Bilionea Laizer asimzoee sana Millard Ayo na waandishi, akumbuke ya Askofu alipoishia na mabilioni

Huyu mmasai hili bilioni 8 haitachukua raundi unajua hela ina watu wake. Hela sio ngo'ombe ina akili zaidi ya ng'ombe.

Futa mawazo haya!

Baada ya kusikia taarifa zake ni kwamba huyu jamaa ni tajiri siku nyingi tu, kama alishaanza kujenga MALL yenye makadirio ya Bilioni 6 tangu 2017 hebu fikiria vizuri.

Amewekeza pesa nyingi mno hadi kufika hapo, na hata huo mgodi anaendesha kwa pesa nyingi tu... kwahiyo hizi 7.8 ni mstuko kwetu ila sio kwake hata kama hajawahi kuzishika kwa mkupuo.

Binafsi hata simjui, nami nimesikia tu!
 
Msichojua ni kuwa production yote inaweza kufanywa kwa siku moja,halafu anaachia vipande wiki nzima
Kingine huyo.Ayo nae ni mmasai,inawezekana na ujamaa na ndio mana aliweza kuwa wa kwanza kufanya exclusive interviewa
Ayo ni mmeru, ila wamasai na wameru ni majirani na kuna baadhi ya mila zao zinafanana.
 
Mwacheni dogo achukue hela kungali mapema, hili laizer akija kushituka basi wawe wamempiga vya kutosha.

Ila unaweza kujiuliza ni story gani kila siku waandishi wanajazana kule mirerani?
Jana wameenda kula nyama kwenye sherehe aliyoandaa laizer kwa ndugu, jamaa na marafiki zake.
 
Ayo naye amezidi sasa habari za nyumba za wake wa bilonea sio inshu kwetu aende basi pale muhimbili aulizie kinachoendelea kati ya wale majeruhi 30 waliosalia ktk ajali ya lorry la mafuta morogoro
 
naona kama ushamba fulani hivi. kama nimepiga hela sasa waandishi wanahusikaje. kwani hii biashara?
watu wanaacha kutangaza mambo ya msingi unafuatilia wake za watu
 
Ukimuangalia kwa makini Laizer yuko makini sana.hana papara wala mbwembwe kama askofu wa Arusha.
 
YAAN ANAONESHA NJAA ZA WAZI UKIFUNGUA KUPATA HABARI MPAKA LEOHII N LAISER KACHINJA NGOMBE ULITAKA ACHINKE WAKEZAKE??KILA ANACHOFANYA LAISER MTAKIONA HOPE SIKU TUTAONA KITANDA CHAKE ANACHOLALIA
Ni Mbabaikaji fulani kwnza watu wa mawe hawapendi promo hizo eti anamuliza Vp mzee utanunua hammer???
Kijamaa kinaboa sana ki front front sana

Ova
 
Jamani si nae yupo Kazini Kwake au? Huwa simkubali kivile Milard Ayo kutokana na Nyeti moja Kumhusu Yeye, ila kwa hili naona mnamuonea tu.
Mkuu itoe hiyo nyepesi nyepesi ya Millard ayo ilikuwa vipi
 
Mkuu itoe hiyo nyepesi nyepesi ya Millard ayo ilikuwa vipi

Acha Upumbavu Mtu akishakuambia kuwa Maadili yanamzuia kuendelea zaidi ya hapo uwe unamuelewa. Wabongo mnaendekeza sana tu Umbea!
 
Mwacheni Ayo lizer afanye kazi kama anaona sehemu kuna ulaji kwanini asiwepo!
 
Kumbe ule mzigo sio wake peke yake nasikia kuna mchimbaji mwenzake watagawana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…