Bila uchunguzi wa kisayansi tutafunga kuku: 1998 dereva wa lori alikufa

Bila uchunguzi wa kisayansi tutafunga kuku: 1998 dereva wa lori alikufa

Mkwawa

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2011
Posts
1,334
Reaction score
1,466
Katika tukio la ugaidi la mwaka 1998 ambapo kulitokea kitendo cha kulipuliwa kwa ubalozi wa Marekani Tanzania, magaidi walitumia watu wengi sana bila kujijua, Dereva aliyepeleka bomu alijua kabeba maji, aliyetengeneza lile tank yaani karakana ya Thomas Lyimo alijua anatengeneza tank la maji. Waliopokea wageni walifikiri wanapokea wageni wema. Kumbe kuna kazi maalumu.

Arusha tumepatwa na simanzi, mshtuko na maafa makubwa. Polisi, usalama wataifa, Jeshi la wananchi naomba tufanye kazi kwa ujuzi, weledi, miiko sio kutoa majibu kwa shinikizo la wanasiasa na kutesa watanzania wasio na hatia na kuwafungulia kesi zisizo wahusu. Jifunzeni kwa wenzenu jinsi wanavyoendesha upepelezi, hii ni taaluma haihitaji akili za akina Mulongo au mwana siasa awe yote, huhitaji akili za Pinda, Nchimbi ili kubaini wahalifu, hawa tayari wanayao kichwani. KURA.

Msifanye uchunguzi kwa shinikizo, ili kutoa majibu ya kubalance story, iiteni beleshi beleshi, mtathaminika sana ndani na nje ya jamii.

Ndugu wanausalama haiingii akilini kwanini manataja jina moja au mawili kati ya watuhumiwa kumi mlionao, kama mnaona kazi ya upepelezi bado mnaharaka ya kwenda wapi?? Raisi kasema eti mmekamata kwa kushuku tu, Mawaziri wanasema mmekamata kumi ila majina ni mawili ambayo yako hadharani. Hao nane wanakinga gani??

Kumbukeni mnavyozidi kucheza siasa ndio mnakimbiza ushahidi. Hili linatufanya tuamini mnaendeleza uchunguzi kama wa Marehemu Mwangosi, ambapo pamoja na kwamba kila jicho alishuhudia lakini danadana mpaka leo. Ulimboka alitekwa na watu wanaojulikana mkatulitea jina la kikenya ambalo uwezekano hakuna mtu mliyemkamata ni mkubwa sana. Kibanda katolewa jicho, meno, Mkaanza na kumtupia lawama Lakwatare ikawashinda mpaka sasa mnarukaruka kama samaki. Padri kauwawa mmekosa jibu , kapigwa risasi mmeshindwa kwa sababu ya siasa kuingizwa kazini.

Sheikh kachomwa kisu mkamalizia kwa kusema eti ni wezi wa mahindi, sheikh kamwagiwa Tindikali mpaka leo hatujui kwanini. Haya yote yanazidisha hasir akwa wananchi na kukosa kabisa imani na vyombo vyetu vya usalama.

Leo mnakamata waendesha bodaboda, halafu bila maelezo ya kujitosheleza mnataka kutuaminisha ndio waliopanga na kukamilisha ulipuaji wa kanisa la Olasik, kwa sababu gani, dereva wa bodaboda aliwapata wapi bomu? Ana hasira ya nini na balozi wa Vatican kwanza inawezekana hata alikuwa hajui kama kuna balozi anakuja, na hii si kwasababu ya majina yao hata angekuwa na jina gani, siamini dereva wa bodaboda anaweza kupata bomu sokoni na kulirusha kanisani kwa manufaa gani?? Hakuna Mtanzania masikini raia wa kawaida awe mkristu, muislamu au dini yeyote mwenye chuki ya kuuwa wenzeka. Wengi wenye chuki hizi ni wale wenye uwezo, madaraka, wasomi, na wenye uchu wa madaraka yawe ya dini, siasa, biashara nk.

Bomu la Arusha ni zaidi na dereva wa bodaboda, naomba wapepelezi wetu rudini kwenye drawing board, msione haya kuomba msaada. Acheni kabisa kudeal na wanasiasa wao wanatafuta KURA na huruma kwa matukio ya kuuwawa sisi. Ndivyo wanavyofanya, watafanya tayari wanafanya.

Updates
Kabla ya Mei 5, mwaka huu, jina la Victor Ambrose (20), halikuwa likijulikana miongoni mwa jamii kubwa ya wakazi wa Jiji la Arusha. Hali kadhalika, kwa Watanzania wengi.
Lakini baada ya tarehe hiyo, jina lake lilianza kujulikana nchi nzima na pengine kimataifa kwa kuhusishwa na tukio la kigaidi la mlipuko wa bomu katika Kanisa Katoliki la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti jijini Arusha.
Parokia hii mpya awali ilikuwa ni kigango cha Parokia ya Burca, ambako ndiko pia yapo makazi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha, Josephat Lebulu, na uzinduzi uliotarajiwa kufanyika Jumapili iliyopita, ilikuwa ni kukipandisha hadhi kigango hicho kuwa parokia kamili.

Hali ilianza kwa shamrashamra, waumini wengi walionekana kuwa na nyuso za furaha, ghafla shamrashamra zao zilizimwa muda mfupi baadaye kabla ya uzinduzi wenyewe na hali ya simanzi ikatawala.
Tukio la mlipuko wa bomu kanisani hapo lilitokea siku ya kuzindua jengo la kanisa hilo, uzinduzi ambao ulikuwa umepangwa kufanywa na Balozi wa Vatican nchini, ambaye ni mwakilishi wa Baba Mtakatifu, Askofu Mkuu Fransisco Padilla, akishirikiana na mwenyeji wake, Askofu Mkuu Lebulu.
Hata hivyo, uzinduzi huo ulikatishwa kwa tukio la mlipuko wa bomu hilo ambao hadi sasa umesababisha vifo vya watu wanne na zaidi ya 66 kujeruhiwa.

Ilikuwa ni asubuhi muda ambao mvua zilikuwa zikinyesha, baadhi ya waumini wakipika chakula kwa ajili ya mlo wa mchana, huku ibada ikiwa ndiyo kwanza imeanza kwa Balozi Padilla, kupiga ishara ya msalaba na kubariki maji.
Umati mkubwa wa waumini kutoka parokia mbalimbali mkoani hapa, unaokadiriwa kufikia zaidi ya watu 2,000 hivi, ulikuwa umejitokeza kuhudhiria uzinduzi wa parokia hiyo.
Baada ya kubariki maji hayo, Askofu Mkuu Padilla, alitaka kunyunyiza maeneo mbalimbali na huku akiwa ameshika kifaa cha kunyunyizia, ghafla mtu mmoja ambaye bado hajakamatwa akiwa nyuma ya watu na nje ya uzio, alirusha kitu kinachoelezwa kuwa bomu kwenye mkusanyiko huo. Haijafahamika mlengwa alikuwa nani, lakini mtazamo wa wengi hauweki shaka kwamba mlengwa Askofu Mkuu Padilla.

VICTOR AMBROCE NI NANI?

Huyu ni dereva wa pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda, kazi ambayo aliianza tangu aliposhindwa kuendelea na masomo yake ya sekondari mwaka 2011 akiwa amefikia kidato cha pili.
Alimaliza elimu ya msingi katika Shule ya Terrat, mwaka 2009, na akaendelea na masomo ya sekondari katika Shule ya Oljoro, zote za mkoani Arusha.
Victor, anaelezwa na bibi yake, Lucia Victor, kuwa katika familia yao walizaliwa watoto wawili, yeye akiwa ni mtoto wa pili kwa wazazi wake ambao wote wawili walishatangulia mbele ya haki. Kaka yake anaitwa Philip.
Bibi Lucia, anasema tangu kufariki dunia kwa wazazi wake, amekuwa akiwalea watoto hao mpaka hapo walipofikia, na kwamba wanaishi eneo la Kwa Mromboo kama linavyotamkwa na wakazi wa Jiji la Arusha.
"Wazazi wa Victor wote walifariki dunia, na mimi ndiye nimekuwa mlezi wao tangu wakiwa watoto wadogo," anasema Bibi Lucia.

Bibi Lucia anasema familia yao pamoja na mjukuu wake, ni Wakristu wa madhehebu ya Katoliki. Anasema wanasali kwenye kigango cha Kwa Mromboo, cha Parokia ya Sombetini. Anamwelezea mjukuu wake kwamba hajawahi kumuona akinywa pombe, kuvuta sigara au kutafuna mirungi.

SIMULIZI KUTOKA KIJIWE CHA BODABODA:

"Tunamfahamu Victor, na hapa ndiyo kijiweni kwake," anaeleza dereva mmoja wa bodaboda. Hata hivyo, dereva huyo alikuwa na wasiwasi mkubwa hata kule kusema tu kwamba hapo ndipo palikuwa ni kijiwe chake, lakini mara kwa mara alikuwa akitaka kujua ni nani anayeongea naye.
Na baada ya kuelewana naye alianza kunielekeza eneo analoishi ingawa alisema hajui nyumba yake ni ipi isipokuwa eneo.

Dereva huyo alikuwa msaada kwangu kwani baadaye alinipa namba ya Mwenyekiti wake wa Jumuiya ndongo ndogo za Kikristo za Kanisa Katoliki na bila kusita nikampigia na kumweleza shida yangu.
Mwenyekiti huyo alikuwa mbali na eneo hilo kwa shughuli za ujenzi na akasema asingeweza kuwahi kwa muda huo, lakini alinielekeza na kufuata ramani hiyo niliweza kuifuata hadi nyumbani kwa Victor, kama vile unaelekea Oljoro.
Baadhi ya wenzake katika kijiwe hicho wanasema kuwa Jumapili Victor alikodiwa na mtu asiyemfahamu ampeleke kanisani na alikubali. Lakini baaada ya kufika, mkodishaji aliteremke na kukimbia bila kumlipa na kwamba wakati anamfuatilia amlipe fedha zake, ghafla ulitokea mlipuko.
Wanasimulia kuwa baada ya mlipuko huo hakumuona aliyemkodi zaidi ya kujikuta akiwa amevamiwa na watu waliokuwa karibu na eneo la kanisa hilo wakimgang'ania kuwa ndiye aliyefika eneo hilo na mlipuaji.

HALI ILIVYO NYUMBANI KWAKE

Majirani wachache na wote akina mama ndiyo waliokuwapo hapo. Ilikuwa nyakati za jioni na walikuwa wenye nyuso za wasiwasi.
Hali hiyo ilinifanya nianze kwa kuwapa pole na kuwafariji kwa yote yaliyotokea nao wakanikaribisha ndani na kuanza mazungumzo huku sauti ya nyimbo za kwaya ikisikika kwenye redio yao, baadhi yao walikuwa wakipika kuandaa chakula cha jioni.
Baadhi ya majirani walisema walipokea kwa mshangao tukio la kukamatwa kwa Victor kwa maelezo kwamba hakuwa wamesikia kama ana matatizo yoyote.
PAROKIANI ST. JOSEPH
Paroko wa Parokia ya Burca, Padri Peddy Castelino, ambaye kigango cha St. Joseph kipo kwenye parokia yake, anasema licha ya kutokea kwa tukio hilo, bado shughuli za misa zinaendelea kama kawaida asubuhi.
Wakatoliki wana kawaida kuadhimisha Misa Takatifu kila siku, maadhimisho ambayo Padri Peddy anasema wanayafanya kwa waumini wa kanisa hilo la St. Joseph.
Mazingira katika eneo hilo la kanisa yapo vile vile, huku walinzi wachache wa kanisa wakilinda viti na vifaa vingine vilivyotumika kwa siku ya uzinduzi. Meza, viti na vitu vingine vimeachwa hapo hapo na pia viatu vya watu vilivyovulika wakati wa purukushani navyo ni vimeachwa hivyo hivyo.
Hakuna ulinzi wa askari waliovaa sare au wale waliovaa kiraia huku wakiwa wameshika bunduki, lakini kwa mbali na eneo hilo kulikuwa na gari la polisi aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili PT 0591, hali inayoashiria kuwa ulinzi upo katika eneo hilo.
Akielezea mahusiano na majirani zao, Padri Peddy, anasema hawana ugomvi wowote na majirani zao tangu waliponunua uwanja huo hadi kukamilika kwa ujenzi.
"Hatuna ugomvi wo wote na majirani zetu, tunaishi nao vizuri tu," alisema
 
CCM bwana, wanaingiza siasa hata sehemu zinazohitaji utaalam na wataalam walio bobea.
Hivi Pinda alienda kufanya nini Arusha?
 
Haya majibu ya polisi wa bongo hayana tofauti yule form four aliyemchora mess!
 
CCM bwana, wanaingiza siasa hata sehemu zinazohitaji utaalam na wataalam walio bobea.
Hivi Pinda alienda kufanya nini Arusha?

alienda kuwaambia modokta. Kuwa kila kipande cha chuma wanachokitoa ktk mwili wa majerui wakipeleke kwa magesa mulongo kwa ajiri ya upelelezi
 
Mkwawa umesema... Ni wakati wa tiss, na vyombo vingine kuonyesha 'kazi' iliyotukuka. Ikibidi watoke hadharani na kujulisha wananchi kuwa uchunguzi unaendelea na kama utachukua muda, wawe wakweli maana usalama wa nchi umechezewa tayari...
 
Mkwawa umenena. Nilishajiuliza humu haraka ya kutaja lile jina moja ilikuwa ya nini? Siku zote polisi wetu hawana haraka kabisa ya kutaja majina ya watuhumiwa, wakati mwingine mpaka wanapowafikisha mahakamani, sababu ikiwa wakitaja watavuruga upelelezi. Kwa hili hsraka ilikuwa ya nini, kama siyo kuscore matakwa ya kunfi fulani? Wapelelezi wenye weledi katika tukio kama hili cha kwanza kufanya baada ya kuwasaidia mahanga/waathirika ni kuhifadhi sehemu ya tukio na kuhakikisha vitu vyote vilivyopo hapo havichafuliwi. Hapa kwetu hiki hakifanyiki, wakifika wstu hapa na hasa viongozi, wakiwemo viongozi wa polisi wote ni wajuzi. Watagusa kila kitu na kujidai kutoa maelexo ambayo mengine hata hayana maana. Nilishangaa jana kumsikia Waxiri Mkuu akiagiza madakitari kuhakikisha chembechembe za vyuma vinavyotolewa kwenye miili ya waathirika viifadhiwe vizuri kwa uchunguzi! Hii haihitaji Waziri Mkuu kuagiza adharani, wapelelezi wanapaswa kufanya kazi na madaktari siyo tu kupata vyuma hivyo hata aina ya majeraha.Jana wakati Bunge linapitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani nilishangaa sana wabunge kupinga hoja ya kuliunda upya. Nani wakiwemo hao wabunge hawajui muunfo wa polisi ulivyokuwa compromised na kuwafanya wasifanye kazi yao kwa weledi na ufanidi? Nani hajui jinsi polisi wanavyobambnikizia watu kesi za ajabu? Taarifa ya habari ya ITV saa mbili leo inaonyesha kiundfi cha polisdi kinambambikizia mtu kesi ya mfanyabiashara kukutwa na kichwa cha mtu (walichokiweka wao) huko Morogoro - na hii pengine ni kutaka kuwaonyesha hao wabunge hali halisi!Tusiingize siasa kwenye vyombo vyetu vya usalama polisi, TISS na JW.
 
CCM bwana, wanaingiza siasa hata sehemu zinazohitaji utaalam na wataalam walio bobea.
Hivi Pinda alienda kufanya nini Arusha?

Haa haa haa. Mkuu nimecheka sana! Nilisoma kwenye gazeti eti Pinda amawaagiza madaktari wasiitupe ile misumari wanayotoa kwenye miili ya majeruhi kwani itatumika baadae kwenye uchunguzi! Sisemi kuwa alitoa wazo baya ila nataka kuonyesha jinsi wapelelezi wa Tanzania wanavyoendeshwa na wanasiasa! Kwani wao walikuwa hawajui mpaka Pinda awaongoze namna ya kufanya upelelezi? Hata kama alikuwa usalama wa taifa lakini hii inaonyesha jinsi hapa kwetu mambo yanavyokorogwa na wanasiasa!
 
nchi si salama tena kila mwananchi ajitafutie mbinu yake ya kupambana na uhalifu kama tunavyopambana na umasikini.
Serikali imeshindwa kutuondolea umaskini,maradhi na ujinga na sasa imeshindwa hata kutulinda.zimebaki show za walinzi wa kiongozi mkuu wa nchi,madoido ya intercoms,suti nyeusi,mawani za jua na sukuma sukuma za hapa na pale huku madereva wa boda boda wakiachiwa kurusha mabomu kanisani.
Watanzania wanatamani mtoto azaliwe bila kucha kumuepusha na misukosuko ya makoleo ya kungo'lea kucha.
 
CCM bwana, wanaingiza siasa hata sehemu zinazohitaji utaalam na wataalam walio bobea.
Hivi Pinda alienda kufanya nini Arusha?

Si hoja yeye kufika pale mapema, ila hoja ni alichoongea kina mashiko?, kimepelekea adui kuogopa?, unakumbuka kauli ya bush pale ground zero dunia nzima ilijua america wamechukia na wanakuja sasa..
 
Mkwawa umenena. Nilishajiuliza humu haraka ya kutaja lile jina moja ilikuwa ya nini? Siku zote polisi wetu hawana haraka kabisa ya kutaja majina ya watuhumiwa, wakati mwingine mpaka wanapowafikisha mahakamani, sababu ikiwa wakitaja watavuruga upelelezi. Kwa hili hsraka ilikuwa ya nini, kama siyo kuscore matakwa ya kunfi fulani? Wapelelezi wenye weledi katika tukio kama hili cha kwanza kufanya baada ya kuwasaidia mahanga/waathirika ni kuhifadhi sehemu ya tukio na kuhakikisha vitu vyote vilivyopo hapo havichafuliwi. Hapa kwetu hiki hakifanyiki, wakifika wstu hapa na hasa viongozi, wakiwemo viongozi wa polisi wote ni wajuzi. Watagusa kila kitu na kujidai kutoa maelexo ambayo mengine hata hayana maana. Nilishangaa jana kumsikia Waxiri Mkuu akiagiza madakitari kuhakikisha chembechembe za vyuma vinavyotolewa kwenye miili ya waathirika viifadhiwe vizuri kwa uchunguzi! Hii haihitaji Waziri Mkuu kuagiza adharani, wapelelezi wanapaswa kufanya kazi na madaktari siyo tu kupata vyuma hivyo hata aina ya majeraha.Jana wakati Bunge linapitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani nilishangaa sana wabunge kupinga hoja ya kuliunda upya. Nani wakiwemo hao wabunge hawajui muunfo wa polisi ulivyokuwa compromised na kuwafanya wasifanye kazi yao kwa weledi na ufanidi? Nani hajui jinsi polisi wanavyobambnikizia watu kesi za ajabu? Taarifa ya habari ya ITV saa mbili leo inaonyesha kiundfi cha polisdi kinambambikizia mtu kesi ya mfanyabiashara kukutwa na kichwa cha mtu (walichokiweka wao) huko Morogoro - na hii pengine ni kutaka kuwaonyesha hao wabunge hali halisi!Tusiingize siasa kwenye vyombo vyetu vya usalama polisi, TISS na JW.
Nadhani wanataka kuonesha siuo suala la udini bali ni ugaidi. Okay. Mbona hayo mengine hayatajwi? Kwani huyo aliyekamatwa hajasema alikopata bomu? Vinginevyo wanyamaze hadi wakamate watu wote. Halafu hayo majina ni kama fake kwa kuwwa kataika hali ya kawaida jina moja lilitakiwa liwe la ukoo lakini hayo majina yote ni ya kistaarabu. Walau lingekuwapo moja la kishenzi.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Sijui viongozi wetu wanadhani wanaongoza watoto jamani!! Sijui tunaonekana hatuna ufaahamu? Sijui kwasababu tunaonekana hatuwezi ku react?

Wakiambiwa akili ndogo inaongoza akili kubwa wanadai wametusiwa. Kwa hili sijui wanawaza nini mpaka saivi kututajia jina moja uku wengine wakifaamika kama wasaudia!!! Na hivi wamerahisishiwa kwa kuambiwa haliusiani na udini tutasikia mengi yakushangaza zaidi ya hili.

Mmmh Tanzania yangu!!! ???.....
 
Haa haa haa. Mkuu nimecheka sana! Nilisoma kwenye gazeti eti Pinda amawaagiza madaktari wasiitupe ile misumari wanayotoa kwenye miili ya majeruhi kwani itatumika baadae kwenye uchunguzi! Sisemi kuwa alitoa wazo baya ila nataka kuonyesha jinsi wapelelezi wa Tanzania wanavyoendeshwa na wanasiasa! Kwani wao walikuwa hawajui mpaka Pinda awaongoze namna ya kufanya upelelezi? Hata kama alikuwa usalama wa taifa lakini hii inaonyesha jinsi hapa kwetu mambo yanavyokorogwa na wanasiasa!

Shangaa tu nawewe unisaidie cse nilibaki mdomo wazi kwa muda niliposikia . Sijui hawa viongozi wakiwaonaga waandishi wa habari wanachanganyikiwa?
 
Nadhani wanataka kuonesha siuo suala la udini bali ni ugaidi. Okay. Mbona hayo mengine hayatajwi? Kwani huyo aliyekamatwa hajasema alikopata bomu? Vinginevyo wanyamaze hadi wakamate watu wote. Halafu hayo majina ni kama fake kwa kuwwa kataika hali ya kawaida jina moja lilitakiwa liwe la ukoo lakini hayo majina yote ni ya kistaarabu. Walau lingekuwapo moja la kishenzi.Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Hilo ndilo tatizo. Haraka haikuhitajika. Kwanza unataka kuonyesha kuwa siyo udini ili iweje? Kwani kulikuwa na vurugu za kulaximisha watu wajue kuwa aliyetupa bomu ana jina la Kikiristu? Sasa tuseme tu inakuja kuonekana kuwa huyu mtu alilipwa na mwenye jina la kiislamu kufanya hivi je hii itaonyesha kuwa ni udini? Weledi ulikosekana hapa. Tunatarajia bado kwamba polidi watatupa majibu ya kuondoa kiu yetu kwa sababu wamesha tuangusha huko nyuma katika matukio ambayo yana hisia kwa wananchi.
 
Mkwawa umenena. Nilishajiuliza humu haraka ya kutaja lile jina moja ilikuwa ya nini? Siku zote polisi wetu hawana haraka kabisa ya kutaja majina ya watuhumiwa, wakati mwingine mpaka wanapowafikisha mahakamani, sababu ikiwa wakitaja watavuruga upelelezi. Kwa hili hsraka ilikuwa ya nini, kama siyo kuscore matakwa ya kunfi fulani? Wapelelezi wenye weledi katika tukio kama hili cha kwanza kufanya baada ya kuwasaidia mahanga/waathirika ni kuhifadhi sehemu ya tukio na kuhakikisha vitu vyote vilivyopo hapo havichafuliwi. Hapa kwetu hiki hakifanyiki, wakifika wstu hapa na hasa viongozi, wakiwemo viongozi wa polisi wote ni wajuzi. Watagusa kila kitu na kujidai kutoa maelexo ambayo mengine hata hayana maana. Nilishangaa jana kumsikia Waxiri Mkuu akiagiza madakitari kuhakikisha chembechembe za vyuma vinavyotolewa kwenye miili ya waathirika viifadhiwe vizuri kwa uchunguzi! Hii haihitaji Waziri Mkuu kuagiza adharani, wapelelezi wanapaswa kufanya kazi na madaktari siyo tu kupata vyuma hivyo hata aina ya majeraha.Jana wakati Bunge linapitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani nilishangaa sana wabunge kupinga hoja ya kuliunda upya. Nani wakiwemo hao wabunge hawajui muunfo wa polisi ulivyokuwa compromised na kuwafanya wasifanye kazi yao kwa weledi na ufanidi? Nani hajui jinsi polisi wanavyobambnikizia watu kesi za ajabu? Taarifa ya habari ya ITV saa mbili leo inaonyesha kiundfi cha polisdi kinambambikizia mtu kesi ya mfanyabiashara kukutwa na kichwa cha mtu (walichokiweka wao) huko Morogoro - na hii pengine ni kutaka kuwaonyesha hao wabunge hali halisi!Tusiingize siasa kwenye vyombo vyetu vya usalama polisi, TISS na JW.
Kwa msimamo wa viongozi wetu wa sasa, mtu mwovu anaangaliwa kwanza dini yake halafu itikadi yake ya kisiasa. Vyombo vyetu vya usalama lazima viepuke mtizamo huo kwa gharama yoyote. Mwovu ni mwovu akiwa Muislamu au akiwa Mkristo. Akiwa shehe au akiwa Askofu! Nadhani sababu ya kutaja harakaharaka jina la Dereva wa bodaboda na kuwaacha wengine ni kwa kuwa ni Mkristo. Tayari hadi hapo mmeshanasa. Aliyeshiriki ugaidi huo ni gaidi tu bila kujali dini yake. Msijaribu hata kubalance kama ambavyo viongozi wetu wanavyofanya. Msifikie mahali pa kusema magaidi wale nusu ni waislamu na nusu ni wakristo. Ni wauwaji tu bila kujali dini zao. Tumeona dalili za kushughulikia matatizo ki hivyo. Makanisa yamechomwa lakini badala ya kuwakamata wahalifu inasemwa, lakini hata misikiti imechomwa pia. Wote hao ni wahalifu. Msiangalie wamevaa nini! Anasakwa Shehe Ilunga lakini na Askofu Mpemba pia. Inafungiwa radio Iman ilakini na redio Kwa neema FM pia. Kanisa linalipuliwa anatajwa mtu mkristo na wengine hawatajwi. Na huenda huyu alikuwa dereva tu. Kama mtakuwa mnamtafuta mhalifu na kunshughulikia bila kuangalia dini yake mtarudisha heshima yenu ambayo inaning'inia karibu kutumbukia shimoni. Mara ngapi wakati wa vurugu mmewagandamiza chadema kwa sababu ya itikadi ya kisiasa tu? Haya!!!!!
 
Mkwawa umenena. Nilishajiuliza humu haraka ya kutaja lile jina moja ilikuwa ya nini? Siku zote polisi wetu hawana haraka kabisa ya kutaja majina ya watuhumiwa, wakati mwingine mpaka wanapowafikisha mahakamani, sababu ikiwa wakitaja watavuruga upelelezi. Kwa hili hsraka ilikuwa ya nini, kama siyo kuscore matakwa ya kunfi fulani? Wapelelezi wenye weledi katika tukio kama hili cha kwanza kufanya baada ya kuwasaidia mahanga/waathirika ni kuhifadhi sehemu ya tukio na kuhakikisha vitu vyote vilivyopo hapo havichafuliwi. Hapa kwetu hiki hakifanyiki, wakifika wstu hapa na hasa viongozi, wakiwemo viongozi wa polisi wote ni wajuzi. Watagusa kila kitu na kujidai kutoa maelexo ambayo mengine hata hayana maana. Nilishangaa jana kumsikia Waxiri Mkuu akiagiza madakitari kuhakikisha chembechembe za vyuma vinavyotolewa kwenye miili ya waathirika viifadhiwe vizuri kwa uchunguzi! Hii haihitaji Waziri Mkuu kuagiza adharani, wapelelezi wanapaswa kufanya kazi na madaktari siyo tu kupata vyuma hivyo hata aina ya majeraha.Jana wakati Bunge linapitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani nilishangaa sana wabunge kupinga hoja ya kuliunda upya. Nani wakiwemo hao wabunge hawajui muunfo wa polisi ulivyokuwa compromised na kuwafanya wasifanye kazi yao kwa weledi na ufanidi? Nani hajui jinsi polisi wanavyobambnikizia watu kesi za ajabu? Taarifa ya habari ya ITV saa mbili leo inaonyesha kiundfi cha polisdi kinambambikizia mtu kesi ya mfanyabiashara kukutwa na kichwa cha mtu (walichokiweka wao) huko Morogoro - na hii pengine ni kutaka kuwaonyesha hao wabunge hali halisi!Tusiingize siasa kwenye vyombo vyetu vya usalama polisi, TISS na JW.

Mkuu umenena......siasa imevuka mipaka Tanzania....kila kitu ni siasa...hadi hali ya hewa....ni vema vitu vinavyohitaji utaalam visemwe na wataalam.....sijafurahishwa na mh waziri mkuu kutoa maelekezo ya kitaalam kwa madaktari kuhusu ukusanyaji wa vielelezo vya uchunguzi wa tukio hili.....kungekuwa na ushirikiano wa moja kwa moja kati ya wapelelezi, madaktari na mashahidi wa tukio bila kupititia kwa wanasiasa.....
 
Mara zote huwa najaribu kulinganisha mambo nayoyaona kwenye movie za holywood au hata tamthiliya ya isidingo tu then nalinganisha na zile show na tambo za mshereheshaji pale uwanja wa taifa najumlisha tena tambo za hao mabwana bar za uswailini"Unajua mi ni nani?"Huku akitoa kitambulisho au bastola basi nachoka naishiwa nguvu kabisa. Kwa maelekezo yale ya pm achilia mbali kuwa alikuwa usalama napata shaka hata kama aliwah soma vitabu vya Elvis Musiba vya Willy Gamba.
 
Mkuu umenena......siasa imevuka mipaka Tanzania....kila kitu ni siasa...hadi hali ya hewa....ni vema vitu vinavyohitaji utaalam visemwe na wataalam.....sijafurahishwa na mh waziri mkuu kutoa maelekezo ya kitaalam kwa madaktari kuhusu ukusanyaji wa vielelezo vya uchunguzi wa tukio hili.....kungekuwa na ushirikiano wa moja kwa moja kati ya wapelelezi, madaktari na mashahidi wa tukio bila kupititia kwa wanasiasa.....
Nimeangalia taarifa ya habari ya saa mbili ITV daktari akieleza ilivyokuwa vigumu kutoa chembechembe za. Yuma. Ilivyoko kwa majeruhi kwa vile. Viliishia kwenye nyama. Nikajiuliza uhusiano wa ili na agizo la jana la Waxiri Mkuu. Bahati mbaya kila mwanasiasa na viongozi sasa wanataka kuonekana jinsi walivyo na huruma na wanavyofanya kaxi kwa bidii!
 
Hakuna Mtanzania masikini raia wa kawaida awe mkristu, muislamu au dini yeyote mwenye chuki ya kuuwa wenzeka. Wengi wenye chuki hizi ni wale wenye uwezo, madaraka, wasomi, na wenye uchu wa madaraka yawe ya dini, siasa, biashara nk.

Damn True...!
 
Back
Top Bottom