Bila Mshikamano wa Kitaifa, Tanzania tuitakayo itakuwa ndoto kuiona

Bila Mshikamano wa Kitaifa, Tanzania tuitakayo itakuwa ndoto kuiona

Kwa matukio haya yanayoendelea kuripotiwa kwenye vyombo mbali mbali vya habari na mitandao mbali mbali ya kijamii ndani ya taifa letu ni kweli hatuko salama kabisa, mshikamano na umoja wa kitaifa haaupo tena. Imefikia hata sasa kila Mwananchi ukimsiliza anaongea kwa hofu na uoga mkubwa. Matumaini ya watu kuishi ndani ya taifa lao hayupo tuna.

Majeshi yetu ya ulinzi na usalama yatakua na kazi kubwa sana kupambana na matukio mbali mbali ya kutisha bila kikomo kama hatutapata kiungo muhimu wa kuwaunganisha watanzania kuishi kwa hofu ya mungu na upendo, tunatakiwa kusikia maneno yenye kutia moyo kulingana na hali halisi ilivyo. Tunatakiwa kuunganishwa kwa kuambiwa ukweli wa mambo pale yanapotokea matukio ya wazi yenye kututenganisha watanzania.


Yameanza matukio ya kutoweka kwa watu na ni zaidi ya miaka miwili sasa hawajulikani walipo, wanatekwa watu na kupotezwa kusikojulikana, mauaji ya kutisha kule wilayani Rufiji-Kibiti mkoani Pwani, Kuvamiwa kwa vituo vya redio na runinga, kuvamiwa kwa ofisi za mawakili na bado zinaendelea kuvamiwa, kupigwa Risasi kwa wanasiasa mfano wa Tundu Lissu juzi tu. Ni vipi kwa matukio haya tunaweza kusema kua taifa liko salama, tutasemaje kua mshikamano wetu upo?

Tusifikiri kuishi kwa mshikamano, amani na utulivu ni kazi ya vyombo vya ulinzi na usalama tuu, laahasha! Yanatakiwa kuzungumzwa maneno mazito yenye kuiondosha hofu iliyotanda kwenye nyoyo za watu. This is not a physical phenomenon, it needs a spiritual approach. Haya mambo ni wazi kua sheitwani anatembea na nyoyo za watu, hofu ya ukubwa wa Mungu haipo tena.


Madhara ya matukio kama haya hua ni makubwa sana, yanaweza kulibomoa taifa kwa muda mfupi sana. Kuanza kuishi kama maadui hakutaweza kulifikisha taifa letu mahali zaidi ya kurudi nyuma. Itatuchukua miongo mingi sana kuja kuwaweka pamoja watu walioishi kama maadui endapo jitihada na tahadhari za makusudi hazitachukuliwa hivi sasa.


Watakaolipasua taifa letu ni wachache kwa kujawa na uovu lakini watakaoumia ni wengi, taifa lenye idadi zaidi ya watu million 50 ni taifa kubwa sana hasa kwa kuzingatia maeneo na mpaka yetu. Hii hofu ya Mungu inayokosekana kwa kasi miongoni mwetu sisi italipeleka kupabaya sana.

Kama ni dini au siasa, kama ni utajiri au ushirikina, ni mambo ambayo wanaohusika waambiwe kwa namna ambayo wataelewa. Ni vipi Mungu ataweka watu wake pamoja endapo hawa watu hawajapenyeshewa hofu ya ukubwa wake. Huwezi kumuondosha mwenzako kwenye mgongo wa ardhi huku ukijua huna life span hata ya miaka 30 kwenye hii dunia? Ni nani mwenye mkataba wa Maisha yake na Mwenyezi Mungu?

Viongozi wa kisiasa na kiimani mnalo jukumu kubwa la kuliunganisha taifa hili, chochote kibaya kitakachotokea kwenye mgongo wa ardhi ambayo mmepewa mamlaka ya kukemea mtaulizwa. Hakikika hamtauepuka moto wa jehanam ikiwa mnakosa aina ya maneno ya kulinganisha taifa badala ya nisubiri shurti.
 
TL kidogo kidogo anaturudisha kwenye umoja wetu!
 
Kweli huo mshikamano wa kitaifa utapatikana kwa uandishi wa makala ndfu kiasi hiki? Ungeandika fupi ili watu wote wasome na kuelewa huo ndio mshkamano wa kitaifa.
 
Swali ,je tanzania tuna umoja mshikamano na amani?
Kwanini chama kikuu cha upinzani hawali chakula meza Moja na chama tawala? kwanini chama kikuu cha upinzani hawatembeleani hospital na chama tawala ccm,kwanini ccm na chadema hawazikani?
Je,kwa matendo kama haya ni kuimarika kwa mshikamano wa kitaifa?
Je,kwa matendo kama haya inawezekana tukakuwa kiuchumi kuliko nchi zote katika ukanda huu wa nchi za Africa ya mashariki na kati?
Je, matendo yanayotokea tanzania,kwa maoni yako yanawafurahisha kenya Uganda Rwanda,burundi Congo,au yanawachukiza?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali ,je tanzania tuna umoja mshikamano na amani?
Kwanini chama kikuu cha upinzani hawali chakula meza Moja na chama tawala? kwanini chama kikuu cha upinzani hawatembeleani hospital na chama tawala ccm,kwanini ccm na chadema hawazikani?
Je,kwa matendo kama haya ni kuimarika kwa mshikamano wa kitaifa?
Je,kwa matendo kama haya inawezekana tukakuwa kiuchumi kuliko nchi zote katika ukanda huu wa nchi za Africa ya mashariki na kati?
Je, matendo yanayotokea tanzania,kwa maoni yako yanawafurahisha kenya Uganda Rwanda,burundi Congo,au yanawachukiza?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wenye madaraka against wataka madaraka..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna jambo baya kama unafiki,uwe wa kikundi au mmoja mmoja,ndiyo maana wahenga walisema bora mchawi kuliko mnafiki.

Watanzania wamekuwa wahanga wa unafiki,wengine wakiutumia kama mtaji kwa ajili ya matumbo yao na wengine wakiathiriwa kwa namna moja au nyingine.

Tunaitwa Watanzania,ambao kwa umoja wetu tuliunganishwa makabila yetu,tukaongea lugha moja ya kiswahili,tukadumisha umoja na mshikamano,lakini leo tumegawanywa tena kwa misingi ya itikadi,tumemalizana kiitikadi tumehamia kwa wenye mawazo mbadala ndani ya itikadi moja..,ilimradi tu kulinda maslahi ya wachache walioshika mpini.

Tukikubali kugawanywa kwa mbinu ya waingereza(divide and rule),tumekwisha. Alipopigwa Lissu risasi watu walibeza na wengine kushangilia,alipotekwa Ben Rabiu halikadhalika,alipoumizwa Dr. Ulimboka hivyo hivyo,sasa kapotea Allan,tunaleta mzaha. Tunataka apotee nani,ndo tujue nchi haiko salama.

Umakini wa serikali kwenye jukumu la ulinzi uko wapi,au kuna siri ya matukio haya inayofanya akina Mambosasa kuwa watu wa kukanusha,huku wakitunukiwa nishani!!!

Leo Jeshi letu la polisi idara ya uchunguzi imepwaya kabisa,wanajibu majibu mepesi kwa maswali magumu,wengine makamanda wa mikoa wanafanya siasa wakiwa na nembo ya jeshi,na uniform za jeshi,ndo maana kinachojiri ni business as usual.

Rais kasema,Watanzania si wajinga nasi tunasema sisi wajinga,pamoja na kuwa si wajinga mbona hatuoni watu wakiwajibishwa kwa matukio yanayo hofisha watu. Kwanini tunaimba kilokole wakati huo huo tunacheza kishetani!!!

Tumeanza kuiona hali hii ya kawaida,tukizoea nchi haitatawalika,kwa kuwa tunapanda mbegu hatarishi ambayo ikimea tutakimbiana.

#Yapo makundi yanafurahia kuona wengine wanaumizwa kwa kuwa tu wanakosoa na kupinga maslahi ya wachache,yapo makundi yanayo furahia walio wachache wakikumbwa na kadhia ya kuwadhuru.

Lakini katika makundi hayo,yana tofautiana,kundi moja linalo tetea maslahi ya wachache likiguswa nguvu inayotumika kuwashughulikia washangiliaji walio wengi ni kubwa mno kuliko kundi linalo tetea maslahi ya wengi.

Kwa kigezo hicho hata ikulu yetu wanasema ni yao,kwa kuwa tu tumewanyamzia na kuruhusu Lumumba kuhamia pale.

Ikiwa katibu mkuu wa chama anaweza sema wasiwadanganye kwa kuwa hawana ikulu,hawana dola tutegemee nini kwa hali ya usalama wetu,kama si uchochezi na baraka kwa makundi yaliyo jipambanua kuwashughulikia wakosoaji wa serikali eti kwa kigezo cha kumlinda rais ni nini!!!

Mbona vyombo vyetu vya usalama viko kimya kwa makundi haya,ambayo yapo wazi yakiendelea kutishia usalama wa watu na huku matukio ya utekaji yakizidi kushamiri!!!!

Hamjui ukimya huu ni salamu kwa wananchi kujiandaa kisaikolojia kujilinda kwa njia wazijuwazo wao.

Kuna sehemu tuna kwama kama taifa,kwa hali kama hii lazima tutegemee wasomi wengi wa majalalani kwa kuwa hawana hoja walizo bakiza zaidi ya nguvu ya dola.

Tumekuwa tukijinadi kuwa tuna muenzi Mwalimu,tunafanya maandamano kama ya Tunduma tukibeba picha yake,lakini tumeshindwa kuishi falsafa yake,tuna tumia nguvu ya dola kuzuia mijadala,mikutano ya wazi ilihali sisi tunafanya.

Mwalimu aliamini katika nguvu ya umma,ndiyo maana wakati tunasoma siasa mashuleni tulitumia falsafa yake ya vijana nguvu ya chama. Mwalimu kwa kulijua hilo Alisisitiza falsafa yake kwa kusema" tunataka vijana wajeuri,wenye nguvu ya kuhoji na kutetea maslahi ya umma bila kujali nguvu ya wenye mamlaka" leo tujiulize vijana hao wapo,au ndo wamegeuka wanyonge wanabebwa na mbeleko ya dola huku wakigeuzwa kama chapati.

Mwalimu alisisitiza kuwa ukikubali kuambiwa jambo la kipumbafu ukalikubali,aliyekuambia atakudharau,lakini ukilikataa atakuheshimu. Vijana wamepotea, walioshangilia Lissu kupigwa risasi,wanaweza kugeuza kibao na kuwa na majonzi iwapo yule wanayemtegemea naye ataonyesha hisia za uchungu kwa maumivu ya Lissu,na hii ndiyo Tanzania mpya.

Turudi kwenye umoja wetu ili kulinda mshikamano wa kitaifa,huu utamaduni mpya wa kutiana hofu,kutekana,kuoneana ni ukaburu kama ukaburu mwingine. Tukemee,tuomboleze sote kwa kuwa hakuna msiba usio na mwenyewe.

Serikali ijue kuwa mamlaka na madaraka yake inayapata kwa mujibu wa katiba toka kwa wananchi,wananchi ndiyo sisi,ninyi,na hata wale waliotekwa. Na serikali inapaswa kujuwa kuwa msingi mkuu wake ni ustawi kwa taifa na watu wake,wenye taifa wakihujumiwa haki yao ya kuishi na kutiwa hofu, mamlaka na madaraka waliyo nayo leo kesho watayapata wapi.

Tuheshimiane kama taifa kulinda umoja wetu,mgawanyiko wa matabaka hautotufikisha popote,tupingane kwa hoja bila kupigana.

#bringbackAllanbringbackBenWasanane#
 
Tuna safari ndefu sana,lakini mbio za farasi huishia ukingoni
 
Tanzania ni nchi ya Amani ila imejaa uchungu

Kumbuka tuu kwamba "Critical Thinking' siyo rahisi kama unavyodhani, ndiyo maana inafanywa na watu wachache. Watu wengi sometimes wana argue kwa feelings and emotions kitu ambacho kinatoa maana halisi ya critical thinking.

Muda wa kutibu majeraha sasa. Tusiendelee kuona ni kitu cha kawaida. watu kufurahi 'kifo' ni kitu kipya sana kwa watanzania. RAIS ana wajibu wa kutuongoza katika hili, RECONCILIATION. Kuwekana magereza, kutekana, kupigana risasi na wahusika hawakamatwi ni matokeo ya chuki hizi.

TUJIULIZE, kwanini Taifa letu limefika hapa? Kwanini tunashangilia matatizo ya wengine? Lissu apigwe risasi, CCM wafurahie, Saanane, Mdude watekwe tuelezwe "wamejiteka hao" wengine washangilie taarifa za ugonjwa wa mwanaCCM, kwanini? TURUDI KWENYE MISINGI! TUJISAHIHISHE!
 
Umeongea kizalendo sana.Mungu akubariki.ila ajisahihishe Sasa,hope majibu anayo.
 
Wametangaza ubaya wanastahili walipwe ubaya

Mamlaka zimewekwa na Mungu anatokea mwanasiasa moja anachuki na Rais anamuombea kifo!
 
Chadema sio wa kuonewa huruma hata kidogo! Ni wa kukanyagwa kwelikweli, wajinga sana!
 
Wametangaza ubaya wanastahili walipwe ubaya

Mamlaka zimewekwa na Mungu anatokea mwanasiasa moja anachuki na Rais anamuombea kifo!
Kama ungeusikia wimbo uliowakaribisha watu ikulu leo. Nafikiri Maghufuli lazima ageuke nyuma aangalie tulipokosea kama taifa. Najua wasaidizi wake watamuweka sawa kuongoza taifa kwa utu na kwa watu wote.
 
Tabia ya watu kushangilia matatizo ya wengine haijaanza leo, haipo Tanzania tu na haipo katika ngazi ya kitaifa, watu hushangilia wengine wakifeli shule, wengine wakifukuzwa kazi, wengine wakishindwa biashara, wengine ndoa za watu zikivunjika kwa kifupi watu hushangilia mabaya ya wengine kama njia yao ya kujipoza na maumivu yanayowasibu, wengi wao huamini mabaya hayo ni kama malipizi kwa ubaya wao jambo ambalo si kweli, unashangilia KIFO kwani nani hatokufa? nani kaja kukaa hapa duniani Milele? AKIFA wewe utanufaikaje na KIFO chake? Matatizo yako yataisha? Asipokufa utaendelea kununa na kusononeka kuishi katika matatizo yako? Mabaya kwa mtu mwengine hayawezi kuwa chanzo cha mafanikio au furaha yako. Furaha au Mafanikio, huzuni au kushindwa ni wewe ndo mwenye jukumu la kuvitengeneza hivi katika maisha yako na sio mtu mwengine
 
Chadema sio wa kuonewa huruma hata kidogo! Ni wa kukanyagwa kwelikweli, wajinga sana!
Mawazo kama yako ndiyo yalioleta chuki kwa wananchi. Cdm wapo kikatiba after all, walipata all most nusu ya kura za WaTz utawapuuzaJe ?!.
 
Tanzania ni nchi ya Amani ila imejaa uchungu

Kumbuka tuu kwamba "Critical Thinking' siyo rahisi kama unavyodhani, ndiyo maana inafanywa na watu wachache. Watu wengi sometimes wana argue kwa feelings and emotions kitu ambacho kinatoa maana halisi ya critical thinking.

Muda wa kutibu majeraha sasa. Tusiendelee kuona ni kitu cha kawaida. watu kufurahi 'kifo' ni kitu kipya sana kwa watanzania. RAIS ana wajibu wa kutuongoza katika hili, RECONCILIATION. Kuwekana magereza, kutekana, kupigana risasi na wahusika hawakamatwi ni matokeo ya chuki hizi.

TUJIULIZE, kwanini Taifa letu limefika hapa? Kwanini tunashangilia matatizo ya wengine? Lissu apigwe risasi, CCM wafurahie, Saanane, Mdude watekwe tuelezwe "wamejiteka hao" wengine washangilie taarifa za ugonjwa wa mwanaCCM, kwanini? TURUDI KWENYE MISINGI! TUJISAHIHISHE!
Wenye macho na waone.Asante Kigogo japo kama mzaha vike, ila huenda likaponya taifa kuwa na umoja na ustawi.
 
Toka week iliyopita na hali iliyokuwa ikiindelea juu ya ugonjwa wa rais wa Tanzania na kukatishwa kwa ziara ya kusini kwa siri na kupelekwa aliko pelekwa imefumua mambo mengi yaliyokuwa yakisemwa au kukemewa kuwa kuna viashiria vya mpasuko wa nchi na kweli vimeonekana.

1. Ile kauli kuwa kipenzi cha watu mara wanyonge mie nimekiona hakipo kabisa kuanzia zoezi la uandikishaji wapiga kura. Kwa sababu kama unapendwa bila shaka wangejitokeza watu wengi kuja kukuunga mkono ila zoezi limegubikwa na upikaji wa idadi ya wapiga kura na nguvu kubwa hadi watoto wa shule wametumika kujaza na kujaza majina hewa kwenye daftari.

2. Mara baada ya uvumi wa ugonjwa ni idadi kubwa waliopenda kusikia yamemkuta na hatukusikia idadi hata hiyo ndogo sio mashehe wala maaskofu wala gamboshi wakitoka kumwombea. Wala waanachama wake wa ccm hawakutokea zaidi ya kundi kubwa kutoka na kuomba iwe kweli. Hapa ni wazi hapendwi na amelijua hilo kuwa hapendwi.

3. Kama taifa limegawanyika wale wanaojiita wazalendo hasa ccm waokila kinachofanywa na rais ni sawa hata kama hakina maslai kwa taifa na kuwa na maslai ya kichama ni sawa. Atakayepinga huyo ni adaui wa taifa na sio ccm ndio wamejengwa ivyo kwa sasa. Tujiulize ule ushindani wa hoja umekufa sasa umebaki ishindani wa kidola na kuitana wahaini na wasaliti baada ya hoja kuisha.

4. Ni kweli hatupendani kama taifa. Tunafurahi hata kiongozi wa nchi akipatwa na matatizo achilia mbali viongozi wa upinzani ndio huwa sherehe kubwa. Ikija kutokea kiongozi wa upinzani jeuri hili taifa litapotea kwenye sura ya dunia. Kwa sababu serikali imejenga chuki baina ya chama chake na upinzani na wanasahau hao wapinzani wana ndugu familia na marafiki kuwa ni watu pia. Na wanawafuasi.
5. Tanzania haina umoja kabisaaa
 
Back
Top Bottom