Bila kuweka ushabiki, unadhani ni matukio gani yanayofanya "uhisi" kuwa hakuna utawala wa sheria?

Bila kuweka ushabiki, unadhani ni matukio gani yanayofanya "uhisi" kuwa hakuna utawala wa sheria?

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Hili la kudai kuwa Tanzania HAKUNA utawala wa sheria naona linazidi kusemwa kila siku. Sasa hebu tuweke hata kwa "hisia" Tu list ya matukio unaona yanathibitisha kukosekana kwa utawala wa sheria Huko Tanzania. Naanza na mfano huu:

1. Kunyimwa dhamana kwa makosa yanayodhaminika.....rejea kesi ya kiongozi wa CHADEMA kule Tanga ambapo mahakama, POLISI na MAGEREZA wako kimya kwa SABABU za kipumbavu.

2. Tukio au matamshi ya kichochezi yanayosemwa na VIONGOZI wa CCM bila kuchukuliwa hatua na POLISI, mfano statements za Tulia Ackson, Yule Dogo wa UVCCM Bukoba, yule DC alikua kiongozi wa UVCCM aliyewahi kusema "this time hatutatumia risasi tutatumia sindano za sumu".

3. Kupotea kwa Watu hasa wenye mrengo wa upinzani bila Polisi na mahakama kufanya Jambo Lolote la maana. Rejea hukumu ya kipumbavu mno ya mahakama kwa CHADEMA na Polisi kuhusu utekwaji wa kijana Deusdedit Soka na wenzake.

4. Matukio tofauti ya Wabunge tena Ndani ya bunge ya kuendelea kuisifia Serikali na kushindwa kuhoji wala kusimamia Serikali na hivyo kujikuta nao kujifanya ni sehemu ya Serikali.

Kwangu Mimi, matukio haya ya haraka haraka yanathibitishia kuwa Tanzania HAKUNA utawala wa sheria.
 
Wastafu kutothaminiwa kwa kushusha kikokoto awamu ya 5 na awamu ya 6 kushindwa kurejesha kama ilivyokuwa awamu ya mtakatifu Mkapa na Kikwete
 
Mtu kuropoka tena hadharani kwamba watu fulani tukiwapoteza polisi msiwatafute, halafu mtu huyo anaachwa bila kuguswa.
 
Kuzuia mikutano ya siasa kwa vyama vya upinzani ilhali ni haki ya kikatiba.
 
Wabunge kumshukuru Rais Kwa kuwagawia pesa za maendeleo ya maeneo yao, wakati wao wenyewe wabunge wanajua kuwa ni Bunge lao pekee, kwa mujibu wa Katiba ya nchi ndilo linalopanga bajeti kuwa pesa zinagawiwa sawasawa Kwa mujibu zitakavyopitishwa.
 
Kutekwa na kuuwawa kikatili kwa Ally Mohammed Kibao itaishi milele na milele awamu ya 6 inasemekana imevuja damu nyingi na utekaji orodha ni kubwa sasa sijui wanaosema hayo ni kweli au uongo? Pengine mamlaka zitapaswa kulibeba kwa tathmini na je wataipa maanani?
 
Hili la kudai kuwa Tanzania HAKUNA utawala wa sheria naona linazidi kusemwa kila siku. Sasa hebu tuweke hata kwa "hisia" Tu list ya matukio unaona yanathibitisha kukosekana kwa utawala wa sheria Huko Tanzania. Naanza na mfano huu;
1. Kunyimwa dhamana kwa makosa yanayodhaminika.....rejea kesi ya kiongozi wa CHADEMA kule Tanga ambapo mahakama, POLISI na MAGEREZA wako kimya kwa SABABU za kipumbavu
2. Tukio au matamshi ya kichochezi yanayosemwa na VIONGOZI wa CCM bila kuchukuliwa hatua na POLISI, mfano statements za Tulia Ackson, Yule Dogo wa UVCCM Bukoba, yule DC alikua kiongozi wa UVCCM aliyewahi kusema "this time hatutatumia risasi tutatumia sindano za sumu"
3. Kupotea kwa Watu hasa wenye mrengo wa upinzani bila Polisi na mahakama kufanya Jambo Lolote la maana. Rejea hukumu ya kipumbavu mno ya mahakama kwa CHADEMA na Polisi kuhusu utekwaji WA kijana Deusdedit Soka na wenzake.......
4. Matukio tofauti ya Wabunge tena Ndani ya bunge ya kuendelea kuisifia Serikali na kushindwa kuhoji wala kusimamia Serikali na hivyo kujikuta nao kujifanya ni sehemu ya Serikali.

Kwangu Mimi, matukio haya ya haraka haraka yanathibitishia kuwa Tanzania HAKUNA utawala wa sheria.
 
Silaha kama hizi ni kwa ajili ya nchi zilizoko vitani... Tungekuwa na utawala wa sheria haya yasingefanyika
20240927_021824.jpg
 
Awamu ya sita imeondoa plea bargain tuu (Yale mambo ya kuchungulia salio na kukimbilia mahakamani kusema flani halipi kodi)
Lakini mengine yote ni hovyo sana ..
Unawezaje kumshikilia mtu kituoni kwa miezi mitatu (Mbwana Kombo) wa Tanga tena hutaki kumpeleka Mahakamani ?
 
Kubinafisisha Ngorongoro

Kubinafisisha bandari

Kubinafisisha tanesco

Kukopa kupita kiasi na pesa zinazokopwa kupigwa na wajanja.

Kujenga mahekaru ya mabilioni ya dollar kizimkazi

Utekaji, wizi wa Mali za umma, chaguzi za hovyo

Kuyachekea majizi

Udini katika idara nyeti Kama TISS na Ikulu.

e.t.c.........
 
Kubinafisisha Ngorongoro

Kubinafisisha bandari

Kubinafisisha tanesco

Kukopa kupita kiasi na pesa zinazokopwa kupigwa na wajanja.

Kujenga mahekaru ya mabilioni ya dollar kizimkazi

Utekaji, wizi wa Mali za umma, chaguzi za hovyo

Kuyachekea majizi

Udini katika idara nyeti Kama TISS na Ikulu.

e.t.c.........
Mbona unayaorodhesha as if hayupo tena madarakani? Au una uhakika hayataongezeka kabla hajamaliza mihula/muhula wake?
 
Kubinafisisha Ngorongoro

Kubinafisisha bandari

Kubinafisisha tanesco

Kukopa kupita kiasi na pesa zinazokopwa kupigwa na wajanja.

Kujenga mahekaru ya mabilioni ya dollar kizimkazi

Utekaji, wizi wa Mali za umma, chaguzi za hovyo

Kuyachekea majizi

Udini katika idara nyeti Kama TISS na Ikulu.

e.t.c.........
Ndo naamka kuna nini na WA mwisho kulala jana alifunga mlango?
 
Kichwa cha habari kingesomeka mambo atakayokumbukwa nayo awamu ya kwanza maana bado tu tuna imani nae kwa awamu nyingine ya pili
 
Ni hisia tu Kama ulivyoiweka hapo.
Hisia zio nzuri
Utafiti ni muhimu kuliko hisia
 
Back
Top Bottom