomu ataendelea kukaa madarakani.
 
Baada ya kifo cha Magufuli na Samia Suluhu Hassan kuanza kuachana na yule aliyemtengeneza, kumekuwa na juhudi za makusudi kwake na chama cha Mapinduzi kushikilia dola. Hata hivyo, wawili hawa wanajua kuwa bila ya kura za Kanda ya Ziwa, hakuna anayeweza kushika madaraka nchini.

Tokana na utendaji na ushawishi aliokuwa nao Magufuli, yeyote anayejitahidi kumweka kapuni ataishia mwenyewe. Kuepuka balaa hili, Samia alipinda katiba na kumteau Dotto Biteko kuwa naibu waziri mkuu cheo ambacho ni upotezaji wa fedha za umma mbali na kutokuwamo kwenye katiba.

Janja ya pili ni kumpa Stephen Wasira umakamu mwenyekiti wa CCM mbali na kuteua mawaziri kama Innocent Bashungwa na Stagomera Tax wanaotoka mikoa ya Mwanza na Kagera wakati Biteko anatoka Geita. Kwa vile mkoa wa Mara mmoja wa mikoa ya Kanda ya Ziwa haukuwa na waziri. Hivyo, wameamua kumpa umakamu mwenyekiti Wasira ili kuirubuni mikoa husika isiwapige kibuti.

Je hii janja itafanikiwa na kuiwezesha CCM kuendelea kushika dola mbali na uchakachuaji wa uchaguzi? Je hii janja itaepusha mgawanyiko ndani ya chama baada ya magwiji kama Makamba na Kinana kuonekana kujiweka mbali nayo?

Je janja hii itazima hasira za wale waliokuwa wakimuunga mkono Magufli walioutupwa nje ya ulaji?
Je bila Kanda ya Ziwa, ccm inaweza kuendelea kushikilia dola?

Je bila Kanda ya Ziwa, Samia anaweza kuwa rais tena baada ya kuupata kwa mkono wa Mungu?
Karibuni tujadili na kudadavua pamoja.
Mwaka 2025 CCM itashinda kwa kishindo!
 
Bila kanda ya ziwa kivipi na wewe mwenyewe umeorodhesha wadau wa kanda ya ziwa waliomo katika mfumo?
Hoja yako ni ipi haswa? Unataka waongezwe? Au hao uliowataja hawafai wabadilishwe?
Nimemaliza na swali rahis, je hizi mbinu au mbuni, mbuno, mbunu kkkk zitafanikiwa?
 
Miaka ya 90 raisi Samia hata angegawa dhahabu kila nyumba kanda ya ziwa ilikuwa ni ngumu kuchukua nchi kwa kuwa watu wa eneo hili hawaamini katika uongozi wa mwanamke katika ngazi yeyote ile ya kimaamuzi. Ila kwa kizazi hiki cha watoto wa 2000 wasiojua mila na desturi, walio lele mama, wapenda mserereko, mama ana nafasi ya kuchaguliwa kwa kishindo.
 
Baada ya kifo cha Magufuli na Samia Suluhu Hassan kuanza kuachana na yule aliyemtengeneza, kumekuwa na juhudi za makusudi kwake na chama cha Mapinduzi kushikilia dola. Hata hivyo, wawili hawa wanajua kuwa bila ya kura za Kanda ya Ziwa, hakuna anayeweza kushika madaraka nchini.

Tokana na utendaji na ushawishi aliokuwa nao Magufuli, yeyote anayejitahidi kumweka kapuni ataishia mwenyewe. Kuepuka balaa hili, Samia alipinda katiba na kumteau Dotto Biteko kuwa naibu waziri mkuu cheo ambacho ni upotezaji wa fedha za umma mbali na kutokuwamo kwenye katiba.

Janja ya pili ni kumpa Stephen Wasira umakamu mwenyekiti wa CCM mbali na kuteua mawaziri kama Innocent Bashungwa na Stagomera Tax wanaotoka mikoa ya Mwanza na Kagera wakati Biteko anatoka Geita. Kwa vile mkoa wa Mara mmoja wa mikoa ya Kanda ya Ziwa haukuwa na waziri. Hivyo, wameamua kumpa umakamu mwenyekiti Wasira ili kuirubuni mikoa husika isiwapige kibuti.

Je hii janja itafanikiwa na kuiwezesha CCM kuendelea kushika dola mbali na uchakachuaji wa uchaguzi? Je hii janja itaepusha mgawanyiko ndani ya chama baada ya magwiji kama Makamba na Kinana kuonekana kujiweka mbali nayo?

Je janja hii itazima hasira za wale waliokuwa wakimuunga mkono Magufli walioutupwa nje ya ulaji?
Je bila Kanda ya Ziwa, ccm inaweza kuendelea kushikilia dola?

Je bila Kanda ya Ziwa, Samia anaweza kuwa rais tena baada ya kuupata kwa mkono wa Mungu?
Karibuni tujadili na kudadavua pamoja.
Acha ujinga CCM hawategemei kura kushindwa chaguzi mbona JPM licha ya kuwa anatokea Kanda ya ziwa alishindwa na lowasa?
 
Miaka ya 90 raisi Samia hata angegawa dhahabu kila nyumba kanda ya ziwa ilikuwa ni ngumu kuchukua nchi kwa kuwa watu wa eneo hili hawaamini katika uongozi wa mwanamke katika ngazi yeyote ile ya kimaamuzi. Ila kwa kizazi hiki cha watoto wa 2000 wasiojua mila na desturi, walio lele mama, wapenda mserereko, mama ana nafasi ya kuchaguliwa kwa kishindo.
CCM hawaitambui kura yako
 
Biteko ana influence gani nje ya jimbo lake. Nani alimjua Biteko kanda ya ziwa, Shibuda alikuwa anajulikana kanda ya ziwa kushinda Biteko.

Shibuda alipokatwa CCM aliweza kulitetea jimbo lake nje ya CCM. Mwambie Biteko atoke nje ya CCM uone kama ana ushawishi wa kutetea jimbo lake nje ya CCM.

Hao watu hawana impact yeyote ndani ya CCM na watanzania wala hawana ubaguzi kwenye kura za taifa.

Magufuli hakuwa anapendwa kanda ya ziwa tu, bali Tanzania nzima.

Mengine ni kujijaza ujinga tu, kanda ya ziwa kama mikoa mingine aihitaji baraża la mawaziri lililojaa wasukuma kufanya maamuzi.

Kwanza ni kuwadharau wasukuma na kuwapa label ya ukabila ambayo haipo huko.

Ujakutana na wasukuma waliokuwa serikalini enzi za Magufuli (hawataki, hata kumsikia).

Mafisadi hayana dini, wala ukabila; na wananchi hawana dini wala ukabila kwenye maamuzi yao zaidi ya imani tu na mtu wakuwatatulia shida zao.

Mengine ni ujinga mtupu mnaojijaza vichwani kwenu tofauti na fikra za watanzania.
 
Back
Top Bottom