Bilal Waikela ni nani?

Bilal Waikela ni nani?

Bwana Mohamed Said "upuuzi" hapa halikuwa tusi ni kinyume cha hoja yenye mantiki ile isiyo na maana ndio upuuzi sio tusi kamwe!! We ndugu yangu nilichosema mimi sio kuwa hatupendi au hatuwaenzi wapigania uhuru wetu la hasha!! Tena ifike mahali wapewe hadhi ya manabii wetu lakini katika context ya Utaifa na sio udini au ukabila Kaka!! Waikela kama yeye ni shujaa wa kumtoa mkoloni kwangu na naamini kwa Watanzania wengi ni mtu muhimu sana bila kujali dini yake au kabila lake. Hapo pia, haitegemei kutembelewa kwake na "mwanasiasa kijana aliye mashuhuri - Zitto Kabwe". Historia yetu imeandikwa na wageni sisi ndio sasa tunaamka kama anavyotaka kuamka rafiki yangu Paskali. Kama hao mashujaa hawakuthaminiwa au hawakutanjwa kwenye historia basi isiwe kuwa tuone ni kwa ajili ya dini zao bali tu kwa ajili ya kile walichokuwa wanakipigania ambacho mgeni alieandika historia hakukipenda. Wewe kama kijana wa sasa rekebisha ukisisitiza Utaifa na sio udini.
Mimi namuelewa mzee MOHAMEDI SAID lkn hebu sasa eleza usahihi wa kile unachokijua wewe, Mzee wangu Mohamedi yeye hicho unchotaka akiseme hakijui eleza wewe hiyo historia itakayoutenga uislm ma harakati za uhuru. Historia yetu inayowaficha wapigania uhuru ingewaficha wote basi na sio hao akina waikela peke yao. Na kama waliofichwa na watu wanaolekea kuwa na mlengo mmoja tu wakiitikadi basi tuseme huyo mgen alikuwa na ajenda yake ya dini na ndicho kinchopelekea kuleta huo mkanganyiko.
 
Bwana Mohamed Said "upuuzi" hapa halikuwa tusi ni kinyume cha hoja yenye mantiki ile isiyo na maana ndio upuuzi sio tusi kamwe!! We ndugu yangu nilichosema mimi sio kuwa hatupendi au hatuwaenzi wapigania uhuru wetu la hasha!! Tena ifike mahali wapewe hadhi ya manabii wetu lakini katika context ya Utaifa na sio udini au ukabila Kaka!! Waikela kama yeye ni shujaa wa kumtoa mkoloni kwangu na naamini kwa Watanzania wengi ni mtu muhimu sana bila kujali dini yake au kabila lake. Hapo pia, haitegemei kutembelewa kwake na "mwanasiasa kijana aliye mashuhuri - Zitto Kabwe". Historia yetu imeandikwa na wageni sisi ndio sasa tunaamka kama anavyotaka kuamka rafiki yangu Paskali. Kama hao mashujaa hawakuthaminiwa au hawakutanjwa kwenye historia basi isiwe kuwa tuone ni kwa ajili ya dini zao bali tu kwa ajili ya kile walichokuwa wanakipigania ambacho mgeni alieandika historia hakukipenda. Wewe kama kijana wa sasa rekebisha ukisisitiza Utaifa na sio udini.
Kokola,
Wala sitakulaumu kwa kuona neno ''upuuzu,'' si tusi na mara nyingi
lugha mfano na hii yako nakutananayo hapa jamvini.

Kwetu siye hilo ni tusi.

Ingekuwa mimi ningeweza kuandikia sentesi hiyo hiyo bila ya kutumia
neno, ''upuuzi.''

Tofauti kati yangu mimi na wewe ni kuwa mimi kwanza ingawa hii nini
historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kubwa ni kuwa historia hii
imewahusu wazee wangu.

Kwa ajili hii basi mimi nayajua mengi ambayo wewe huyajui.

Ukweli ni kuwa palikuwapo na bado ipo njama ya kuifuta historia hii
na laiti kama nisingeliandika historia hii mengi yasingejulikana.

Hili la Uislam katika historia ya TANU huwezi kuliepuka hata ukifanya
nini kwa kuwa ndiyo historia yenyewe ilivyokuwa na mifano iko wala
si ya kutafuta.

Waasisi wa African Association 1929 ndiyo hao walioasisi Al Jamiatul
Islamiyya Fi Tanganyika 1933.

Al Jamiatul Islamiyya ndiyo iliyotoa viongozi wa mwanzo wa TANU na
wanachama wake.

Mimi sijaona ubaya wowote katika kuandika historia hii.

Idd Faiz Mafungo kadi yake ya TANU ni No. 25 na yeye ndiye alikuwa
mweka hazina wa Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika na pia mweka
hazina wa TANU.

Idd Faiz ndiye aliyekuwa mkusanyaji wa fedha za kumpeleka Nyerere UNO
mwaka wa 1955.

Umepata popote kumsikia akitajwa?
 
Mimi namuelewa mzee MOHAMEDI SAID lkn hebu sasa eleza usahihi wa kile unachokijua wewe, Mzee wangu Mohamedi yeye hicho unchotaka akiseme hakijui eleza wewe hiyo historia itakayoutenga uislm ma harakati za uhuru. Historia yetu inayowaficha wapigania uhuru ingewaficha wote basi na sio hao akina waikela peke yao. Na kama waliofichwa na watu wanaolekea kuwa na mlengo mmoja tu wakiitikadi basi tuseme huyo mgen alikuwa na ajenda yake ya dini na ndicho kinchopelekea kuleta huo mkanganyiko.
Ndugu Expirience man nachotaka kusema nishasema labda hujakielewa hilo moja, pili kama hao wageni walikuwa na ajenda ya kidini je sisi katika kurekebisha makosa yao ndio tuegemee kwenye ajenda ya udini pia..? Hekima hiyo unavyoona wewe!!! Na haswa ukizingatia udini huo unachangia kutugawa na hivyo kutudhoofisha..?!!
 
Paskali rudia kunisoma ili uelewe nilichoandika. Hakuna mahali niliposema Rashid Kheri Bagdelleh alimtia kizuizini Bilal Waikela. Waikela pamoja na babu yangu na Sheikh Jumanne Bias waliwekwa kizuizini chini ya Dentation Act ya 1962. Nikuongeze kitu. Bagdelleh alikuwa rafiki ya baba yangu na akija nyumbani kwetu.
Mkuu, Heshima kwako. Kikawaida Historia inapogusa mambo ambayo wengi hatuyapendi huwa inaleta ukakasi hata katika kuisoma. Yupo soko la mitumba Manzese mwanae Mzee Waikela anaitwa Ramadhani Waikela Pasco anaweza kumtafuta atapata anayoyataka maana Mzee Waikela hakuwa na khofu kuusimulia ukweli kwa yeyote maisha yake yote.
 
Ndugu Expirience man nachotaka kusema nishasema labda hujakielewa hilo moja, pili kama hao wageni walikuwa na ajenda ya kidini je sisi katika kurekebisha makosa yao ndio tuegemee kwenye ajenda ya udini pia..? Hekima hiyo unavyoona wewe!!! Na haswa ukizingatia udini huo unachangia kutugawa na hivyo kutudhoofisha..?!!
Mkuu udini Tanzania haukwepeki kama Kompyuta zilivyokosea katika kufelisha waislamu!! Mkuu Ukabila pia haukwepeki kama bado tunabaguana kwa makabila "hawa wa kaskazini hawafai kuongoza... hawa vibalagashia hawakusoma nk!!"
 
Ndugu Expirience man nachotaka kusema nishasema labda hujakielewa hilo moja, pili kama hao wageni walikuwa na ajenda ya kidini je sisi katika kurekebisha makosa yao ndio tuegemee kwenye ajenda ya udini pia..? Hekima hiyo unavyoona wewe!!! Na haswa ukizingatia udini huo unachangia kutugawa na hivyo kutudhoofisha..?!!
unakwepaje historia ya uislam ktk uhuru wakat hata hao wapigania uhuru mwanzo walikutana kwenye hizo taasisi za dini na kuanzia harakati huko hapa ipo taasisi kama JAMIIATUL ISLAMIYA FI TANGANYIKA. Najua historia ikiongea mambo usoyapenda utapinga tu lkn ndo inabaki kuwa historia tu. Hata mtu akikambia baba yako mzazi aliyekuzaa alikua mlevi hutopenda kusikia historia hiyo. hebu mfuate bilalal waikera anaijua historia kuliko wewe ulioyosoma ya magogoni ya kuinjinia hiyo!!
 
unakwepaje historia ya uislam ktk uhuru wakat hata hao wapigania uhuru mwanzo walikutana kwenye hizo taasisi za dini na kuanzia harakati huko hapa ipo taasisi kama JAMIIATUL ISLAMIYA FI TANGANYIKA. Najua historia ikiongea mambo usoyapenda utapinga tu lkn ndo inabaki kuwa historia tu. Hata mtu akikambia baba yako mzazi aliyekuzaa alikua mlevi hutopenda kusikia historia hiyo. hebu mfuate bilalal waikera anaijua historia kuliko wewe ulioyosoma ya magogoni ya kuinjinia hiyo!!
 
Asalaam aleikum maalim.
Nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa makala na maandiko yako mengine.Hongera sana kwa kuutangaza na kuutetea umma was kiislamu ingawa historia "ya pili" imekuwa ni kikwazo katika hili.
Naamini Allah (s.w) ataendelea kukuongoza udumu katika kheri.Inshaallah.
Pamoja na hayo, natamani kupata nakala(hata soft copy) za maandiko yako.
Hili suala naona watu mnalipeleka kwenye udini.kwani kama waislamu walishiriki kupigania Uhuru wetu,je kulikuwa na makubaliano waliyowekeana kwamba baada ya Uhuru waislamu wapewe upendeleo na nchi hii iwe na sheria za kiislamu?
Kama hakukuwa na makubaliano lawama za waislamu zinatoka wapi.tukumbuke pia harakati za Uhuru sio kweli kwamba wakristo hawakushiriki kabisa walishiriki mfano ni Mwl Nyerere.
Wakati tunapata Uhuru kanisa la wasabato Tanzania ndilo lililokuwa na mashule mengi kuliko makanisa yote hapa Tanzania wakati huu.
Serkali chini ya mwalimu Nyerere ikazitaifisha shule zote za kanisa LA wasabato na kuzifanya za serkali.mbona wasabato hawalalamiki kwamba wanaonewa na serkali. Ebu tuweke utaifa Mbele tuache udini
 
Bwana Mohamed Said "upuuzi" hapa halikuwa tusi ni kinyume cha hoja yenye mantiki ile isiyo na maana ndio upuuzi sio tusi kamwe!! We ndugu yangu nilichosema mimi sio kuwa hatupendi au hatuwaenzi wapigania uhuru wetu la hasha!! Tena ifike mahali wapewe hadhi ya manabii wetu lakini katika context ya Utaifa na sio udini au ukabila Kaka!! Waikela kama yeye ni shujaa wa kumtoa mkoloni kwangu na naamini kwa Watanzania wengi ni mtu muhimu sana bila kujali dini yake au kabila lake. Hapo pia, haitegemei kutembelewa kwake na "mwanasiasa kijana aliye mashuhuri - Zitto Kabwe". Historia yetu imeandikwa na wageni sisi ndio sasa tunaamka kama anavyotaka kuamka rafiki yangu Paskali. Kama hao mashujaa hawakuthaminiwa au hawakutanjwa kwenye historia basi isiwe kuwa tuone ni kwa ajili ya dini zao bali tu kwa ajili ya kile walichokuwa wanakipigania ambacho mgeni alieandika historia hakukipenda. Wewe kama kijana wa sasa rekebisha ukisisitiza Utaifa na sio udini.
Tena dini zenyewe bora hata zingekuwa zetu kweli.

Zote za kuletewa na meli.

Zote zina mambo tofauti sana na tamaduni zetu.

Na tumezibugia kama mtu mwenye njaa kwenye dhifa.
 
unakwepaje historia ya uislam ktk uhuru wakat hata hao wapigania uhuru mwanzo walikutana kwenye hizo taasisi za dini na kuanzia harakati huko hapa ipo taasisi kama JAMIIATUL ISLAMIYA FI TANGANYIKA. Najua historia ikiongea mambo usoyapenda utapinga tu lkn ndo inabaki kuwa historia tu. Hata mtu akikambia baba yako mzazi aliyekuzaa alikua mlevi hutopenda kusikia historia hiyo. hebu mfuate bilalal waikera anaijua historia kuliko wewe ulioyosoma ya magogoni ya kuinjinia hiyo!!
Experience...
Sheikh Hassan bin Amir ndiye alikuwa aMufti wa Tanganyika katika
miaka ile ya 1950.

Mwaka wa 1950 TAA ndani yake ilianzisha kamati iloiyopewa jina la
TAA Political Sub Committee.

Sheikh Hassan bin Amir alikuwa mmoja wa wanakamati hii, wengie
ni Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando, John Rupia,
Sheikh Said Chaurembo.

Kamati hii ndiyo iliyoweka mipango ya kuunda TANU na TANU ilipoasisiwa
mwaka 1954, Sheikh Hassan bin Amir akawa anauza kadi za TANU
msikitini.

Mtoro Rehani aliuziwa kadi ya TANU na Sheikh Hassan bin Amir ndani
ya msikiti.

Haiwezekani ukaandika historia ya TANU na haya yakwa hayapo.
Hii ndiyo historia yenyewe ya TANU.
 
Tena dini zenyewe bora hata zingekuwa zetu kweli.

Zote za kuletewa na meli.

Zote zina mambo tofauti sana na tamaduni zetu.

Na tumezibugia kama mtu mwenye njaa kwenye dhifa.[/QUOTE
Al Watan,
Mimi sijaandika habari za dini ya Kiislam nimeandika historia ya Waikela.
Sijui hizi habari za dini na ''kuletwa na meli,'' zinaingiaje hapa.
 
Ndugu Expirience man nachotaka kusema nishasema labda hujakielewa hilo moja, pili kama hao wageni walikuwa na ajenda ya kidini je sisi katika kurekebisha makosa yao ndio tuegemee kwenye ajenda ya udini pia..? Hekima hiyo unavyoona wewe!!! Na haswa ukizingatia udini huo unachangia kutugawa na hivyo kutudhoofisha..?!!
Ukweli haudhoofishi bali utatufanya tuwe imara zaidi kama Marekani pamoja historia ya utumwa, bado weupe na weusi wanajenga nchi yao
 
Hili suala naona watu mnalipeleka kwenye udini.kwani kama waislamu walishiriki kupigania Uhuru wetu,je kulikuwa na makubaliano waliyowekeana kwamba baada ya Uhuru waislamu wapewe upendeleo na nchi hii iwe na sheria za kiislamu?
Kama hakukuwa na makubaliano lawama za waislamu zinatoka wapi.tukumbuke pia harakati za Uhuru sio kweli kwamba wakristo hawakushiriki kabisa walishiriki mfano ni Mwl Nyerere.
Wakati tunapata Uhuru kanisa la wasabato Tanzania ndilo lililokuwa na mashule mengi kuliko makanisa yote hapa Tanzania wakati huu.
Serkali chini ya mwalimu Nyerere ikazitaifisha shule zote za kanisa LA wasabato na kuzifanya za serkali.mbona wasabato hawalalamiki kwamba wanaonewa na serkali. Ebu tuweke utaifa Mbele tuache udini
Tunene,
Hili la makubaliano umelitoa wapi?
Wapi imesemwa kuwa Waislam wanataka upendeleo?

Wapi zimelelezwa habari za Wasabato na shule zao?
Hapa mimi nimeeleza historia ya Bilal Rehani Waikela.

Ikiwa unataka tujadili kutaifishwa kwa shuke basi funguo
uzi mwingine.
 
Pascal,
Ni vigumu kueleza historia ya Mzee Waikela katika mahali kama hapa JF
kwa ajili ya nafasi.

Kwani historia yake inaanza 1955 wakati wa kuunda TANU Tabora hadi
kufika kupatikana kwa uhuru mwaka wa 1961 yeye akiwa mshiriki mkuu
katika historia yenyewe ya kwanza kuundaTANU na kushiriki katika matukio
makubwa ya wakati ule kama Kura Tatu ya 1958 yeye akiwa kijana.

Mzee Waikela wakati ule alikuwa pia ni kiongozi wa EAMWS akiwa katibu
wa Western Province na mfuasi wa Mufti wa Tanganyika, Sheikh Hassan
bin Amir.


Nilipokwenda kuonana na Mzee Waikela, hakuwa peke yake aliwaita wazalendo
wenzake, Abdallah Kassongo, Mohamed Mangiringiri na Ramadhani
Singo.

Sijapatapo kukutana wana TANU waliokuwa wanaijua historia ya chama chao na
wakaieleza kwa utulivu na ufasaha kama watu hawa.

Baada ya hahojiano haya Mzee Waikela akanita pembeni mimi na walionisindikiza
kwake, marehemu Sheikh Ilunga Hassan Kapungu na shemeji yake Salum
Mkangwa
.

Mzee Waikela alituambia turejee kesho atueleze yale yaliyotokea baada ya uhuru
kupatikana mwaka wa 1961.

Nilirejea na wenyeji wangu siku ya pili na Mzee Waikela alifunguka.
Alizungumza kwa takriban saa tatu sote tukiwa kimya tukimsikiliza.

''Mohamed mimi niliwekwa kizuizini jela ya Uyui mwaka wa 1964 na babu yako, Mkuu
wa Jela akiwa Bwana Munthali na Regional Commissioner akiwa Rashid Kheri
Bagdelleh,
ilikuwa mwezi wa Ramadhani na walinifuata usiku kunikamata na ndiyo
kwanza nilikuwa naanza kula daku....''

Mazungumzo yale na Mzee Waikela ndiyo yaliyotengeneza sehemu ya tatu katika
kitabu cha Abdul Sykes na sehemu hiyo nikaipa jina, ''Njama Dhidi ya Uislam (1961 -
1970).

Tulipomaliza mahojiano nilimwambia Mzee Waikela, ''Mzee Waikela umenieleza habari
nzito sana na za kutisha mimi nataka unifahamishe ikiwa unanipa ruhusa ya kukutaja
wewe kwa jina kuwa hizi taarifa chanzo chake ni wewe.''

''Nitaje bila hofu waeleze kuwa hizi habari nimekupa mimi Bilal Rehani Waikela.''

Tulipokuwa tunaagana, Mzee Waikela alinyanyua mikono juu akaniombea dua ndefu
sana na akaniambia, ''Mohamed kitabu kitoke Waislam waujue ukweli wa historia yao
kisiishie katika makaratasi.''
Nimejikuta roho imeniuma sana kusoma ukurasa huu sijui kwann, dah mungu unusuru uisilam na watu madhalimu
 
Al Watan,
Mimi sijaandika habari za dini ya Kiislam nimeandika historia ya Waikela.
Sijui hizi habari za dini na ''kuletwa na meli,'' zinaingiaje hapa.

Hujaandika kwa msisitizo wa habari za Waislamu?

Kwa nini uislamu uwe muhimu sana?
 
Hujaandika kwa msisitizo wa habari za Waislamu?

Kwa nini uislamu uwe muhimu sana?
Al Watan nimeandika kitabu kizima ambacho kinaitwa, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes the Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika." Umuhimu wake ni kuwa walijitolea kupambana na ukoloni.
 
Al Watan nimeandika kitabu kizima ambacho kinaitwa, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes the Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika." Umuhimu wake ni kuwa walijitolea kupambana na ukoloni.
Kwa watu wanaotaka kujenga umoja wa kitaifa, kuanza kuwagawa Watanganyika kwa mafungu ya kidini ni kuharibu umoja wa kitaifa.

Unawaambia wao si wamoja. Kuna waislamu na wakristo.

Sasa hapo kwenye waislamu napo aje mtu aandike kuhusu mchango wa Shia. Wa Shia nao watuambie Wa Ismaili na Zaydi nao walikuwa na mchangi wao tofauti.

Mimi naamini katika kuandika historia, maadam kilichoandikwa ninkweli, lakini naamini pia kwamba unaweza kuandika historia ikaleta kupinda ukweli.

Hususan kama historua yenyewe imekitwa kwenye hizi "imagined realities" za dini za kutungwa.

Hapo ndipo mnapowapa msemo wale watu wanaosema kwamba nia ya Uislamu ni kutawala dunia na popote pale ambapo uislamu haujatawala, utataka kunung'unika na kuua mpaka utawale.

Kwamba mnanung'unika sio kwa sababu mmeonewa (Wasabato wameonewa, makanisa yamenyang'anywa shule etc lakini hatuwasikii wakilalamika kama nyinyi) ila mnalalamika kwa sababu mmefundishwa kuchukua nchibkwa upanga na kueneza dini dunia nzima kama ilivyoenea kutoka Uarabuni mpaka Spain.
 
Al Watan wapi nimesema maneno hayo? Hii ni historia ya waliopigania uhuru wa Tanganyika. Hayo mengine mimi siyajui.
 
Back
Top Bottom