Bila kutenda HAKI ni ndoto kudumisha AMANI nchini, iwe ndiyo "slogan" ya Taifa kuanzia sasa

Bila kutenda HAKI ni ndoto kudumisha AMANI nchini, iwe ndiyo "slogan" ya Taifa kuanzia sasa

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tokea Mwenyekiti wa Chadema, shujaa Freeman Mbowe, atoke jela, siku chache zilzopita, alikokuwa amekaa zaidi ya miezi 8 kwa Kesi ya michongo ya ugaidi, amekuwa alisisitiza Sana neno HAKI kuwa likidumishwa nchini, Taifa letu litapona.

Hata kwenye maandiko matakatifu ya Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 imenenwa "Haki huinua Taifa" mwisho wa kunukuu.

Hivi inakuwaje Katika nchi yetu, tuwaachie Polisi watende mambo wanavyotaka wao, halafu wasichukuliwe hatua yoyote??

Tumejionea Katika Kesi ya "michongo" ya ugaidi iliyofunguliwa mahakamani namna Polisi wetu walivyothibitika bila shaka yoyote, namna wanavyoweza kumbambikia mtu Kesi kubwa, kama hii ya ugaidi, pasipo kuwajibishwa.

Tumejionea namna mhimili wetu wa Mahakama, ambao ndiyo tunaoutegemea utende HAKI nchini, namna ulivyokuwa "umemezwa" na mhimili mwingine wa Serikali na kutoa maamuzi yaliyoacha maswali mengi nchini na nje ya nchi.

Hivi inakuwaje viongozi wetu wakuu wa dini waendelee kutuhimiza wananchi tuendelee kudumisha AMANI nchini, huku hawakemei watawala wetu wakishirikiana na Polisi wakiendelea kutotenda HAKI kwa wananchi wao?

Tulijionea namna uchaguzi mkuu ulivyoendeshwa nchini, bila kufuata misingi ya HAKI, huku wasimamizi wa kura, wakiwatimua mawakala wa vyama vya upinzani nchini, huku zoezi hilo likisimamiwa kikamilifu na Polisi wetu!

Kuanzia hivi sasa iwe ni wajibu wa kila mzalendo nchini, apaze sauti kubwa kadri awezavyo kila siku, kuhimiza itendwe HAKI nchini Ili tudumishe AMANI nchini.

Kwa kuwa AMANI ni tunda la HAKI
 
Tuna polisi wa hovyo sn
Yaani hata bila kuambiwa, ni LAZIMA kwa hivi sasa, Rais Rais Samia afanye uamuzi mgumu, alifumue Jeshi lote la Polisi na amtimue Kazi IGP Sirro, ambaye aliutangazia Ulimwengu kuwa sisi wananchi tunaomuona Mbowe ni malaika, tuisubiri Mahakama itakapothibitisha ugaidi wake!

Kiko wapi sasa, mbona DPP wenu, ameamua "kuichomoa" Kesi hiyo mahakamani, kabla hatujathibitishiwa pasipo shaka yoyote kuwa Mbowe ni gaidi??
 
Haki ianzie ndani ya Chadema kwenye uchaguzi mwenyekiti taifa
Wewe kada peleka propaganda zako mtaa wa Lumumba, ukapate posho yako ya huku 7 itakayokukimu wewe na familia yako😁
 
Yaani hata bila kuambiwa, ni LAZIMA kuwa hivi sasa, Rais alifumue Jeshi la Polisi na kumtimua IGP Sirro, ambaye aliutangazia Ulimwengu kuwa sisi wananchi tunaomuona Mbowe ni malaika, tuisubiri Mahakama itakapothibitisha ugaidi wake!

Kiko wapi sasa, mbona DPP wenu, ameamua "kuichomoa" Kesi hiyo mahakamani, kabla hatujathibitisjiwa pasipo shaka yoyote kuwa Mbowe ni gaidi??
Mzee Sirro atakuwa amefoji umri atakuwa hata na miaka 78 huko maana uwezo wake wa kufikiri umeisha kabisa
 
Mzee Sirro atakuwa amefoji umri atakuwa hata na miaka 78 huko maana uwezo wake wa kufikiri umeisha kabisa
Hahaaaaa.......😁😅

Hebu imagine mbunge Tundu Lissu amemiminiwa risasi zaidi ya 16 mfululizo, mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi wakuu wa Serikali, zaidi ya miaka minne iliyopita, hajakamata hata mshukiwa mmoja wa kumuhoji!🙄
 
Hahaaaaa.......[emoji16][emoji28]

Hebu imagine mbunge Tundu Lissu amemiminiwa risasi zaidi ya 16 mfululizo, mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi wakuu wa Serikali, zaidi ya miaka minne iliyopita, hajakamata hata mshukiwa mmoja wa kumuhoji![emoji849]
Dah!
inasikitisha kwakweli
 
Haki ianzie ndani ya Chadema kwenye uchaguzi mwenyekiti taifa
Acha zako wewe mbona uchaguzi unafanyika ila wanachama wote wanapitisha ndugu FAM kwakuwa anafaa na anauwezo mkubwa kuendesha chama..wewe kinakuuma nini..kama wanachama wamekubaliana naye awe mwenyekiti wao mpaka atakapo choka yeye.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na lile limwenge likakae makumbusho ya taifa, halina tija zaidi ya kuturoga na kutupumbaza.

Hata miradi inayozinduliwa na mwenge huwa haidumu, hufa baada ya muda mfupi
 
Acha zako wewe mbona uchaguzi unafanyika ila wanachama wote wanapitisha ndugu FAM kwakuwa anafaa na anauwezo mkubwa kuendesha chama..wewe kinakuuma nini..kama wanachama wamekubaliana naye awe mwenyekiti wao mpaka atakapo choka yeye.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizo ni propaganda za wanaccm tulizozizoea.

Mbona wanaojimikisha vyama vyao akina John Cheyo na UDP yake na Augustine Mrema wa TLP, hutaki kuwagusa??
 
Back
Top Bottom